Watanganyika amkeni usingizini

canular

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2018
Posts
1,068
Reaction score
1,268
Amkeni Watanganyika

Tafakari hali yetu ya sasa: Taifa letu limeuzwa, tumechukuliwa mamlaka ya kumchagua au kumuweka kiongozi. Sasa tuna watu ambao hatuwataki wala hatukuwachagua.

Haki hii ambayo ni halali kwa kila raia wa taifa letu kikatiba imechukuliwa kwa Bunduki na risasi, taifa limenunuliwa.

Hiii ni hali ya kutisha, lakini tunaweza kubadilisha kwa nguvu za umoja wetu.

Tarehe 9 Desemba 2025, tuchukue hatua za kusitisha wizi huu na uhuni huu walioufanya CCM.

Twendeni kwenye maandamano ya amani tuwapinge na kuwakataa kila sehemu kwa nguvu na sauti moja.

Tufanyeni maandamano, tujitokeze kila mmoja na bango lake kuonesha upinzani wetu kwa wale walio nunua nchi yetu.

Tukumbuke, Watanzania wenzetu wameuwawa na hawa majambazi wahuni wa ccm, tusikubali kudanganywa tena.

Pamoja, kwa umoja na mshikamano, tuwapinge vikali ccm na wote wale walionunua Taifa letu.

Tarehe 9 Desemba, tuipe ujumbe dunia nzima hatuko tayali kutawaliwa kwa bunduki na risasi pia hatuko tayari kutawaliwa na watu yaliojiweka madarakani
 
D9 Tunatoka na si kizembe....si kizembe
 

D9 anayebaki nyumbani ni mtoto mchanga, mama mjamzito, wagonjwa na wazee. Watanganyika wengine wote tutakuwepo 🫵
 
Tanganyila inatakiwa kuongozwa na kiongozi mzalendo! Na siyo mamluki kutoka nje, akishirikiana na wahuni wake wachache + familia yake. Hii siyo nchi ya Kisultani. Hivyo ukombozi wa kweli haukwepeki hiyo D9.
 
SOUTH SUDAN WALIPAMBANA MPAKA WAKAJITENGA NA SUDANI YA MAPONJORO
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…