Nyalotsi
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 6,978
- 5,025
Kuna wadogo zangu ambao ni walimu kwa level ya degree. Wameajiriwa mwezi wa pili mwaka huu. Mshahara wa february hawakupewa wakaambiwa majina hayakwenda hazina,wakakubali. Mwezi wa tatu mishahara ikaja hawakuingiziwa kwenye akaunt zao wakiambiwa namba zao hazipo! Wakaandika barua kuomba waingiziwe wakiorodhesha na account zao,bbda ya siku tatu zikawa tayari. Mwezi uliopita tatizo limejirudia tena na sasa hivi wiki mbili zimeshapita bila kuwekewa fedha zao. Nilipowauliza mnakula nini, wakanijibu tunaishi hivo hivo! Yaani ningekuwa karibu ningewanasa vibao! Unaendaje shule ukiwa na njaa? Ukianguka darasani nani atalaumiwa? Yaani ningekuwa mimi siku ya kwanza tu ya tatizo naandika barua kwa mkurugenzi kumtaari kwamba nitaenda shule mshahara wangu utakapoingia. Huwezi kuwa unaumia kwa makosa ya wengine,lazima ujifunze kupigania haki yako! Huu sio wakati wa kukaa na kumbembeleza mtu akupatie haki yako,idai kwa nguvu zote!