Birds in bush
Member
- Sep 15, 2013
- 42
- 23
Naanzisha hii thread ili tupate maoni kati ya wanawake ambao wanaweza kuwa viongozi wa nchi kati ya Rose Migiro, Anna Makinda na Prof Tibaijuka. Je Rose Migiro anaweza kuwa Rais wa Tanzania hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa naibu katibu mkuu wa UN pamoja na kwamba hakupewa nafasi ya kumaliza ngwe yake ya pili kwa sababu ambazo hazijulikani!!!! Pili Anna Makinda ambaye ameliongoza bunge la JMT kwa kipindi cha takribani miaka minne sasa huku kukiwa na kelele nchi nzima namna anavyoongoza bunge hilo na Prof Tibaijuka, mama wa shoka ambaye alikuwa UN habitat ambapo baadaye amekuwa Waziri wa ardhi licha ya kuendelea na kuwa na miji isiyopangika katika nchi yetu, ujenzi holela kila sehemu kana kwamba hakuwa hata mtu wa kusema sasa imetosha miji yetu kujengwa hovyo hovyo utadhani uko nchi ambayo wananchi hawajui hata umuhimu wa kujipanga vizuri ili iwe rahisi hata kupata huduma za kujamii.
Leteni mawazo
Leteni mawazo