Kwa siku mbili au tatu zilizopita nimekuwa nikifuatilia kwenye vyombo vya habari juu ya rai ya NEC kuwataka watu kuondoka kwenye vituo vya kupigia kura mara baada ya kupiga kura.
Katika jamii ya watu wastaarabu na wanaotendeana haki hivyo ndo inavyotakiwa kuwa. Katika makala yake Generali Ulimwengu kama wiki mbili zimepita alisema katika chaguzi za nchi za Afrika hatujafikia kiwango cha ustaarabu cha kutendeana haki.
Katika kudhihirisha hilo katika uchaguzi uliopita kama watu wangepiga kura wakarudi nyumbani leo hii mbunge wa Arusha mjini Lema asingekuwa mbunge. Wenje Nyamagana asingekuwa mbunge, Nasari asingekuwa mbunge. Wasimamizi walikuwa wakipewa presha watangaze watu walioshindwa kuwa washindi, lkn kwa usimamizi wa wananchi waliobaki vituoni ushindi ulilindwa. Kwa mfano Arumeru thermosi zilikuwa zinaingizwa na kura lkn wananchi walizuia.
Isitoshe CCM ni chama bilionea uwezekano wa kuwahonga wasimamizi ni mkubwa sana. Kwa hiyo NEC inapotoa matamko yake ijue inafanya kazi ktk jamii ambayo kutendeana haki bado kuko katika kiwango cha chini, kwa hiyo watwambie ni kwa namna gani tunaweza kuzuia hilo.
Nawakilisha wanajamii
Katika jamii ya watu wastaarabu na wanaotendeana haki hivyo ndo inavyotakiwa kuwa. Katika makala yake Generali Ulimwengu kama wiki mbili zimepita alisema katika chaguzi za nchi za Afrika hatujafikia kiwango cha ustaarabu cha kutendeana haki.
Katika kudhihirisha hilo katika uchaguzi uliopita kama watu wangepiga kura wakarudi nyumbani leo hii mbunge wa Arusha mjini Lema asingekuwa mbunge. Wenje Nyamagana asingekuwa mbunge, Nasari asingekuwa mbunge. Wasimamizi walikuwa wakipewa presha watangaze watu walioshindwa kuwa washindi, lkn kwa usimamizi wa wananchi waliobaki vituoni ushindi ulilindwa. Kwa mfano Arumeru thermosi zilikuwa zinaingizwa na kura lkn wananchi walizuia.
Isitoshe CCM ni chama bilionea uwezekano wa kuwahonga wasimamizi ni mkubwa sana. Kwa hiyo NEC inapotoa matamko yake ijue inafanya kazi ktk jamii ambayo kutendeana haki bado kuko katika kiwango cha chini, kwa hiyo watwambie ni kwa namna gani tunaweza kuzuia hilo.
Nawakilisha wanajamii