Wapinzani wanadi sera ipi uchaguzi mdogo?

Wapinzani wanadi sera ipi uchaguzi mdogo?

desertfox

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2014
Posts
347
Reaction score
244
Habari wanajamvi.

Nini maoni yako kuhusu uchaguzi mdogo wa wabunge majimbo ya Kinondoni na Siha? Je wapinzani wanadi sera ipi ili kupigiwa kura na wapigakura?

Binafsi yangu naona baadh ya sera au hoja zitawavuta wananchi:-

> Hali ya uchumi wa wananchi hapa watumie nukuu ya Mwl "Uchumi wa kweli ni uchumi wa watu sio uchumi wa vitu"

> Uhuru wa jamii husika ikiwemo kutoa maoni kukosoa muenendo wa viongoz n.k.

> Upatikanaji wa huduma za kijamii hasa afya

> Uimarishwaji wa uchumi hasa mzunguko wa pesa

> Upatikanaji wa ajira hasa kwa watoto maskini

NB: Watumie ahadi za Mkulu alizozitoa kwenye kampeni na hali ilivo sasa.

Karibuni
 
Wanadai Lissu, Roma, Ben Saanane na UKUTA tu mkuu. Na nimesahau pia wanadai Bashite afukuzwe na pia Nape arudishiwe uwaziri.
 
Mkulu amejitahidi kukusanya kodi ili kuinua uchumi na kafanikiwa, lakini kabaka Sera ya elimu bure ambapo pato hutoka point A kwenda point B. Kifupi ni sawa na kuchimba shimo na kulifukia bila kujua kama unapoteza nguvu.
 
Uasaliti, ysaliti. Usalititusimchague huyu kwa kuwa aliwasaliti nyinyi na kuhamia kwa wale sio mkeli wala hafai.
 
Kwa hali ilivyo, hata wakienda wakapanda jukwaani kusalimia na kushuka watapigiwa kura na watashinda, hakuna anaeitaka ccm, wanashindaga kwa wizi, maana ni wezi wazoefu. Wizi ndio sifa kuu ya hiki chama, ikifuatiwa na unafiki.
 
Kwa hali ilivyo, hata wakienda wakapanda jukwaani kusalimia na kushuka watapigiwa kura na watashinda, hakuna anaeitaka ccm, wanashindaga kwa wizi, maana ni wezi wazoefu. Wizi ndio sifa kuu ya hiki chama, ikifuatiwa na unafiki.
Umeanza vizuri umemalizia kwa kuandika mashudu.
 
Dah yani wapinzani leo wanafanya kuwaomba wananchi Sera?
 
Back
Top Bottom