Wale funza wa miguu waliishia wapi?

Braza Kede mara ya mwisho lini kufika Kigoma? Maeneo ya Manyovu, uvinza, Kakonko Nyakanazi n.k
Huko bado funza wametia kambi
Funza ni Wadudu wenye asili ya America ya Kusini na ya Kati. Walikuja Africa kwa kupitia meli za Wareno na waathirika wa kwanza walikuwa Angola.

Ni bahati mbaya kama bado wapo Kigoma lakini kwa sehemu kubwa ya jamii za Kitanganyika hawa wadudu wasumbufu kwa binadamu wametokomezwa kabisa
 
Kama ushawahi kuona mtu ana funza au walikushambuli bas ni muda sahihi wa kuandika wosia watu wagawane Mali zako
 
Hawa hapa
Hawa hapa:
 
Braza Kede mara ya mwisho lini kufika Kigoma? Maeneo ya Manyovu, uvinza, Kakonko Nyakanazi n.k
Huko bado funza wametia kambi
ndio inawezekana siwezi kukubishia kwa hilo. ila nachojua kwa maeneo mengi ya nchi wadudu hawa hawapo tena.
 
Funza n noma Sana kipindi hicho Ludewa uko funza wa kutosha,wakizidi kweli mguu unapinda, asubuhi huwa Wana washa miguu
Haahaa ni kweli wakiingia kuna kamuwasho fulani katamu ila ukizubaa tu kusikilizia ladha ya huo utamu unakuta ameshataga mayai na ana watoto tayari [emoji1]
 
Matumizi ya maji na sabuni yamechangia sana kupungua kwa funza ingawa bado wapo sehemu zilizosahauliwa, zisizo na lami. Funza chawa na kunguni ni kielelezo cha uchafu wa mwili na kutokujali kanuni za afya.
labda kuna sababu zingine kiongozi ila ivyo vyote havikuwa shida vilikuwepo
 
Kwanza nimshukuru raisi wa awamu ya sita kwa kuhakikisha Jamii yetu inapitia mabadirko makubwa, mbili nimshukuru kuwapa afya njema viongozi wetu wa serikali haswa makamu wa raisi na waziri mkuu,
Niseme bila yeye Funza wangekuwepo mpaka leo hii
 
Daah ila stori zingine bwana🤣🤣 kwamba funza inafanya miguu ipinde?
 
Mliteseka sana poleni aisee!!
-kiongozi shida hazijawahi kuisha.
-maisha ya wkt huo yalikuwa mazuri tu tena pengine bora zaidi ya leo hii.
-mambo mengi tu mazuri yaliwepo. watu wakiishi kwa ubinadam/utu/uaminifu/unyenyekevu halisi. watu wengi wazuri walikuwepo.
-watu hawakuwa wengi km leo.
-hewa safi ya kutosha ilikuwepo.
-heshima iliitangulia pesa.
kwa mazingira ya leo sio rahisi sana ukamuelezea mtu akaelewa ila ni hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…