Wataalamu Wa Maabara Tanzania

Wataalamu Wa Maabara Tanzania

gasozi

Member
Joined
Jun 8, 2019
Posts
25
Reaction score
26
Habari wanajukwaa,
Kuna hili suala la usajili wa wataalamu wa maabara Tanzania, hili ni jambo zuri ili kupata wataalam waliokidhi vigezo vya kutoa huduma.

Nina tatizo juu ya utaratibu unaotumika, wao husajili mtu kwa kumpa hati ya muda(provisional registration) ambayo huitumia kwa miezi kumi na mbili baada ya hapo huhitajika kufanya mtihani ili aweze kupata usajili kamili.

Ikumbukwe huyu mtu anakuwa ameshamaliza mitihani ya mwisho na kuifaulu kwa viwango vilovyowekwa na baraza.
Swali: Kuna ulazima gani wa kufanya mtihani baada ya mwaka mzima wa kuhitimu moduli zako zote ulizofaulu?

Maoni: Wizara iweke utaratibu wa kufanya mtihani huo pindi muhitimu anapokuwa anafanya mtihani wake wa mwisho ili kuondoa usumbufu wa kufanya mitihani mara mbili mbili kana kwamba wizara haziaminiani.
 
Shughulikeni na CORONA kwanza, haya mengine ya maslahi achana nayo kwanza maaana unatuchanganya tu.
 
kati yetu na kongo nani wakuchanganyukiwa,? Mkuu wa nchi kashasema shughul ziendelee
Shughulikeni na CORONA kwanza, haya mengine ya maslahi achana nayo kwanza maaana unatuchanganya tu.
 
haha dah ........sitaki kukumbuka mengi yalopita 😊🙌
 
Walikudaka nn??
Utakua na kimeo hadi leo huja clear!!!!

Komaaa mzee mtihan huo hatuwez utoa
Hahaa aah wapi ....

sijawah pata below 50 wala sup kipindi nipo chuo na wala sikukamatwa na hao na hawawezi hata watunge popote.....

sema t elimu yetu ina complications nyingi Sana halafu muda unapoteza , pesa na mwisho wa siku unabaki na mikaratasi yako kwenu... kuanzia academic , professional, intern certificate, leseni uloipata Kwa pepa na KAZI huna ....and NO BODY CARES...
 
Back
Top Bottom