Chee4
Member
- May 17, 2021
- 35
- 125
Kuna Msemo usemao Roma Haikujengwa kwa Siku moja. Msemo huu inaonekana wengi huwa hawauelewi.
Msemo huu pamoja na tafsiri nyingi unaimanisha kuwa Uzuri wa Roma katika kila nyanja ulichukua muda mwingi kujengwa kupitia kodi na nguvu nyingi za watu wa taifa ile.
Nimeona nianze na msemo huu kuonesha kuwa sisi watu wa Mombasa tumeanza kukerwa na kelele za wapinzani wa Tanzania na watanzana wasiojua maendeleo yanakujaje kupinga tozo na kodi mbalimbali ambazo zimewekwa ili kujenga miundo mbinu ya barabara, shule na hospitali.
Watanzania lazima muamke msisikilize kelele za wapinzani kwani bila nyie kujenga nchi yenu kwa jasho lenu mikopo ya wazungu itawaacha maskini na kamwe hamtafurahia matunda ya uhuru wenu mlioupata tangu mwaka 1961.
Kwetu sisi Tanzania ni kama kioo kwa sababu viongozi wengi tangu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere hadi leo Mama Samia Hassan wamewajengea dhana nzuri ya kujitegemea kupitia kodi zenu.
Nyote ni mashahidi kuwa bila kulipa kodi hakuna chochote mtakachojifanyia mtabaki kukopa na mtanuka madeni.
Tunayo mifano mingi ya namna mataifa mbalimbalimbali yalitumia kodi ya wananchi kujenga nchi zao na leo mataifa hayo baada ya kupata maendeleo ndo yanasaidia nchi zetu na kutuita maskini.
Nchi ya kwanza ni China ambayo miaka ya 70 ilikuwa na maendeleo kama ya Tanzania. Nchi hii ikaweka mageuzi makubwa ya kimfumo iliyohusisha pamoja na mambo mengine kutumia vizuri kodi za wananchi.
China ikajenga miundo mbinu ya barabara hadi vijijini na mashambani wakulima wakapata kupeleka mazao yao viwandani na watu wakaweza viwanda vijijini leo hii China ndo mkopeshaji mkubwa wa nchi zote duniani.
Sio hiyo tu juzi hapa wakati nchi hiyo inasherekea miaka 100 ya tangu kuanzishwa Chama cha Kikomunisti cha China Rais wa nchi hiyo alitangaza kuwa China sio maskini tena.
Kama hiyo haitoshi juzi tu hata mwezi haujapita Rais wa Marekeni Joe Biden aliomba bunge liidhinishe dola trilioni mbili kujenga miundo mbinu ya barabara ili kujenga uchumi. Japo hakupewa kiwango chote lakini alipewa theluthi tatu ya hela hiyo.
Tofauti na Tanzania Marekani imeishakusanya hiyo kodi wanapanga matumizi nyie Tanzania ndo mnakusanya mpange matumizi.
Ninachowaambia watanzania acheni kusikiliza wanaharakati na wanasiasa wanaotaka kuwakwamisha. Makundi haya yanapewa hela nyingi kupinga maendeleo ili kuzifanya nchi za Afrika ikiwemo Tanzania kuendelea kuwa wategemezi.
Nyie watanzania ni mashahidi mliona katika uchaguzi wa wenu wa mwaka jana CHADEMA, wanaharekati na watetezi wa haki za binadamu walivyowapa wakati mgumu kushirikiana na baadhi ya watu wa mataifa ya nje kuvuruga uchaguzi wenu.
Mtakumbuka Tundu Lissu aliyekuwa Mgombea kupitia CHADEMA alivyoshirikiana na Robert Amsterdam wakili wa kimataifa kutaka kuyumbisha Tanzania kwa maslahi yao.
Leo baada ya Rais wenu mama Samia kuomba kodi ajenge nchi watu walewale wameanza fujo na kelele nyingi kukataa kodi zisilipwe, kudai katiba na kutaka kuanza maandamano nchi nzima ya Tanzania.
Yote haya wanayafanya kwa niaba ya watu wasioitakia maendeleo Tanzania.
Watanzania ninawaasa muamini Rais wenu tena Mama Samia atawavusha.
Akina mama huwa hawasemi uongo kwa sababu Mungu aliwaumba hivyo kulea watoto duniani.
Lipeni tozo za simu na kodi nyingine baada ya hapo ndo muanze kuuliza kama yaliyoaidiwa mkilipa hizo tozo yamefanywa au la.
Sisi wakenya tunawaonea wivu kwa sababu spidi ya Mama Samia nasi twaitamani lakini tunawatakia kila kheri watanzania.
Muungeni Mkono Mama Samia atawavusha kama alivyowaahidi.
Tanzania na miundo mbinu imara, shule za kutosha, hospitali na maji kwa kila mwananchi inawezekana. Lipa kodi kuwezesha hilo lifanyike.
Msemo huu pamoja na tafsiri nyingi unaimanisha kuwa Uzuri wa Roma katika kila nyanja ulichukua muda mwingi kujengwa kupitia kodi na nguvu nyingi za watu wa taifa ile.
Nimeona nianze na msemo huu kuonesha kuwa sisi watu wa Mombasa tumeanza kukerwa na kelele za wapinzani wa Tanzania na watanzana wasiojua maendeleo yanakujaje kupinga tozo na kodi mbalimbali ambazo zimewekwa ili kujenga miundo mbinu ya barabara, shule na hospitali.
Watanzania lazima muamke msisikilize kelele za wapinzani kwani bila nyie kujenga nchi yenu kwa jasho lenu mikopo ya wazungu itawaacha maskini na kamwe hamtafurahia matunda ya uhuru wenu mlioupata tangu mwaka 1961.
Kwetu sisi Tanzania ni kama kioo kwa sababu viongozi wengi tangu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere hadi leo Mama Samia Hassan wamewajengea dhana nzuri ya kujitegemea kupitia kodi zenu.
Nyote ni mashahidi kuwa bila kulipa kodi hakuna chochote mtakachojifanyia mtabaki kukopa na mtanuka madeni.
Tunayo mifano mingi ya namna mataifa mbalimbalimbali yalitumia kodi ya wananchi kujenga nchi zao na leo mataifa hayo baada ya kupata maendeleo ndo yanasaidia nchi zetu na kutuita maskini.
Nchi ya kwanza ni China ambayo miaka ya 70 ilikuwa na maendeleo kama ya Tanzania. Nchi hii ikaweka mageuzi makubwa ya kimfumo iliyohusisha pamoja na mambo mengine kutumia vizuri kodi za wananchi.
China ikajenga miundo mbinu ya barabara hadi vijijini na mashambani wakulima wakapata kupeleka mazao yao viwandani na watu wakaweza viwanda vijijini leo hii China ndo mkopeshaji mkubwa wa nchi zote duniani.
Sio hiyo tu juzi hapa wakati nchi hiyo inasherekea miaka 100 ya tangu kuanzishwa Chama cha Kikomunisti cha China Rais wa nchi hiyo alitangaza kuwa China sio maskini tena.
Kama hiyo haitoshi juzi tu hata mwezi haujapita Rais wa Marekeni Joe Biden aliomba bunge liidhinishe dola trilioni mbili kujenga miundo mbinu ya barabara ili kujenga uchumi. Japo hakupewa kiwango chote lakini alipewa theluthi tatu ya hela hiyo.
Tofauti na Tanzania Marekani imeishakusanya hiyo kodi wanapanga matumizi nyie Tanzania ndo mnakusanya mpange matumizi.
Ninachowaambia watanzania acheni kusikiliza wanaharakati na wanasiasa wanaotaka kuwakwamisha. Makundi haya yanapewa hela nyingi kupinga maendeleo ili kuzifanya nchi za Afrika ikiwemo Tanzania kuendelea kuwa wategemezi.
Nyie watanzania ni mashahidi mliona katika uchaguzi wa wenu wa mwaka jana CHADEMA, wanaharekati na watetezi wa haki za binadamu walivyowapa wakati mgumu kushirikiana na baadhi ya watu wa mataifa ya nje kuvuruga uchaguzi wenu.
Mtakumbuka Tundu Lissu aliyekuwa Mgombea kupitia CHADEMA alivyoshirikiana na Robert Amsterdam wakili wa kimataifa kutaka kuyumbisha Tanzania kwa maslahi yao.
Leo baada ya Rais wenu mama Samia kuomba kodi ajenge nchi watu walewale wameanza fujo na kelele nyingi kukataa kodi zisilipwe, kudai katiba na kutaka kuanza maandamano nchi nzima ya Tanzania.
Yote haya wanayafanya kwa niaba ya watu wasioitakia maendeleo Tanzania.
Watanzania ninawaasa muamini Rais wenu tena Mama Samia atawavusha.
Akina mama huwa hawasemi uongo kwa sababu Mungu aliwaumba hivyo kulea watoto duniani.
Lipeni tozo za simu na kodi nyingine baada ya hapo ndo muanze kuuliza kama yaliyoaidiwa mkilipa hizo tozo yamefanywa au la.
Sisi wakenya tunawaonea wivu kwa sababu spidi ya Mama Samia nasi twaitamani lakini tunawatakia kila kheri watanzania.
Muungeni Mkono Mama Samia atawavusha kama alivyowaahidi.
Tanzania na miundo mbinu imara, shule za kutosha, hospitali na maji kwa kila mwananchi inawezekana. Lipa kodi kuwezesha hilo lifanyike.