Wachungaji wa makanisa binafsi mjiheshimu kulinda maadili ya kanisa

Wachungaji wa makanisa binafsi mjiheshimu kulinda maadili ya kanisa

uwe hodari

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2022
Posts
4,041
Reaction score
8,633
Ukristo duniani kote unaendeshwa kwa upendo,amani na kuvumiliana

Ila wachungaji wa makanisa binafsi wanafanya mambo yaliyovuka kiwango cha ibada na kuonekana zaidi kama wanafanya vituko

Naamini wachungaji wengi walikuwa na lengo la kumtumikia na Kutangaza injili ya krstu walipoanza malengo yao ila kwa namna moja ama nyingine wengi wamepotoka njiani na kuanza kufanya ujinga na vituko kanisani

Nilimsikia dada mmoja anajiita mchungaji anahubiri yeye ni mchungaji akiwa kanisani tu ila akiwa chumbani anayaachia yote km mwanamke

Nikijisikia vibaya kwa kweli kuhusu ile clip kwasababu kwa mazingira pale walionekana wapo kwenye Ibada

Ingelikuwa wapo kwenye semina ya ndoa angeyazungumza hayo wala isingekuwa ajabu kwasababu angekuwa anakutana na watu wanaojiandaa kuingia kwenye ndoa

Imagine umejiandaa jumapili kwenda kwenye ibada unakutana na dada mmoja mpuuzi km huyu anahubiri sex kwenye saa za Ibada takatifu

Niliona yupo comfortable kabisa kwasababu ule umma wa waumini wake waliokuwa wanamsikiliza hawakuonesha reaction ya kutokupenda maongezi yake yasio maana

Niliona Pia clip nyingine mchungaji anawalisha matango waumini wako eti

"mwaka 2024 utakuwa mwaka wa mafanikio kwasababu unagawanyika kwa mbili"

Ni mchungaji fulani alikula suti yupi calm kabisa anaropoka haya

Sasa nukajiuliza ni wapi Biblia Takatifu imenukuu miaka ya neema kuwa ni ile inayogawanyika kwa mbili?

Ni bora hata angekusia kuhusu mstari ya Biblia Takatifu kuhusu miaka Saba ya neema na Miaka saba ya njaa ( kuwa maisha yamegawanyika ktk vipindi viwili kwenye kila jambo)

Lkn yeye aliishia kusema tu mwaka 2024 utakuwa mwaka wa mafanikio kwa kuwa unagawanyika kwa mbili
Bahati mbaya mpiga picha hakuonyesha waumini wake nione muitikio wa ile kauli

Kiufupi huyu mchungaji aliokota maneno ya mtaani tu kuhusu assumption zake

Haya makanisa binafsi mengi yanaenda ili mradi hakuna litrujia

Mchungaji anaanza kuongea saa nne asubuhi hadi saa tisa alasiri? Inahuruma nini zaidi ya kusababisha watu waanze kusinzia kanisani? Na maana ya ibada kutopotea?

Kila kitu kina utaratibu wake tengenezeeni mpangilio wa ibada mnaboa kwa kweli

Wengi wa wahanga wa hizi ibada ni wanawake wanaondoka na watoto nyumbani asubuhi kurudi nyumbani usiku


Wakristo wengi hawajui km kuomba na kujiombea binafs kuna nguvu sana kuliko kwenda kupokea mafundisho ya sio na kichwa wala miguu kwa wachungaji watafuta riziki

Kwanza mwanamke unakuwaje mchungaji?
 
Imagine hata Masanja nae ana kanisa
anahubiri akiwa kavaa mlegezo

Ukristo ndani ya miaka 50 tu utakuwa kituko, ila ndio muda huo Yesu atarudi kutimiza andiko kwamba siku za mwisho anapokaribia kurudi kutakuwa na wachungaji feki wengi sana.
 
Wachungaji wenyewe ndio kama huyu??
images (50).jpeg
images (49).jpeg
 
Ndo maana mim ntapooa kigezo mojawapo hatakiw awe anasali madhehebu binafsi au kanisa binafsi ambalo sio taasisi
 
Ukristo umeharibiwa sana na shetan na bado wachungaji weng sana wanatumia nguvu za giza kuwa na waumin wengi dah
 
Ukristo duniani kote unaendeshwa kwa upendo,amani na kuvumiliana

Ila wachungaji wa makanisa binafsi wanafanya mambo yaliyovuka kiwango cha ibada na kuonekana zaidi kama wanafanya vituko

Naamini wachungaji wengi walikuwa na lengo la kumtumikia na Kutangaza injili ya krstu walipoanza malengo yao ila kwa namna moja ama nyingine wengi wamepotoka njiani na kuanza kufanya ujinga na vituko kanisani

Nilimsikia dada mmoja anajiita mchungaji anahubiri yeye ni mchungaji akiwa kanisani tu ila akiwa chumbani anayaachia yote km mwanamke

Nikijisikia vibaya kwa kweli kuhusu ile clip kwasababu kwa mazingira pale walionekana wapo kwenye Ibada

Ingelikuwa wapo kwenye semina ya ndoa angeyazungumza hayo wala isingekuwa ajabu kwasababu angekuwa anakutana na watu wanaojiandaa kuingia kwenye ndoa

Imagine umejiandaa jumapili kwenda kwenye ibada unakutana na dada mmoja mpuuzi km huyu anahubiri sex kwenye saa za Ibada takatifu

Niliona yupo comfortable kabisa kwasababu ule umma wa waumini wake waliokuwa wanamsikiliza hawakuonesha reaction ya kutokupenda maongezi yake yasio maana

Niliona Pia clip nyingine mchungaji anawalisha matango waumini wako eti

"mwaka 2024 utakuwa mwaka wa mafanikio kwasababu unagawanyika kwa mbili"

Ni mchungaji fulani alikula suti yupi calm kabisa anaropoka haya

Sasa nukajiuliza ni wapi Biblia Takatifu imenukuu miaka ya neema kuwa ni ile inayogawanyika kwa mbili?

Ni bora hata angekusia kuhusu mstari ya Biblia Takatifu kuhusu miaka Saba ya neema na Miaka saba ya njaa ( kuwa maisha yamegawanyika ktk vipindi viwili kwenye kila jambo)

Lkn yeye aliishia kusema tu mwaka 2024 utakuwa mwaka wa mafanikio kwa kuwa unagawanyika kwa mbili
Bahati mbaya mpiga picha hakuonyesha waumini wake nione muitikio wa ile kauli

Kiufupi huyu mchungaji aliokota maneno ya mtaani tu kuhusu assumption zake

Haya makanisa binafsi mengi yanaenda ili mradi hakuna litrujia

Mchungaji anaanza kuongea saa nne asubuhi hadi saa tisa alasiri? Inahuruma nini zaidi ya kusababisha watu waanze kusinzia kanisani? Na maana ya ibada kutopotea?

Kila kitu kina utaratibu wake tengenezeeni mpangilio wa ibada mnaboa kwa kweli

Wengi wa wahanga wa hizi ibada ni wanawake wanaondoka na watoto nyumbani asubuhi kurudi nyumbani usiku


Wakristo wengi hawajui km kuomba na kujiombea binafs kuna nguvu sana kuliko kwenda kupokea mafundisho ya sio na kichwa wala miguu kwa wachungaji watafuta riziki

Kwanza mwanamke unakuwaje mchungaji?
Wa maombezi ya "shakabobobasherukanda" walitakiwa wasiwe hata na Muumini mmoja maana ni utapeli usiofichika.

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.
 
Back
Top Bottom