Wanajeshi Zimbabwe wapinga kurefusha muhula wa urais

Wanajeshi Zimbabwe wapinga kurefusha muhula wa urais

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
812
Reaction score
1,870
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa, anakabiliwa na pingamizi la kisheria kutokana na azma yake ya kuongeza muda wake madarakani.

Kundi la wanajeshi wa vita vya ukombozi wa nchi hiyo wamefungua shauri mahakamani kuzuia serikali kufanya marekebisho ya katiba ili kuongeza ukomo wa mihula ya urais na bunge kutoka miaka mitano hadi saba.

Haya ni baada ya serikali ya Zimbabwe kutoa taarifa rasmi kuthibitisha mpango wake wa kubadili katiba ya nchi ili kuongeza muda wa uongozi wa Rais wa sasa Mnangagwa, jambo linalochukuliwa kama lenye nia ya kusambaratisha uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka wa mwaka 2028.

Mapendezo hayo ambayo yaliwasilishwa na kuidhinishwa na bunge wiki iliyopita yananuia kuongeza muda wa urais na ubunge hadi mwaka wa 2030.
 
The former South African president the late Pieter Willem Botha once said, "the gravest mistake that will never be pardoned is to allow the black man to rule." Today the evidence is there for all to see. Independent African countries are the laughing stock of the world 🌎🌍
 
Most likely huyo rais mwizi ataongezewa miaka 2 zaidi.

Ipo hivi,

1. Serikali ina control taarifa zote zinazohusu mabadiliko ya katiba na kama hapa Tz watatumia machawa kulaghai wananchi hohehahe.

2. Vitisho kwa yoyote yule atakayepinga.
- hapa kama ni businessman/woman utarudishwa zero.
- police brutality
- serikali wakishirikiana na machawa watawalebel wanaopinga anti-state au foreign influenced kama unavyoona hapa bongo.

3. Wananchi wengi wa Zimbabwe ni masikini sana focus yao kubwa ni kuamka asubuhi wakatafute pesa ya kula sasa kufuatilia kwa undani na kuhakikisha katiba inalindwa ni jambo gumu.

4. Mahakama za Zimbabwe kama hapa Tz ni uharo mtupu. Well, kwenye kesi za kawaida pengine unaweza kupata fair judgement lakini inapohusu majambazi wnaojiita serikali sahau hilo jambo.
 
Juzi si walikuwa makao yao makuu!? mbona hawakumkanya mwenzao? watu wakifa kwenye machafuko watapiga kelele kulaani. sijui nani katuloga.
 
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa, anakabiliwa na pingamizi la kisheria kutokana na azma yake ya kuongeza muda wake madarakani.

Kundi la wanajeshi wa vita vya ukombozi wa nchi hiyo wamefungua shauri mahakamani kuzuia serikali kufanya marekebisho ya katiba ili kuongeza ukomo wa mihula ya urais na bunge kutoka miaka mitano hadi saba.

Haya ni baada ya serikali ya Zimbabwe kutoa taarifa rasmi kuthibitisha mpango wake wa kubadili katiba ya nchi ili kuongeza muda wa uongozi wa Rais wa sasa Mnangagwa, jambo linalochukuliwa kama lenye nia ya kusambaratisha uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka wa mwaka 2028.

Mapendezo hayo ambayo yaliwasilishwa na kuidhinishwa na bunge wiki iliyopita yananuia kuongeza muda wa urais na ubunge hadi mwaka wa 2030.
Huyu Emmerson amegeuka Mugabe mwingine.
 
The former South African president the late Pieter Willem Botha once said, "the gravest mistake that will never be pardoned is to allow the black man to rule." Today the evidence is there for all to see. Independent African countries are the laughing stock of the world 🌎🌍
Huyu Mzee alitoa speech Moja heavy sana 😄😄

Imejaa kejeli zenye uhalisia mtupu
 
Back
Top Bottom