Wanafunzi watazamwe kuhusu kadhia ya usafiri

Wanafunzi watazamwe kuhusu kadhia ya usafiri

TheForgotten Genious

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
2,436
Reaction score
3,557
Wanafunzi wa Dar es salaam wananyanyaswa sana na makondakta wa daladala,watoto wanawahi mapema stand lakini hawawabebi na mara nyingine wanawatusi kabisa.

Wanaweza kukaa stand takribani masaa 4 wakisubiri usafiri lakini kila gari linalokuja wana wazuia.

Kuna watoto wa darasa la 1-7 mara kasha’s nimeshuhudia wakisukumwa na kondakta wasipande gari ,mara nyingine nimekua nikilazimika kuwalipia nauli ya mtu mzima ilikuwafariji.

Mtoto Anatolia nyumbani saa kumi alfajiri anaenda stand lakini anafika shule saa tatu ama 4;akitoka anafika saa 21 mpaka 23,

Wazazi kwanini msiwape nauli za watu wazima .

Hawa watoto hasa wakike wanaingia kwenye vishawishi kwa sababu kama hizi.
 
Wanafunzi wa Dar es salaam wananyanyaswa sana na makondakta wa daladala,watoto wanawahi mapema stand lakini hawawabebi na mara nyingine wanawatusi kabisa.

Wanaweza kukaa stand takribani masaa 4 wakisubiri usafiri lakini kila gari linalokuja wana wazuia.

Kuna watoto wa darasa la 1-7 mara kasha’s nimeshuhudia wakisukumwa na kondakta wasipande gari ,mara nyingine nimekua nikilazimika kuwalipia nauli ya mtu mzima ilikuwafariji.

Mtoto Anatolia nyumbani saa kumi alfajiri anaenda stand lakini anafika shule saa tatu ama 4;akitoka anafika saa 21 mpaka 23,

Wazazi kwanini msiwape nauli za watu wazima .

Hawa watoto hasa wakike wanaingia kwenye vishawishi kwa sababu kama hizi.
Ni kweli mkuu, wanafunzi wanateseka mno jamani, hii sio sawa kabisa.

Usafiri kwa Dar es salaam ni changamoto kubwa kwa abiria wote ila wanafunzi ndio wahanga wakubwa.
 
Wazazi/walezi wanapaswa kuhamishia watoto wao kwenye shule zilizopo karibu na makazi yao.

Utakuta mwanafunzi anatoka Majohe kwa Ngozoma anaenda kusoma Tegeta kana kwamba huko hakuna shule au maeneo jirani hayana shule.

Usipomhurumia kwanza mwanao, ni ngumu serikali/walimwengu kumhurumia mtoto wako.
 
Wanafunzi wanateseka ila bado kuna wanaopenda kujichelewesha na wengine ni wababe wa kijinga hali inayosababisha kupata ugumu kwenye vyombo vya usafiri, kuna watoto ni wadogo ila wana lugha chafu sana.
 
Wazazi/walezi wanapaswa kuhamishia watoto wao kwenye shule zilizopo karibu na makazi yao.

Utakuta mwanafunzi anatoka Majohe kwa Ngozoma anaenda kusoma Tegeta kana kwamba huko hakuna shule au maeneo jirani hayana shule.

Usipomhurumia kwanza mwanao, ni ngumu serikali/walimwengu kumhurumia mtoto wako.
Well said
 
Wanafunzi wanateseka ila bado kuna wanaopenda kujichelewesha na wengine ni wababe wa kijinga hali inayosababisha kupata ugumu kwenye vyombo vya usafiri, kuna watoto ni wadogo ila wana lugha chafu sana.
Wameathiriwa na mazingira ,makondakta wanawapelekesha imefika sehemu wanajihami
 
Ukitaka asisumbuke mpe nauli kamili
Vinginevyo mnatafuta lawama kwenye biashara za watu
 
halafu anakuja mzalendo mmoja na kundi lake kuponda wanaosomesha shule za mabasi ya njano.
 
Back
Top Bottom