Walimu mnajiangusha wenyewe! Acheni kulalamika!

Nyalotsi

JF-Expert Member
Jul 20, 2011
6,978
5,025
Kuna wadogo zangu ambao ni walimu kwa level ya degree. Wameajiriwa mwezi wa pili mwaka huu. Mshahara wa february hawakupewa wakaambiwa majina hayakwenda hazina,wakakubali. Mwezi wa tatu mishahara ikaja hawakuingiziwa kwenye akaunt zao wakiambiwa namba zao hazipo! Wakaandika barua kuomba waingiziwe wakiorodhesha na account zao,bbda ya siku tatu zikawa tayari. Mwezi uliopita tatizo limejirudia tena na sasa hivi wiki mbili zimeshapita bila kuwekewa fedha zao. Nilipowauliza mnakula nini, wakanijibu tunaishi hivo hivo! Yaani ningekuwa karibu ningewanasa vibao! Unaendaje shule ukiwa na njaa? Ukianguka darasani nani atalaumiwa? Yaani ningekuwa mimi siku ya kwanza tu ya tatizo naandika barua kwa mkurugenzi kumtaari kwamba nitaenda shule mshahara wangu utakapoingia. Huwezi kuwa unaumia kwa makosa ya wengine,lazima ujifunze kupigania haki yako! Huu sio wakati wa kukaa na kumbembeleza mtu akupatie haki yako,idai kwa nguvu zote!
 
ndo maana na cwt wanawakata fedha kila mwaka na matatizo yenu yako pale pale!
 
ualimu ni kama ujinga dunia nzima wanafanana..yaani si kupiga vibao tu..viboko! kama yule mkuu wa wilaya..CWT c wanakula kodi..eti wanaanza kulalamikia serikali kodi kubwa wakati chama kinakula bure..ghorofa imesimama/imejengwa mapato kimya..na sasa viongozi wananunuliana vitara kila mmoja wilayani...ndio maana nsema mawziri wanakazi sana,,zingine hawazijui
 
tchaz, sehem nyngine hawana matatizo. ila wilaya nyingiine sasa, lazima waamke
 
Hiyo ni kweli mkuu yaani waalimu wanazungushwa kwenye haki zao hadi huruma,
kuna walimu wako wilaya ya chato yaani tangu uhakiki ufanyike mwezi january hawajalipwa mshahara hadi sasa na kila wakifatilia majibu ni yaleyale 'bado tunashughulikia hadi leo' na kazini wanaenda
 
Nadhani tatizo liko kwenye baadhi ya halimashauri zetu zilizojaza michwa.
 
Hiyo ni kweli mkuu yaani waalimu wanazungushwa kwenye haki zao hadi huruma,
kuna walimu wako wilaya ya chato yaani tangu uhakiki ufanyike mwezi january hawajalipwa mshahara hadi sasa na kila wakifatilia majibu ni yaleyale 'bado tunashughulikia hadi leo' na kazini wanaenda

thanks god sikusomea ualimu. Nisingevumilia huu upuuzi hata kidogo! Watu wanahold mshahara wako ili uwabembeleze! Wakiingiziwa wenzangu tu,mimi bado,nachukua likizo mpaka utakapoingia. Nilizoea kusikia walimu wa upe ndo wananyanyaswa kiasi hiki,kumbe hata waliosoma? Nini umuhimu wa kupata elimu ni kujikomboa? Pigania haki yako,usisubiri watu wengine wakusaidie.
 
thanks god sikusomea ualimu. Nisingevumilia huu upuuzi hata kidogo! Watu wanahold mshahara wako ili uwabembeleze! Wakiingiziwa wenzangu tu,mimi bado,nachukua likizo mpaka utakapoingia. Nilizoea kusikia walimu wa upe ndo wananyanyaswa kiasi hiki,kumbe hata waliosoma? Nini umuhimu wa kupata elimu ni kujikomboa? Pigania haki yako,usisubiri watu wengine wakusaidie.

poor thinking
 
ualimu ni kama ujinga dunia nzima wanafanana..yaani si kupiga vibao tu..viboko! kama yule mkuu wa wilaya..CWT c wanakula kodi..eti wanaanza kulalamikia serikali kodi kubwa wakati chama kinakula bure..ghorofa imesimama/imejengwa mapato kimya..na sasa viongozi wananunuliana vitara kila mmoja wilayani...ndio maana nsema mawziri wanakazi sana,,zingine hawazijui

poor thinking
 
Mimi nadhani waalimu tunawaonea bure kwa jinsi utaratibu wa kazi ulivo, wengine wilaya za KISHAPU NA SHINYANGA VIJIJINI nao hawakuwepo ktk uhakiki kwani walikuwa masomoni basi ishakuwa taabu kuwarudishia mishahara yoo ingiwa wanavielelezo vyote vinawaruhusu kwenda masomoni. dah shida shida sana salary sleep zinakuja lakini account hazisomi. Cwt wamelala. ndo maana matatizo ya utovu wanidhamu hayaishi mtu hawezi fanya kazi kimbuzimbuzi lazima kuna namna atajilipa au atamwibia mwajiri. YAANI HADI MGAMBO WA JIJI WANAWAZIDI KTK KUDAI MASLAHI YAO AU NDO HAIBA?
 
poor thinking

whats ur suggestion? Au na we ni mmoja ya wanaowanyonya walimu unaogopa wakiamka utakosa ulaji? Kama ni mwalimu basi hata mawazo yako ni mgando hayawezi kuchanganua mambo zaidi ya kukariri vitabu na kuwakaririsha watoto majibu. Itakuwaje mwalimu wiki mbili hujaingiziwa mshahara na unaendelea kwenda shule na fedha zipo wilayani? Au wenzetu kunyanyaswa mnajisikia fahari?
 
Back
Top Bottom