Waligombea begi la fedha na wote walikuwa ni vijana wenye nguvu

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,487
13,611
Mwezi uliopita katika maeneo ya posta ya zamani,karibu na forodhani primary school, begi la fedha lilianguka kwa bahati mbaya kutoka kwenye gari iliyokuwa inakatiza. Rundo kubwa la vijana waliibuka barabarani na kuzigombea noti nyingi nyekundu.

Wengine walitoka nyuma ya zile ofisi za kukatia tiketi za boti ziendazo Zanzibar, wengine walitokea karibu na posta ya zamani, wengine walitokea kwenye ile bustani iliyopo mbele ya NBC, ilikuwa ni patashika nguo kuchanika. Hakuna aliyejali magari yaliyokuwa yakikatiza mida ya saa saba mchana, na ni bahati kwamba madereva wa Dar walikuwa wastaarabu, walipunguza mwendo ili vijana wazipambanie noti za bure, wagombee neema iliyowaibukia bila ya kutegemea.

Mwenye nguvu ndiye aliyekula nyama, wale wenye misuli kama mabaunsa waliambua noti nyekundu zaidi ya kumi, wale wembamba waliambulia noti moja. Kitu cha kusikitisha, kwa jinsi nilivyowaona vijana wake, umri wao ni kati ya 18-35. Umri sahihi katika uzalishaji, lakini ubangaizaji ndio unawaweka jijini.

Rais JPM anaposema watu wakalime kwa nguvu ni kwamba anawaongelea aina hiiya vijana. Lakini mimi nadhani kinachotakiwa kufanyika ni kuleta mapinduzi kwenye elimu ya VETA. Kitu cha pili ni kuhakikisha mapitio ya sera ya michezo yanafanyika katika hali ya umakini. Kwani michezo inao uwezo mkubwa wa kuajiri kundi kubwa sana la vijana.

Didier Drogba katika hospitali yake, ameajiri madaktari ambao wanaendesha maisha yao na ya wale watu waliowaajiri majumbani mwao na kwenye miradi yao binafsi.

Maria Mutola mwanariadha wa zamani wa Msumbiji anaendesha taasisi yake huko kwao, anawatengeneza vijana waweze kuwa wakimbiaji kama yeye, kaajiri watu wengi kwenye miradi yake.

Wanariadha wa Ethiopia na Kenya wanaobeba medali kwenye olimpiki, wanategemewa na jamii zao na wanachangia kwa kiasi kikubwa katika kupambana na tatizo la ajira.

Kuwapeleka vijana kwa nguvu kwenda kulima, isiwe ndio suluhisho la mwisho. Yanahitajika mapinduzi kwenye utoaji wa elimu ya ufundi (VETA) pamoja na mapinduzi ya michezo. Mdogo mdogo ipo siku tutafika.
 
Mwezi uliopita katika maeneo ya posta ya zamani,karibu na forodhani primary school, begi la fedha lilianguka kwa bahati mbaya kutoka kwenye gari iliyokuwa inakatiza. Rundo kubwa la vijana waliibuka barabarani na kuzigombea noti nyingi nyekundu.

Wengine walitoka nyuma ya zile ofisi za kukatia tiketi za boti ziendazo Zanzibar, wengine walitokea karibu na posta ya zamani, wengine walitokea kwenye ile bustani iliyopo mbele ya NBC, ilikuwa ni patashika nguo kuchanika. Hakuna aliyejali magari yaliyokuwa yakikatiza mida ya saa saba mchana, na ni bahati kwamba madereva wa Dar walikuwa wastaarabu, walipunguza mwendo ili vijana wazipambanie noti za bure, wagombee neema iliyowaibukia bila ya kutegemea.

Mwenye nguvu ndiye aliyekula nyama, wale wenye misuli kama mabaunsa waliambua noti nyekundu zaidi ya kumi, wale wembamba waliambulia noti moja. Kitu cha kusikitisha, kwa jinsi nilivyowaona vijana wake, umri wao ni kati ya 18-35. Umri sahihi katika uzalishaji, lakini ubangaizaji ndio unawaweka jijini.

Rais JPM anaposema watu wakalime kwa nguvu ni kwamba anawaongelea aina hiiya vijana. Lakini mimi nadhani kinachotakiwa kufanyika ni kuleta mapinduzi kwenye elimu ya VETA. Kitu cha pili ni kuhakikisha mapitio ya sera ya michezo yanafanyika katika hali ya umakini. Kwani michezo inao uwezo mkubwa wa kuajiri kundi kubwa sana la vijana.

Didier Drogba katika hospitali yake, ameajiri madaktari ambao wanaendesha maisha yao na ya wale watu waliowaajiri majumbani mwao na kwenye miradi yao binafsi.

Maria Mutola mwanariadha wa zamani wa Msumbiji anaendesha taasisi yake huko kwao, anawatengeneza vijana waweze kuwa wakimbiaji kama yeye, kaajiri watu wengi kwenye miradi yake.

Wanariadha wa Ethiopia na Kenya wanaobeba medali kwenye olimpiki, wanategemewa na jamii zao na wanachangia kwa kiasi kikubwa katika kupambana na tatizo la ajira.

Kuwapeleka vijana kwa nguvu kwenda kulima, isiwe ndio suluhisho la mwisho. Yanahitajika mapinduzi kwenye utoaji wa elimu ya ufundi (VETA) pamoja na mapinduzi ya michezo. Mdogo mdogo ipo siku tutafika.

Akili ya panya ni shida sana
 
Watu kukimbilia hela za bure ndio kukosa kazi...

Kama ni wapita njia walikuwa wanaenda kwenye shughuli zao je?!
 
Watu kukimbilia hela za bure ndio kukosa kazi...

Kama ni wapita njia walikuwa wanaenda kwenye shughuli zao je?!
Zile ni akili za mwehu! Anataka kutuambia wote wale walikuwa hapo wakisubiri mabegi ya PESA yadondoke? Ukute hata mleta mada naye alizigombea!

JPM katoa mfano wa kulima, lakini zipo pia kazi zaidi ya hizo zinazohitaji kijana kuzifanya!

Eti anataka wapelekwe VETA! Hajui kuwa kati ya hao pia wapo waliokataa shule!? Wanaendaje VETA bila kuwa na sifa? CDM wamebaki kuwa walalamishi tu
 
Mwezi uliopita katika maeneo ya posta ya zamani,karibu na forodhani primary school, begi la fedha lilianguka kwa bahati mbaya kutoka kwenye gari iliyokuwa inakatiza. Rundo kubwa la vijana waliibuka barabarani na kuzigombea noti nyingi nyekundu.

Wengine walitoka nyuma ya zile ofisi za kukatia tiketi za boti ziendazo Zanzibar, wengine walitokea karibu na posta ya zamani, wengine walitokea kwenye ile bustani iliyopo mbele ya NBC, ilikuwa ni patashika nguo kuchanika. Hakuna aliyejali magari yaliyokuwa yakikatiza mida ya saa saba mchana, na ni bahati kwamba madereva wa Dar walikuwa wastaarabu, walipunguza mwendo ili vijana wazipambanie noti za bure, wagombee neema iliyowaibukia bila ya kutegemea.

Mwenye nguvu ndiye aliyekula nyama, wale wenye misuli kama mabaunsa waliambua noti nyekundu zaidi ya kumi, wale wembamba waliambulia noti moja. Kitu cha kusikitisha, kwa jinsi nilivyowaona vijana wake, umri wao ni kati ya 18-35. Umri sahihi katika uzalishaji, lakini ubangaizaji ndio unawaweka jijini.

Rais JPM anaposema watu wakalime kwa nguvu ni kwamba anawaongelea aina hiiya vijana. Lakini mimi nadhani kinachotakiwa kufanyika ni kuleta mapinduzi kwenye elimu ya VETA. Kitu cha pili ni kuhakikisha mapitio ya sera ya michezo yanafanyika katika hali ya umakini. Kwani michezo inao uwezo mkubwa wa kuajiri kundi kubwa sana la vijana.

Didier Drogba katika hospitali yake, ameajiri madaktari ambao wanaendesha maisha yao na ya wale watu waliowaajiri majumbani mwao na kwenye miradi yao binafsi.

Maria Mutola mwanariadha wa zamani wa Msumbiji anaendesha taasisi yake huko kwao, anawatengeneza vijana waweze kuwa wakimbiaji kama yeye, kaajiri watu wengi kwenye miradi yake.

Wanariadha wa Ethiopia na Kenya wanaobeba medali kwenye olimpiki, wanategemewa na jamii zao na wanachangia kwa kiasi kikubwa katika kupambana na tatizo la ajira.

Kuwapeleka vijana kwa nguvu kwenda kulima, isiwe ndio suluhisho la mwisho. Yanahitajika mapinduzi kwenye utoaji wa elimu ya ufundi (VETA) pamoja na mapinduzi ya michezo. Mdogo mdogo ipo siku tutafika.
Mawazo yako sio ya magufuli, gombea urais na wewe ufanye hayo unayoyataka wenzako hapo ndio mwisho wao wa kufikiri
 
Magufuli amewabadilishia gia angani vijana. Kutoka tanzania ya viwanda mpaka tanzania ya kulima
Viwandani utapeleka hizo Goroli zako mbili!? Au unadhani malighafi za viwandani ni hizo porojo zako!?
 
Zile ni akili za mwehu! Anataka kutuambia wote wale walikuwa hapo wakisubiri mabegi ya PESA yadondoke? Ukute hata mleta mada naye alizigombea!

JPM katoa mfano wa kulima, lakini zipo pia kazi zaidi ya hizo zinazohitaji kijana kuzifanya!

Eti anataka wapelekwe VETA! Hajui kuwa kati ya hao pia wapo waliokataa shule!? Wanaendaje VETA bila kuwa na sifa? CDM wamebaki kuwa walalamishi tu
Uliyoyasema ni ya msingi na ndio nilichotaka kusema

Lakini sasa CDM imeingiaje hapo?
 
Zile ni akili za mwehu! Anataka kutuambia wote wale walikuwa hapo wakisubiri mabegi ya PESA yadondoke? Ukute hata mleta mada naye alizigombea!

JPM katoa mfano wa kulima, lakini zipo pia kazi zaidi ya hizo zinazohitaji kijana kuzifanya!

Eti anataka wapelekwe VETA! Hajui kuwa kati ya hao pia wapo waliokataa shule!? Wanaendaje VETA bila kuwa na sifa? CDM wamebaki kuwa walalamishi tu
Kaka tumia lugha ya kiungwana, usilete hasira zako kwenye hii thread, asilimia kubwa ya vijana waliogombea hizo fedha ni wale wanaoshinda kwenye ile bustani, wengine wanashinda maeneo ya baharini. Nilichokiandika nimekiandika kwa lengo pana zaidi ya kuwazungumzia vijana wale peke yao. Tembea maeneo mengi ya Dar itaona vijana wengi wamekaa idle mchana bila ya kufanya lolote, linapotokea gari linaloangusha mfuko wa fedha hawawezi kujiuliza mara mbili. Ninao uhakika wengi wa wale waliogombe zile fedha hawana kazi, na ndio lengo la thread.
 
Back
Top Bottom