Wanajf leo nimeshuhudia kisa ambacho kimenifurahisha sana,tulikuwa kwenye semina flani na haikuwepo dalili ya kuisha mapema semina hy ingawa muda wa jioni ulikuwa umekaribia ambapo kinamama wengi walianza kutoka na kuchukua posho zao kwa gea kuwa wananyonyesha,basi akainuka mbaba mmoja nae kasema ananyonyeshaga hivyo nae apewe kipaumbele atoke mapema,basi kuona hivyo mwezeshaji akatoa ruhsa kwa wababa wote wanaonyonyesha mabebi zao waende kuchukua posho waende wakanyonyeshe watoto wao,na ndio ikawa mwsh wa semina,wote tukatoka,uzuri tulikuwepo watu wazima tupu,vp wakuu na nyie mnanyonyesha mabebi zenu?