mkunyegere
JF-Expert Member
- Aug 21, 2013
- 453
- 93
Kwa muda wa wiki lote hili lililoisha nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana suala la "OPERATION TOKOMEZA UJANGILI". Lakini baada ya kufuatilia kwenye vyombo vya habari nemegundua kuwa hiyo operation haikuwatendea haki wananchi wengi sana wanoishi karibu na hifadhi za Taifa. Sasa basi kwa kuwa uamuzi umeshatilewa kusitisha operation hiyo, na tayari imeleta madhara makubwa sana katika jamii zetu,kwanini waliohusika kusimamia na kuratubu operation hiyo wasiwajibishwe kwa kufikishwa kwenye vyombo vya sharia kwa matumizi mabaya ya madaraka waliyokabidhiwa?