Wachambuzi:Trump hawezi kuishambulia N/Korea Haraka, hizi hatua 3 kabla hajafikiria Vita na Kim

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,735
Pamoja na Mikwara yote inayoendelea mipango ya Trump kufanya ambacho wenzake wameshindwa inakutana na Ukomo mapema sana.

ZIFUATAZO NDIO NJIA ZA AWALI KABLA YA VITA
1:Vikwazo vikali vipya vya Kiuchumi kwa N/Korea
N/Korea ndio nchi duniani yenye vikwazo vingi lakni bado imekuwa na Uwezo wa kutengeneza silaha hatari.
Sasa Trump kuwakomesha anafikiria kuzuia ndege zao zote kutokwenda mataifa mengine, Kuzuia mafuta kuingia nchni humo, Kuzizuia meli zake kutokukatiza bahari yoyote Ile, na Kuziadhibu na kuzikataza bank zote za China kufanya biashara na N/Korea (hapo pagumu)

2:Mashambulizi ya Virus kweny mitandao yote ya kijeshi Kwa kushirikiana na Israel

Anatarajia kufanya Israel walichowafanyia iran kwa kuwaingizia kirus hatari Stuxnet kuharibu mtambo ya Nuclear. Jaribio hili tayari US wamekwishafeli kila walipojaribu. Ikumbukwe N/Korea kikosi kinachopendwa na kulipwa mshahara mkubwa na marupurupu mengi ni kikosi cha jeshi la mtandao. Huko wamejidhatiti vilivyo na wanamitandao yao tofauti na hii ya kawaida. Kikosi Chao maarufu kama Bureau 121.
Kuna sintofahamu mbili wapo wanasema kufeli kwa Jaribio juzi ni matokeo ya shambulizi la mtandao kutoka US, wengine wanasema wao wenyewe walifanya makusudi ili tu kumuonyesha Trump japo hawakua na Nia ila wamefanya kile ambacho Trump alipaswa kujibu kijeshi lkn hadi sasa mzee Trump yuko kimya.
Inasemekana US wako katika mradi wa kutengeneza mfumo wa kuyahujumu mabomu ya masafa marefu ya adui zake kabla au wakati wa kuruhusiwa shambulizi badala ya kufunga mamitambo ya kukinga makombora.

3:Njia ya Tatu ni Mazungumzo
Miaka Saba Sasa toka mazungumzo Kati ya US na N/Korea yamefeli, njia hii hajawahi kusemwa waziwazi na Trump anaonekana kutoipa kipaumbele lakn wachina ndio wanaipendekeza zaidi kwa US.

4:Utata wa Kuivamia Kijeshi na kuifanya njia hii kuwa ngumu kwa US

Njia hii ni tata na inalenga kwanza kuzuia bahari Kim asifanye Jaribio la kombora lolote. Pili Kumpindua kabisa kijana Kim na kuukomesha utawala wake.

Tatizo haijulikani hawa N/Korea watajibu vipi hata kwa shambulio dogo tu kutoka US maana tayari wameshasema watashambulia kwa nguvu zao zote. Shambulio lolote lile linawaweka katika hatari raia zaid ya Mil 20 wa Korea kusini ambao wako ndani ya Range ya mabomu na vifaa lukuki vya kijeshi vilivyopangwa kwa ustadi mpakani vikisubiri amri. Wanatishia hadi kuisambaratisha ikulu ya S/Korea.
Ndio maana mshauri wa ulinzi wa Trump anasema nguvu ya kijeshi ni ya mwisho kabisa...

MAREJEREO
Factbox: Despite tough talk on North Korea, Trump's options limited
 
Zote hizo ni hisia tu.

Anachotafuta US ni sababu kamili za kuipiga NK, kwani mpaka sasa hakuna uhalali wa kumpiga NK.
Marekani anajua kuwa ili hii vita iwe rahisi kwake ni kushambulia kwa njia ya anga, na nilazima US atupe makombora yake kila sehemu anayohisi kuwa kuna silaha za NK.
Na kwakufanya hivyo US atauwa wakorea wengi (raiya) na hilo tukio litapelekea UN kuilaumu US kwa kukiuka haki za kibinahadamu.

Kama njia/sababu itapatikana, Mf:- NK akajitoa ufahamu na kuzishambulia meli za US zilizopo katibu na fukwe zake, hapo ndio itakuwa nafuu ya US kwani atakuwa ameshabata njia ya kujitetea baada ya vita.

Ikumbukwe kwa sheria za NK kila raiya anayefikisha umbri wa miaka 18 ni lazima kujiunga na jeshi, na pindi taifa lao linapoingia kwenye habari/vita basi kila raia mwenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea hukabiziwa kombati na mtutu ili kupigana nchi yake.
Sasa hapo inamaana vita ikianza Marekani hana budu kuuwa watu wengi ili kuondoa upinzani.



Pasaka njema
 
kauli ya pensi leo hii ni shahiri kua US wataipiga north korea na hakuna wa kuingilia
 
China Kinga yake ni North korea hwmawezi kuruhusu jamaa apigwe kirahisi hivyo. Si mnakumbuka vita umya 1950
 
Tukiwa tunaendelea na uchambuzi wetu kwa kile kinachoendelea eneo la Asia Pacific leo tutakijita kwenye kitengo cha intelligence kitengo number moja ktk uwanja wa mapambano hasa ktk ukusanyaji wa taarifa za kijeshi na Usalama wa adui wako

Dunia nzima kuna taasisi 3 za kijasusi zinazosikika sana kutokana na operation zake na pia watu wengi kufatilia sana taarifa zinazotoka kwenye taasisi hizi
1 CIA 2 Mossad 3 MI6 japo zipo nyingine lakini hzi zimekuwa maarufu sana sasa leo tutakijita kwenye CIA japo zipo taarifa nying hapa jukwaani zikielezea CIA mm sito kuwa hapa kuelezea sana lakini tutakijita kwenye kile kinachoendelea eneo la Asia Pacific

Central intelligence agency (CIA) ni moja ya taasisi kubwa sana duniani ya intelligence wakiwa na vitengo vitano

1Digital invasion
2 Analysis
3 Operations
4 support
5 Scienceand technology

Sasa leo tujikite kwenye kitengo cha OPERATIONS kitengo chenye majukumu ya kukusanya foreign intelligence kwa kutumia (HUMINT SOURCE) au human intelligence kwani kazi ya kukusanya intelligence kwa njia ya kisasa yani technology intelligence ni kazi ya National Security Agency ( NSA ) ndio wenye wajibu wa kukusanya taarifa za intelligence kutumia vitu pendwa na wana mabingwa ktk fani hizo kama
1 Lingwist
2 Computer scientist
3 Analyst
4 Mathematician
5 Voice Interpreters
Mpaka mwaka 1992 nchi nyingi zilijikita kwenye technology intelligence sana kuliko human intelligence japo human intelligence ndio 100% kwa usahihi wa taarifa kwani mpaka leo hakuna mtu akiweza kumuhack binadamu lakini system zinaweza kuwa hacked na kuleta false information sasa kutokana na kukua kwa technology NSA ndio intelligence agency yenye Bajeti kubwa na wafanyakazi wengi kuliko agency zingine 17 zilizo kwenye Intelligence Community ambazo ni muunganiko wa intelligence zote ndani ya US

Sasa tukiangalia kile kijulikanacho kama CIA activities in North Korea zinaonekana ni kuanzia mwaka 1949,1950,1980 na 1996 na nying zinahusisha Russia naweza nukuu chache

1 "In the 16 July 1949 Weekly Summary, the Agency describes North Korea as a Soviet puppet regime. On 29 October, a Weekly Summary states that a North Korean attack on the South is possible as early as 1949, and cites reports of road improvements towards the border and troop movements there.

2 On 6 June, CIA reported another interesting international development: all East Asian senior Soviet diplomats were recalled to Moscow for consultations. The CIA believed the purpose of the recall was to develop a new plan to counter anti-Communist efforts in the region.
3 On 2 February, Director of Central IntelligenceJohn Deutch tells a US Senate Select Committee that North Korea is developing long-range missiles. The United States, according to Deutch, should focus on stopping North Korea from acquiring guidance-and-control technology that could make its long-range missiles more accurate and lethal.
Zipo nying lakini hzo ni chache tu lakini ni miaka hyo nilivyosema hapo mwanzo

NORTH KOREA Duniani sifa kubwa ya kuwa na intelligence nzuri moja wapo ni kuhakikisha siri za serikali na nchi azitoki nje au kuwafikia maadui na Korea ndio nchi pekee Duniani ambayo ni ngumu sana kujua kinachoendelea ndani ya Pyongyang yanayofanikiwa kutaka ni machache sana na mengi hayana uhakika kama ni 100% ya ukweli so ktk hapo tunawasifu kwa intelligence yao kufanya kazi nzuri sana kwa kuweza kuprotect taarifa za nchi yao kwa maadui kujua

Ndani ya Korea kuna vitengo vitatu ambavyo ni
1 People's Security
ambao kazi yao ni kudeal na internal Security , Social control na basic Police

2 Borders Guard
ambao ni kikosi maalum cha makomando unapofuzu kuwa komando wa North Korea si mchezo wewe jiulize ndio nchi yenye wanajeshi wengi duniani na jeshi la akiba pekee ni watu milion 8 sasa mpaka Uwe komando utakuwa ni mtu wa aina gani

3 State Security
kikosi maalum cha askari ambao kazi yao ni intelligence na kuhakikisha nchi inakuwa safe na siri za serikali zinakuwa safe hawa wanareport moja kwa moja kwa Kim wakimwambia fulani anatakiwa kufa kwa ajili ya National security bhasi hata akiwa mjomba wa Kim ni kitanzi tu .
Sasa bila ya kuwa na taarifa sahihi za intelligence ya nchi unayotoka kupigana nayo ni hatari sana kwani kuna kitu kinaitwa Priemtive Strike (PS) ni mashambulizi ambayo yanafanyika kwenye maeneo yenye vifaa au silaha za kijeshi nzito ambapo mara nying taarifa za maeneo hayo zinatoka kwenye Intelligence mara nying Israel anafanya Priemtive Strike kwenye eneo la Middle East kwenye vinu au mitambo ya nuclear kwenye nchi za Middle East je US anazo taarifa za kutosha za kijeshi na intelligence za North Korea kwani ni ngumu kwenda kupigana na mtu ambae ujui ana silaha gani kwenye ghala lake kwani unaweza kwenda na SMG kumbe mwenzio anakusubili na RPG

Jamani Marekani anatisha hakuna nchi yeyote Duniani ambapo marekani wakiipiga biti wakakomaa tumeona China,Russia wakati mwingine wanakuwa wapole mbele ya American Eagle lakini Kim au Korea kaskazini ndio wamekosa adabu mbele ya huyu Police wa dunia mfano leo IGP anakuja kumtamata mtuhumiwa lakini mtuhumiwa amwogopi akiambiwa kaa chini yeye anasimamia akiambiwa kaa kimya yeye anapiga kelele kama IGP inatakiwa ujiulize maswali matatu kichwan mwako
1 mtuhumiwa ni chizi
2 mtuhumiwa hana cha kupoteza na yupo tayali hata kufa

3 mtuhumiwa anawatu nyuma yake ambao wapo tayali kumtetea au kupigana na ww ila walikuwa wanakutafutia sababu
ze kokuyo
Nalendwa
 
Zote hizo ni hisia tu.

Anachotafuta US ni sababu kamili za kuipiga NK, kwani mpaka sasa hakuna uhalali wa kumpiga NK.
Marekani anajua kuwa ili hii vita iwe rahisi kwake ni kushambulia kwa njia ya anga, na nilazima US atupe makombora yake kila sehemu anayohisi kuwa kuna silaha za NK.
Na kwakufanya hivyo US atauwa wakorea wengi (raiya) na hilo tukio litapelekea UN kuilaumu US kwa kukiuka haki za kibinahadamu.

Kama njia/sababu itapatikana, Mf:- NK akajitoa ufahamu na kuzishambulia meli za US zilizopo katibu na fukwe zake, hapo ndio itakuwa nafuu ya US kwani atakuwa ameshabata njia ya kujitetea baada ya vita.

Ikumbukwe kwa sheria za NK kila raiya anayefikisha umbri wa miaka 18 ni lazima kujiunga na jeshi, na pindi taifa lao linapoingia kwenye habari/vita basi kila raia mwenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea hukabiziwa kombati na mtutu ili kupigana nchi yake.
Sasa hapo inamaana vita ikianza Marekani hana budu kuuwa watu wengi ili kuondoa upinzani.



Pasaka njema
Ni kweli Kila kijana mwenye umri kuanzia miaka 18 kapitia mafunzo ya jeshi, lakini kumbuka siyo watu wote wanaipenda serikali na kuunga mkono lazima kuna kikundi kinasubiria Kwa hamu kuchukua madaraka Aidha kipo ndani au nje ya Nchi.
 
Dunia yenyewe inaogopa na haijui USA ataifanya Nini Korea...Wewe wa mbande umekazana USA atapigwa USA atapigwa....Kumbuka USA ndo nchi yenye NGUVU KUBWA za KIJESHI DUNIANI na ndo nchi yenye NGUVU za KIJESHI za ziada.....Mfano tu Kama Ana ndege zaidi ya 6000 za KIJESHI Tena zenye teknolojia ya Hali ya juu hebu pata picha Nini kitamkuta kipank....
 
Sasa leo tujikite kwenye kitengo cha OPERATIONS kitengo chenye majukumu ya kukusanya foreign intelligence kwa kutumia (HUMINT SOURCE) au human intelligence kwani kazi ya kukusanya intelligence

Samahani mkuu izzo,
nimechukua kipande hiki ili kibebe maoni yangu ; Ni kwamba katika hicho kitengo cha OPERATIONS kwa HUMINT SOURCE Marekani na Marafiki zake huwa wanatumia mara nyingi vikundi vya misaada ya kibinadamu kama matibabu,mavazi, mahema na vyakula kwenye majanga kama matetemeko, mafuriko au majanga yoyote ya asili au ya kutengenezwa ,kwa kisingizio cha kutoa misaada kwa waathirika.

Ilishawahi kutokea miaka michache iliyopita sikumbuki hasa ni ipi, Iran ilikumbwa na tetemeko la Ardhi kubwa sana, Marekani akaona nimepata upenyo niingize inzi wangu. Uongozi wa Iran ukataa msaada wao.

Na ndiyo maana miaka ya karibuni Marekani wakimtumia mbwa wao South Korea walipiga propaganda sana kwamba North Korea imekumbwa na majanga ya njaa sana, ili tu wajifanye kupeleka misaada ya kibinadamu.
 
PLANS TO DESTROY MISSILE SITES

DONALD Trump is considering “utterly destroying” Kim Jong-un’s nuclear sites, according to one of the President’s closest military advisers.

A source told British diplomats that America could launch pre-emptive strikes and has the firepower to smash North Korea’s nuclear program.

President Trump wants to heap pressure on China by making it clear that the US will take military action against the secretive country.


×*************×
The Times reported that senior sources said the American armed forces could “utterly destroy” North Korea’s key nuclear targets using conventional weapons.

×**************×
Trump weighs strike on Kim’s nuke sites
 
Pamoja na yote kwenye mambo haya ya vita na tetesi za vita, uongo huwa ni mwingi kuliko ukweli na uhalisia.
Tukumbuke kidogo ww2, uingeleza waliidanganya ujerumani na dunia kwa ujumla kuwa mapirot na wanajeshi wake walikuwa wanakula carrot ndio maana waliweza kuona usiku sana, hata makombora waliyaona kabla hayajafika kumbe ukweli walikuwa wamegundua rada lkn wakaificha watu wengine wasijue siri ya uwezo wao kuona usiku.

Hadi leo wabongo wanakula karoti ili waone saana kama masalia ya ufake Ule. Tutegemee uongo story fake nyingi sana ktk tetesi hizi za vita vinavyosadikika kunukia korea.
 
Hiyo namba mbili sidhani kama itawezekana ukizingatia NK wana bureau 121 hata Trump anaijua hii
 
Pamoja na yote kwenye mambo haya ya vita na tetesi za vita, uongo huwa ni mwingi kuliko ukweli na uhalisia.
Tukumbuke kidogo ww2, uingeleza waliidanganya ujerumani na dunia kwa ujumla kuwa mapirot na wanajeshi wake walikuwa wanakula carrot ndio maana waliweza kuona usiku sana, hata makombora waliyaona kabla hayajafika kumbe ukweli walikuwa wamegundua rada lkn wakaificha watu wengine wasijue siri ya uwezo wao kuona usiku.

Hadi leo wabongo wanakula karoti ili waone saana kama masalia ya ufake Ule. Tutegemee uongo story fake nyingi sana ktk tetesi hizi za vita vinavyosadikika kunukia korea.
hahaha, itabidi tule corot kwa wingi tuwaone malawi
 
Back
Top Bottom