Wapi naweza kupata vifaa vya saluni ya kike

Wapi naweza kupata vifaa vya saluni ya kike

laii

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2016
Posts
853
Reaction score
1,126
Kuna Dada anaishi Dar Es Salam-kinondoni,kaniomba nimuulizie hii kitu, yeye hana smart phone ila nilipomwelezea faida nazopata kupitia Jf akatokea kuvutiwa nayo na kunituma huu ujumbe. Location anayotegemea kufungua ni mkwajuni. Ntakua naleta mrejesho wa kila hatua kama akiridhia wakuu.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza naomba mnipe chimbo nitakalopata viafaa vya saluni ya kike vyenye ubora MA bei ya kawaida. Naamini huku kuna wabobezi, nikipata mtu akanipa na tips za usimamiaji nitafurahi sana sana. Mimi sijawahi fanya biashara ya saluni. Na muda mwingi nakua kazini, kazi yangu ni mtu Wa masijala somewhere, sasa natafuta kitu cha kuongeza Kipato.jinsia Ke.
 
Kama ukiwa unatoka Kinondoni ukishavuka Jangwani utakutana na makutano ya Morogoro Rd na UN Rd/Swahili Rd.

Ukifika kwenye hayo makutano utapinda kulia kuelekea Kariakoo, upande wa kushoto kuna petrol station na kulia kwako kuna yard vuka hiyo yard, vuka barabara ya vumbi iliyopo kulia kwako then kuna duka moja kubwa sana hapo linauza vifaa mbalimbali vya salon za kike na kiume.

Ulishindwa hapo nenda Kariakoo upande wa maduka ya vipodozi mtaa wa Jangwani kama skosei karibu na mabasi yanayoenda Mbezi nilishakuta vitu vya salon pia.

Ukitaka nikupeleke karibu PM.

KLH.
 
Kama ukiwa unatoka Kinondoni ukishavuka Jangwani utakutana na makutano ya Morogoro Rd na UN Rd/Swahili Rd.

Ukifika kwenye hayo makutano utapinda kulia kuelekea Kariakoo, upande wa kushoto kuna petrol station na kulia kwako kuna yard vuka hiyo yard, vuka barabara ya vumbi iliyopo kulia kwako then kuna duka moja kubwa sana hapo linauza vifaa mbalimbali vya salon za kike na kiume.

Ulishindwa hapo nenda Kariakoo upande wa maduka ya vipodozi mtaa wa Jangwani kama skosei karibu na mabasi yanayoenda Mbezi nilishakuta vitu vya salon pia.

Ukitaka nikupeleke karibu PM.

KLH.
Asante sana kwa maelekezo, nitamwelekeza huyu dada, pia ningepata mchangiaji anaye jua kuhusu usimamizi wa salun, vifaa na dawa za nywele
 
Back
Top Bottom