Wanawake: Kuna watu mnawachagua wa kula nao raha wengine kuwachuna

apologize

JF-Expert Member
Jul 22, 2015
709
568
Habari wakuu,

Hii kitu imenitokea kwangu na ninahisi mwanaume mwezangu simtendei haki, kuna binti mmoja nilikuwa naye kwenye mahusiano kipindi cha nyuma, tukapotezana takribani miaka miwili, kutoka na shughuli za kimasomo na wakawa wamehama mkoa moja kwa moja.

Mimi na yeye tukakubaliana tuvunje mahusiano yetu na tukayavunja kwa amani,miezi kadhaa iliyopita nikapokea sms akinilaumu kwa kukaa kimya sana mimi nikamjibu, simu nilibadilisha hivyo namba nyingi nilikuwa nimezipoteza na hiyo namba aliyonitext ilikuwa ni ya airtel,kwa kuwa mimi sina laini ya airtel nikashindwa kumwangalia kwenye airtel money nijue ni nani? Zaidi ya kumwambia nimepoteza namba nyingi naomba ujitambulishe akasema OK, lakini akagoma kusema yeye ni nani, na mimi nikaamua kupotezea siku hiyo kutokana na majukumu kunibana.

Sasa kuna siku rafiki yake akanipigia simu akaniambia fulani nimekutana nae Dodoma na sasa hivi yupo huko Dar, nikasema naomba namba yake akanitumia sasa kuisave na kumtumia text ya salamu nikaikumbuka hii namba baada ya simu kuonesha text za nyuma naamini hapo mmenielewa smartphone zinavyoonesha chat history.

Baada ya hapo tuliwasiliana na kupanga kuonana, akanielekeza nikamfata mpaka alipo kuwa kwenye duka la nguo la mama ake tukapiga story sana na cha ajabu mapenzi yakaanza upya tena kwa kasi ya ajabu.

Sasa Jana akaniambia niende kwao mambo sikukuuu nikamtembelee nikatimiza wajibu wangu nikafika kutii mwaliko, sasa kuna namba nilikuwa nashida nayo ambayo yeye alikuwa nayo, akaniambia chukua kwenye simu akaniachia simu yake, huwa sina tabia ya kukagua simu ya mtu, Jana uvumilivu ukanishinda nikasema leo ngoja nizame kwenye sms zake.

Nilichokikuta huko ni binti kulalamika jamaa wake kuwa mbona umechelewa kunitumia pesa na jamaa kugomba pesa zote umepeleka wapi nilizokupatia mwisho jamaa akamwambia subiri mshahara wa Mwezi huu ukitoka.

Hili swala nimelileta kwenu mnisaidie kimawazo, maana naamini mawazo ya wengi yananguvu nifanye nini juu ya binti huyu? Kuniomba hela huwa hataki, mimi nikimpa ni kwakulazimisha sana, kitu kingine nilimuuliza kama hatarudi Dodoma akasema harudi kuja huku ndo moja kwa moja,hii inamaanisha ni vigumu kuonana na huyo mpenzi wake aliyepo huko Dodoma.

Hofu yangu sijui mimi wana malengo gani na huyo jamaa wake maana kwenye sms zake nimekutana na mambo mengi waliyopanga na huyo jamaa wake pili kwangu ndo kaniganda balaa hadi aninitambulisha kwa ndugu zake na kuning'ang'ania niende kwao mara kwa mara.

Naombeni ushauri kwa hili na sipendi ajue kama nimekagua simu yake na kukutana na mambo mengine huko.

Nawasilisha
 
Naomba unisaidie ushauri wako ktk hili, nichukue maamuzi yapi?
leave her alone...Sio kila binadamu ana roho ya upole.Wengine ni katili,imagine huyo jamaa akija kugundua baadae kwamba anachezewa pesa zake si atawafanyia kitu kibaya? wengine wanaweza kukuroga uwe tahira na kumbe kosa sio lako! mwakbie tu ukweli huyo dada hauko tayari kushea,kama anakuhitaji wewe aachane na huyo jamaa!
 
hiyo ni kawaida xna kwa mabint, ila na sisi wanaume huwa ni sbb kwa maana unamtokea bint anakuweka waz kuwa anaye ampendaye unamshawishi na viela vyako inabid uchunwe tu hamna namna.

Alaf mbaya zaid jinsi unavyoombwa hela ndivyo unavyozid kupenda, Kumbe anayekuomba hela anakuona boya maumiv utayajua badaye.
 
Okay tatizo ni kumchuna mwenzio we huchunwi au tatizo ni nini?
Hapa nilipo nabaki njia mbaya, anachonesha ni kunihitaji mm kwa sana, lakin hapo hapo naona Kama anamuomba pesa Huyu mwanaume mwengine zangu hataki, ndo nachohofia kuna kitu gani kwa nyuma?
 
leave her alone...Sio kila binadamu ana roho ya upole.Wengine ni katili,imagine huyo jamaa akija kugundua baadae kwamba anachezewa pesa zake si atawafanyia kitu kibaya? wengine wanaweza kukuroga uwe tahira na kumbe kosa sio lako! mwakbie tu ukweli huyo dada hauko tayari kushea,kama anakuhitaji wewe aachane na huyo jamaa!
Ntamuachaje sasa na atanielewa vipi, maana mm ndo ntakuwa chanzo tena, mwanzo mimi ndo nilimwambia tuachane akakubali lakin kwa kulazimisha, sasa hiv alivyo ning'ang'ania had kunilazmsha kwenda kwao na kunitambulisha kwa ndugu zake.... Hapo unachomokaje si nitaonekana muhuni
 
Si mlishavunja mahusiano, unamendea nini tena mkuu au tindikali ili akili ikukae sawa??
 
Moyo wako unasemaje mwenzio ana chunwa pesa na wewe ana kuchuna ROHO? kama umekubali na unataka kua nae
kaanae chini mweleze muelekeo wako na nini unataka kufanya nae kwenye maisha,la umeamua kula na kukimbia
basi tulia kama una nyolewa ..........
 
Ntamuachaje sasa na atanielewa vipi, maana mm ndo ntakuwa chanzo tena, mwanzo mimi ndo nilimwambia tuachane akakubali lakin kwa kulazimisha, sasa hiv alivyo ning'ang'ania had kunilazmsha kwenda kwao na kunitambulisha kwa ndugu zake.... Hapo unachomokaje si nitaonekana muhuni
Wewe,hauhitaji ushauri
 
Moyo wako unasemaje mwenzio ana chunwa pesa na wewe ana kuchuna ROHO? kama umekubali na unataka kua nae
kaanae chini mweleze muelekeo wako na nini unataka kufanya nae kwenye maisha,la umeamua kula na kukimbia
basi tulia kama una nyolewa ..........
Asant kwa ushauri wako ntaufanyia kazi, unanishaur vipi kwa hapa niendelee kuchunguza simu yake nijue hitimisho yake na huyo jamaa maana yeye anadai npo peke yangu na aliyekuwa naye wameachana
 
Asant kwa ushauri wako ntaufanyia kazi, unanishaur vipi kwa hapa niendelee kuchunguza simu yake nijue hitimisho yake na huyo jamaa maana yeye anadai npo peke yangu na aliyekuwa naye wameachana
Kwanini uji stress? una kua busy na kutafuta pesa na maisha mazuri bado unajitia stress zisizokua za lazima
zungumza nae na let her know kua unajua yuko na mtu na kama wanataka kurudiana akwambie so that you can move on else kuanzia sasa kusiwe na siri,na wewe pia kama ulivyo ichukua cm ya mwenzio ukaona vimeo vyake,na wewe pia usije kua una vimeo vyako kushinda yeye.....
 
Back
Top Bottom