Waliopata divisheni 0 hawapo kwenu tu hata kwetu wapo

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,870
34,352
profjoycendalichako.jpg

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako.

MATOKEO ya Kidato cha Nne yametangazwa, shule zilizoaibika kwa matokeo mabaya ni za serikali zinazosomesha watoto wa maskini.

Tukioanisha mantiki, ufaulu wa wanafunzi miaka ya hivi karibuni ni sawa na vita ya matajiri na maskini; mwaka huu tena walalahoi wamevuna aibu ya ufukara wao. NANI MWENYE KUJALI KATIKA HILI?

Wakati mwingine fikra ni kitu cha ajabu, ndiyo maana katika muktadha huu wa matokeo mabaya ya shule nyingi za wasio nacho ni wachache waliotafakari taifa letu linaelekea wapi?

Ni wazi kabisa, taifa lipo kwenye mtikisiko mkubwa wa ki-hali! Maisha na mafanikio bora yanachukuliwa mikononi mwa maskini walio wengi na kurasimishwa kwa matajiri wachache.

Fedha hivi sasa inaongea! Ukitaka elimu bora, tiba nzuri, huduma za kijamii za kisasa usitumie kinywa chako; mfuko uteme noti; kila kitu ni murua! Hata nafasi za kisiasa bila fedha hupati.

Nawasihi Watanzania wenzangu, tusikubali kurudi enzi za ukoloni wa Wazungu waliopora utashi wetu kwa kutumia utajiri na maarifa yao kwa kuwapa nafasi matajiri weusi kuwa watawala wetu wapya kwa mfano wa Wazungu tuliowatimua wakati tukidai uhuru.

Kama ilivyokuwa enzi za ukoloni, Rais wa Kwanza wa Tanzania, Julius Nyerere, aliwaongoza wananchi wanyonge walio wengi kupigania usawa wa huduma na haki kwa wote na kufanikisha vita ya kujikomboa iliyotufikisha hapa.

Shime wanyonge wote wa leo! Tuungane na Rais wa Awamu ya Tano, John Magufuli aliyeonesha nia ya kuwatetea wanyonge kuutokomeza mfumo wa ‘fedha inaongea’.

Ni wazi kuwa nchi hii si ya matajiri, bado ni ya wakulima na wafanyakazi maskini, hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa huduma bora haziendi kwa matajiri wachache bali kwa Watanzania wote.

Ni muda wa kila mwananchi kutafakari kwa nini shule za matajiri zinaongoza ufaulu kitaifa? Tujiulize ziko wapi shule za umma za watoto wenye vipaji, mfano Tabora Boys, Mazengo, Ifunda, Ilboru, Msalato na nyingine nyingi?

Shule hizi si tu zilikuwa mkombozi wa watoto wa maskini kupata elimu bora lakini ndizo zilizozalisha wataalamu na viongozi wengi ambao taifa linajivunia hivi sasa.

Watanzania wenzangu; wanafunzi waliopata divisheni 0 hawapo huko kwenu tu, hata kwetu wapo! Ni kilio cha taifa zima; vipi hisia zetu zisiumizwe na hili na kuona ipo haja ya kuunganisha nguvu zetu kuisaidia serikali kupambana ili kurejesha nchi mikononi mwa wanyonge!

Tukiacha shule za ada za milioni 3 kwa mwaka ambazo wananchi wengi hawawezi kupeleka watoto wao huko ziwe ndiyo njia ya kupata elimu bora, maana yake tunakubali watoto wa maskini wawe watawaliwa na wachunga ng’ombe maisha yao yote.

Nahamasisha; ukombozi wa elimu bora kwa wote unaanzia katika jamii zetu, tujitoe kadiri tuwezavyo kuchangia ubora wa elimu kwa watoto wetu.

Tuwahamasishe watoto wapende shule, tukatae utoro na tuwape msaada uwafaao katika maisha yao ya shule kamwe tusikwepe majukumu yetu kwa kisingizio cha serikali kuwahudumia.

Tukumbuke serikali ni watu, tukifanyacho sisi imefanya serikali. Si vibaya tukijenga nyumba bora za walimu na madarasa kwa kujitolea halafu serikali kuu ikachangia tulipokomea lengo ni ushiriki wa wananchi wote katika vita hii. Tumuunge mkono rais Magufuli kwa uwezo wetu wote.

Natoa wito kwa watendaji na viongozi wote wa mitaa na vijiji kuhakikisha kuwa shule zilizopo maeneo yenu zinafanya vizuri, msikubali zishike mkia kwa kufelisha wanafunzi, wenye hasara na matokeo mabaya ni ninyi wakazi wa eneo husika na taifa kwa ujumla.

Nachochea tu.

Chanzo: GlobalPublishers
 
Mkuu ninaona hoja yako ni nzuri isipokuwa, kuna sehemu ninaona panahitaji mjadala. Sioni uwiano kati ya failures za shule za serikali na passes za shule binafsi, zinapowianishwa na vita ya matajiri na maskini.

Watu ambao si lazima waitwe matajiri, amabo wengine ni watu wa kawaida sana, wanapeleka watoto wao private schools kwa kufahamu kwamba shule za serikali na serikali kwa ujumla ni silaha ya maangamizi. Hapo hakuna vita kati ya hawa wazazi dhidi ya wale wanaopeleka watoto serikalini ama dhidi ya watoto wenyewe. Hakuna kitu mzazi wa mtoto anayesoma private school amefanya ambacho kinasababisha mtoto wa mwingine apelekwe shule za serikali.

Tatizo lililopo ni juu ya uendeshaji wa shughuli za serikali na pengine ulingwanishwa na ule wa sekta binafsi. Inakuwaje serikali iwe ya ovyo katika nyanja zote? Ukitaka kujua serikali ya Tanzania ni ya ovyo katika kila kitu, usiishie kwenye ufaulu wa elimu tu, naomba uende mbele zaidi utazame vitu kama huduma za afya mahospitalini. Usishangae kuona mtu akiambiwa kwenda ofisi ys serikali no matter ngazi gani, kufuatilia suala lake, anavyoshusha pumzi kama vile amepewa death sentence.

Badala ya kulifanya hili suala vita, ninaomba niwe wazi tu kwamba serikali inalazimika kujifunza uendeshaji kutoka katika sekta binafsi. Kwa nini zinafanikiwa? Badala ya kuwa na mtazamo kama wa muhongo, wenye mwelekezo kwamba kwa kuwa serikali hifanyi vizuri basi serikali itumie nguvu kuweka viwango sawa kwa kuwabana sekta bianfsi, inapaswa kuliangalia kwa namna nyingine. Bila shaka ufaulu mzuri ndicho kiitu tunataka, bilashaka matibabu safi kila mtu anapenda, na bila shaka huduma nzuri mahala popoe kila mtu anataka. La muhimu ni serikali kuinua viwango vyake katika mambo yote ili vikidhi mahitaji ya binadamu na viendane na mahitaii halisi yaliyopo na mipango ya baadaye. Inapawa kuanza upya kutafiti sababu ya uduni wa viwango vya huduman na elimu katika taasisi zake, na kuhakikisha inatatua gatizo hilo mara moja bila usanii wa kugawa marks bure na kuwafaulisha watu wajinga ili kujionyesha infanya vizuri kama yule jamaa aliyepita.

Utafiti ufanyike na si utafiti wa kukaa hotlini kuandiks habari za kubuni na kila uratibu rekebishi ufanyike ili kuhakikisha elimu inayotolewa na taasis za serikali inafikia viwango. Kinyume cha pale, ndiyo kama kila mtu anvyoona products za udom n.k.

Twende pamoja.
 
Back
Top Bottom