Wasanii kuweni wazalendo

Wasanii kuweni wazalendo

kibavu

Senior Member
Joined
Oct 15, 2008
Posts
136
Reaction score
82
Wasanii wa mnapoalikwa kwenye shughuli za kisiasa, linapokuja suala la wimbo wa taifa na alama za kitaifa suala la siasa na usanii uwekwe pembeni. Kwa mfano jana msanii Single Mtambalike amechemka sana wakati wa zoezi la kufungua kampeni za CCM, kwani wakati watu wakiwa wametulia na kuimba wimbo wa Taifa yeye alikuwa akipepea bendera kitu ambacho ni kinyume na taratibu za uimbaji wa wimbo wa taifa. Pia kulikuwa na wasanii walioonekana wakifanya ‘movement’ mbalimbali wakati zoezi hilo likiendelea!

Kama hiyo haitoshi hata yule msanii aliyepewa kazi ya kuimbisha wimbo wa taifa naye pia alichemka kwa kuimba wimbo wa taifa kama vile anapiga ‘remix’ ya wimbo huo. HII SI SAWA NA HAIKUBALIKI.... ALAMA ZA TAIFA LAZIMA ZIHESHIMIWE MAHALI POPOTE, WAKATI WOWOTE NA WATU WOTE!

USHAURI: Inapotokea WASANII mmealikwa kwenye shughuli ya kisiasa kama hiyo ambayo ina mtazamo wa kitaifa basi fanyeni mazoezi ya pamoja ‘rehearsal’ ili kuondoa hali ya sintofahamu na kujishushia hadhi yenu na hadhi ya wale walio waalikeni.
 
ushauri mzuri sana, uzalendo wa nchi yako unaanzai na kuheshimiu nembo zake kama wimbo wa taifa
 
Wasanii wetu njaa Kali, hivyo wanaona ni bora waongeze mbwembwe ili waonekane wamejituma walipwe poa
 
Kama ningekuwa msanii nisingejihusisha na mambo ya ushabiki wa vyama manake mwisho wa siku nitajiongezea maadui. lakini ikitokea ninayemsapoti akashindwa, nitaanzaanzaje kujikomba kwa niliyekuwa namponda! Nawashauri wasanii punguzeni njaa, nyie hamna tofauti na wanahabari na wahubiri au mashehe. hata kama unakipenda chama fulani jichanganye kama raia wengine, kama umelipwa kwa shoo fanya kazi yako ya shoo then take care.
 
jana ilikuwa fiesta haukuwa uzinduzi wa kampeni
 
ruby(kama nimepatia) aliimba kama siku Jamie Foxx alipoimba wimbo wa taifa la Marekani kwenye pambano la Mayweather na Manny Pac
 
Wasanii waliokuwepo Jangwani jana wote ni wale vimeo. Wasanii wanaojitambua nadhani hukuwaona jana.
Subiri UKAWA waanze kampeni ndo utajua vizuri aina za wasanii waliopo Bongo.
 
Back
Top Bottom