Sele Mkonje
JF-Expert Member
- Oct 2, 2011
- 643
- 844
Habari zenu Brothers and sisters in Humanity.
Hakuna asiefahamu tukio lililotekea hivi majuzi huko Bukoba,watu mbali mbali wamejitokeza kutoa michango yao kuwasaidia wahanga wa Tetemeko.
Cha ajabu ni kwamba mpaka sasa hakuna msanii wala wasanii waliojitokeza kutoa mchango wa hali na mali kwa wahanga.
Ndugu zangu,hali ni mbaya sana huko Bukoba,watu wanalala nje kutokana na nyumba zao kubomoka. Inasikitisha sana kwa hawa tunaowaita kioo cha jamii kujiweka mbali na mambo muhimu ya kijamii kama haya.
Pia nimeshangaa sana Kuona kuna baadhi ya wasanii wamediriki hata kuachia nyimbo mpya wakati huu watu wanatafakari ni jinsi gani wawasaidie wanaBukoba.
Lakini sio wasanii tu wanaotakiwa wajitokeze,hata sisi raia wa kawaida ni wajibu wetu kuwasaidia wenzetu kwa chochote tulicho nacho na kama huna kama mimi basi tuwaombee dua njema wahanga na waliopoteza maisha walazwe mahali wanapostahili. Amina
Natumaini Ujumbe huu wataupata na kujitokeza kuwachangia wahanga wa tetemeko..
[HASHTAG]#mckonjetv[/HASHTAG]
Hakuna asiefahamu tukio lililotekea hivi majuzi huko Bukoba,watu mbali mbali wamejitokeza kutoa michango yao kuwasaidia wahanga wa Tetemeko.
Cha ajabu ni kwamba mpaka sasa hakuna msanii wala wasanii waliojitokeza kutoa mchango wa hali na mali kwa wahanga.
Ndugu zangu,hali ni mbaya sana huko Bukoba,watu wanalala nje kutokana na nyumba zao kubomoka. Inasikitisha sana kwa hawa tunaowaita kioo cha jamii kujiweka mbali na mambo muhimu ya kijamii kama haya.
Pia nimeshangaa sana Kuona kuna baadhi ya wasanii wamediriki hata kuachia nyimbo mpya wakati huu watu wanatafakari ni jinsi gani wawasaidie wanaBukoba.
Lakini sio wasanii tu wanaotakiwa wajitokeze,hata sisi raia wa kawaida ni wajibu wetu kuwasaidia wenzetu kwa chochote tulicho nacho na kama huna kama mimi basi tuwaombee dua njema wahanga na waliopoteza maisha walazwe mahali wanapostahili. Amina
Natumaini Ujumbe huu wataupata na kujitokeza kuwachangia wahanga wa tetemeko..
[HASHTAG]#mckonjetv[/HASHTAG]