Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,178
- 162,654
Leo nimesikiliza kipindi cha magazeti kupitia Channel 10 lakini nimeshangazwa sana na kitu kimoja.
Kama mnavyofahamu,Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu hapa nchini,jana walitoa tamko kupinga katiba kwa kigezo cha mahakama ya kadhi kutokuwepo katika katiba inayopendekezwa.
Binafsi, sikubaliana na msimamo wa jumui hizo lakini kinachonishangaza ni kuona habari hii imepewa kisogo na magazeti mengi isipokuwa matatu ambayo ni Tanzania Daima,Jambo Leo na The Guardian tu.Mwananchi halikusomwa.
Yaani hii habari kwa wahariri wengi kwao si habari!Magazeti ya serikali ndio kabisa yote yamekwepa kuripoti habari hii.
Nilitarajia hii habari kama sio kuwa habari kuu,basi ingepewa walau hata uzito mdogo lakini hali imekuwa tofauti kabisa utadhani hili ni jambo dogo sana lisilo na athari yoyote kwa taifa hili.
Hivi hii tamko si jambo zito kwa upande wa katiba inayopendekezwa?Mnangoja waanze kujadili misikitini ndio mripoti?
Waandishi, kuficha vitu vingine ni kujidanganya tu kwani vinagusa umma moja kwa moja na vina impact kubwa sana.Leo mtaficha hii habari lakini ni nyinyi hao hao ambao kesho na keshokutwa mtakuja kuripoti yatokanayo na tamko hilo na hapo sijui mtakuwa mmekwepa nini?
Hatua hii ni sawa na kujaribu kuficha moto wakati moshi unafuka.Uamuzi wenu hauisadii serikali wala umma bali ni kujidanganya tu.Timizeni wajibu wenu.
Kama mnavyofahamu,Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu hapa nchini,jana walitoa tamko kupinga katiba kwa kigezo cha mahakama ya kadhi kutokuwepo katika katiba inayopendekezwa.
Binafsi, sikubaliana na msimamo wa jumui hizo lakini kinachonishangaza ni kuona habari hii imepewa kisogo na magazeti mengi isipokuwa matatu ambayo ni Tanzania Daima,Jambo Leo na The Guardian tu.Mwananchi halikusomwa.
Yaani hii habari kwa wahariri wengi kwao si habari!Magazeti ya serikali ndio kabisa yote yamekwepa kuripoti habari hii.
Nilitarajia hii habari kama sio kuwa habari kuu,basi ingepewa walau hata uzito mdogo lakini hali imekuwa tofauti kabisa utadhani hili ni jambo dogo sana lisilo na athari yoyote kwa taifa hili.
Hivi hii tamko si jambo zito kwa upande wa katiba inayopendekezwa?Mnangoja waanze kujadili misikitini ndio mripoti?
Waandishi, kuficha vitu vingine ni kujidanganya tu kwani vinagusa umma moja kwa moja na vina impact kubwa sana.Leo mtaficha hii habari lakini ni nyinyi hao hao ambao kesho na keshokutwa mtakuja kuripoti yatokanayo na tamko hilo na hapo sijui mtakuwa mmekwepa nini?
Hatua hii ni sawa na kujaribu kuficha moto wakati moshi unafuka.Uamuzi wenu hauisadii serikali wala umma bali ni kujidanganya tu.Timizeni wajibu wenu.