Wanaokatisha ticket ndani ya train hawafaiiiii!!!!!!

Wanaokatisha ticket ndani ya train hawafaiiiii!!!!!!

Mchokozi

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2012
Posts
215
Reaction score
29
Leo nimepanda train kutokea Mabizo mwananchi kuelekea mjini stesheni na kujifunza yafuatayo:

1. Wale wa dada wanaokatisha ticketi ndani ya train hawana uzoefu na ni waoga, kwani walikuwa wanadai abiria huku wakiwa wananyuso za uoga.

2. Hawakuwa na ticketi za kutosha kwa abiria tuliopandia njiani ambako hawajaweka vituo vya kukatia ticketi matokeo yake zilimwishia na mimi kushindwa kumpa pesa bila ticketi............inaniuma sana kwani nilipanda buree bila kulipa.

3. Inasemekana wanaokatisha ticketi ni kampuni binafsi na si wafanyakazi wa TRL, kwa nini imepewa Kampuni binafsi???......source...mfanyakazi wa TRL tuliyekuwa naye ndani ya behewa.

Ili waweze kufanikiwa kukusanya mapato naomba hawa wadada waliowekwa waondolewa na kupewa kazi hiyo wafanyakazi wa TRL wenyewe kwani tunahitaji usafiri huu uendelee kuwepo kwa manufaa ya wa Tz.

Nawasilisha wana JF !!!!!
 
mwanzo mgumu nadhani watarekebisha Wawatrain vijana wa kiume waliomaliza Secondary na vyuo wanaoshinda vijiweni Jobless.
 
duuuuu bongo bwana unaweza kuta kuna mtu ameshakula tenda hapo ya kukatisha tiketi wakati kunawafanya kazi wa TRL wanacheza karata ofisini
 
unaweza ukute hiyo kampuni ya kukata ticket inamilikiwa na mke wa mkurugenzi wa TRL...usifanye mchezo na wabongo...
 
duuuuu bongo bwana unaweza kuta kuna mtu ameshakula tenda hapo ya kukatisha tiketi wakati kunawafanya kazi wa TRL wanacheza karata ofisini

Ni kweli mkuu, yaani hii nchi ni ufisad tu kila mahali. Wanaongeza gharama za uendeshaj bila sababu. Watajikuta hii project inashindwa kuwa sustainable na kisha ku-collapse. Waanaacha kuwatumia wafanyakazi wao wasio na kazi maofisini mwao na kukodi kampuni nyingine bila ulazima wowote.
 
Ati nini? unamaanisha shirika lina upungufu wa wafanyakazi? na hao walioajiriwa ni kwa utratibu na vigezo vipi? na kwa nini ni wanawake tu? kama ticket zinakwisha na watu wansafiri bure inamaana hata control ya revenue pia ni ya mashaka!
 
Inawezekana imepewa kampuni binafsi kama tenda! Ni kawaida ya serikali nyingi ulimwenguni kutumia mfumo wa tenda. So usione ajabu kijana
 
Hao TRL ni kitu gani wamekifanya kwa ufanisi ? Usafiri wa reli TZ umekufa sababu ya uzembe wao , wengi wao walaji na wavivu. Wapeni makampuni na myape malengo thabiti ya ufanisi na kamishen kufuatana na ubora wa kazi yao muone kama hawawezi kufanya kazi nzuri. Tatizo la vyombo vya umma ni kuwa wafanyakazi wake wao ndio kwanza na wateja wa huduma ni wa mwisho na wanaona kama wanawafadhili wateja na si kama wanastahili kupata huduma sababu wanalipa.
 
Ku out source ni Vizuri sana, Ila Changamoto ni Nyingi!! Mimi ningependelea Kwenye Vituo vyote vilivyoteuliwa Viwekewe Fence na Mkatisha ticket awepo Kwenye defined office na electronic Ticketing Machine!! Na pia kuwepo na option ya kukata hata tikect za msimu au za muda mrefu kidogo say kwenda na kurudi ili kuondoa usumbufu wa Change!!
 
mwanzo mgumu nadhani watarekebisha Wawatrain vijana wa kiume waliomaliza Secondary na vyuo wanaoshinda vijiweni Jobless.

usinikumbushe ya Ezekiel Kimwaga na kuanzishwa kwa simba tv
 
Wapeni muda kidogo wajameni, too early to judge!
 
unaweza ukute hiyo kampuni ya kukata ticket inamilikiwa na mke wa mkurugenzi wa TRL...usifanye mchezo na wabongo...

inawezekana kabisa maana hata juzi kule bungeni Dk. Mwakyembe aligusia kuwa tayari kuna wajanja wachache wameshaanza ufirauni wao...
 
Hii nchi imejaa virus..inatakiwa tuiformat kwanza..yaani kila sehemu watu wanapiga deal zao tu..bado Ikulu sasa utaskia kuna mtu amechukua tenda ya kufua ngua za Mh.
 
duuuuu bongo bwana unaweza kuta kuna mtu ameshakula tenda hapo ya kukatisha tiketi wakati kunawafanya kazi wa TRL wanacheza karata ofisini
.....unanikumbusha kichefuchefu kingine ubungo bus terminal nasiki mzee kingunge & co naye amekula shavu!
 
Ku out source ni Vizuri sana, Ila Changamoto ni Nyingi!! Mimi ningependelea Kwenye Vituo vyote vilivyoteuliwa Viwekewe Fence na Mkatisha ticket awepo Kwenye defined office na electronic Ticketing Machine!! Na pia kuwepo na option ya kukata hata tikect za msimu au za muda mrefu kidogo say kwenda na kurudi ili kuondoa usumbufu wa Change!!

Big point.... Yani iwe kama pale kwenye pantoni
 
Back
Top Bottom