Wabunge wampa makavu Waziri Kitwanga, Masha aonyesha umbumbumbu

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997

Siku moja baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga kutimuliwa nafasi hiyo kwa ulevi, wabunge na wasomi wameendelea kumbana zaidi wakisema hatua hiyo ya Rais imechelewa.

Wapinzani wamekuwa wakimtaka Rais amuondoe kwenye nafasi hiyo kutokana na kuhusishwa na Kampuni ya Infosys ambayo ilitoa ushauri kwa Kampuni ya Lugumi Enterprises iliyopewa zabuni ya kufunga vifaa vya kuchukua alama za vidole (AFIS) katika vituo vya polisi.

Wakati wasomi wakisema hayo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema uamuzi huo ulikuwa sahihi na swali ambalo Kitwanga hakulijibu vizuri kutokana na hali ya ulevi, litapaswa kujibiwa upya baada ya wabunge kuomba mwongozo wa swali hilo.

Majaliwa alisema Rais ametengua uteuzi wa Kitwanga kuanzia juzi baada ya kuonekana amelewa wakati wa kazi.

“Na hili lilibainika pale alipokuwa akijibu maswali ya wizara yake...,”alisema Majaliwa.

Alisema uamuzi wa Rais Magufuli umefuata kanuni za utumishi wa umma ambazo zinakataza mtumishi kulewa akiwa kazini.

Ingawa Majaliwa hakutaja kanuni hiyo, Kifungu cha 34 cha Sheria ya Utumishi wa Umma ya Mwaka 2002 pamoja na Kanuni ya 65 (1) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za Mwaka 2003, kinasema, “Watumishi wa Umma wanapaswa kuepuka tabia ambayo inavunja heshima ya utumishi wao kwa umma hata wanapokuwa nje ya mahali pa kazi."

Tabia inayoweza kuvunja heshima hiyo inatajwa kuwa ni pamoja na matumizi ya dawa za kulevya, ulevi, kukopa kwa kiwango ambacho hawawezi kurejesha na mwenendo mbaya na kujihusisha na vitendo vyovyote viovu mbele ya jamii.

Bunge kuchukua hatua?
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah alipoulizwa adhabu ambazo mbunge anaweza kupata iwapo ataingia bungeni akiwa amelewa, alisema wanaoweza kujibu hilo ni Waziri Mkuu ambaye ni kiongozi wa shughuli za Serikali bungeni na Mnadhimu wa Serikali Bungeni, Jenister Mhagama.

Hata hivyo, Mhagama ambaye ni Waziri Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, alisema hawezi kueleza hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa kuwa tayari Rais ameshachukua uamuzi wa kutengua uteuzi huo.

“Ila Bunge lina taratibu na kanuni zake, nadhani Spika au katibu wa Bunge watakueleza vizuri,” alisema Mhagama.

Spika Job Ndugai hakupatikana kwenye simu, huku Naibu Spika simu yake iliita bila kupokewa.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel alisema: “Kanuni hazijaweka utaratibu wa mbunge anayeingia bungeni amelewa ila kuhusu suala la Kitwanga ni la nidhamu ya utumishi wa umma, labda kama atafanya jambo ambalo siyo la kawaida.”


Wabunge 'Wampa Makavu'
Wabunge wa CCM na upinzani nao walitoa maoni kuhusu hatua hiyo wakisema ilikuwa haki kwa waziri kuachishwa kazi kwani alikuwa ametia aibu Serikali huku wakimpongeza Rais Magufuli kuwa yuko makini.

Mbunge wa Kaliua (CUF), Magdalena Sakaya alisema alichokifanya Magufuli ni kizuri na kwa sababu waziri huyo alishindwa kujiwajibisha mwenyewe.
Sakaya ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), alisema kitendo cha Dk Magufuli kumtimua mtu wake wa karibu, ni ishara tosha kuwa amedhamiria kuwasaidia wanyonge na kuwatahadharisha mawaziri wengine kuwa makini na kazi zao.

“Huyu waziri angeweza kujiwajibisha mwenyewe kutokana na makandokando yake, lakini akachelewa na sasa amekutana na mkono wa Rais kwa kuwa hataki uchafu, ni kweli jana (juzi) Kitwanga alikuwa amelewa wala siyo utani,” alisema Sakaya.

Mbunge wa Sumve, Richard Ndasa (CCM), alimpongeza Rais Magufuli kwa kuona jambo hilo akisema, haiwezekani kufanya kazi na watovu wa nidhamu hasa katika masuala ya ulevi.

Ndasa alisema kulewa ni sehemu ya utovu wa nidhamu lakini inakuwa shida zaidi pale viongozi wenye dhamana wanapolewa tena nyakati za kazi kwani inakuwa ni mfano mbaya, hivyo waziri huyo amevuna alichopanda.

Ali Saleh (Malindi – CUF) alisema Kitwanga alichelewa kuondolewa katika nafasi yake kwani alikuwa ni miongoni mwa majipu.

Alisema waziri huyo alipaswa kuchunguzwa na Ikulu mapema baada ya kuanza kwa kelele za wapinzani, lakini watu wengi walishindwa kumpa Rais habari za ukweli kuhusu waziri wake.

Alisema kutumbuliwa kwa Kitwanga kusitafsiriwe kwa mambo ya ulevi pekee, maana wakuu wa mikoa na wilaya wataanza kufanya hivyo kwa uonevu kwa watu ambao watakuwa wamewanyima hata pombe vilabuni.

Joel Mwaka (Chilonwa – CCM) alimpongeza Rais Magufuli kuwa ni mtu anayeyaishi yale anayoahidi na hivyo kuwapa nafasi kubwa Watanzania na hasa wa chini huku akitahadharisha viongozi kuacha kuwadharau watu wa hali ya chini.

Suzan Kiwanga (Mlimba – Chadema) aliyeanzisha sakata hilo, aliwalaumu wasaidizi wa Kitwanga pamoja na dereva wake kwamba walishindwa kumshauri asiingie bungeni.

“Hakuwa katika hali ya kawaida, alilewa sana jamani hadi akashindwa kujibu swali, ningeshauri Rais aangalie sana kwa mawaziri wake kwani wengi wanaonekana kulewa hata madaraka na kujibu maswali kwa nyodo,” alisema Kiwanga.

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema alisema: “Eti wanadai ametumbuliwa sababu ya ulevi, hebu jiulize Waziri wa Mambo ya Ndani ana wasaidizi, ana mlinzi ana katibu ana dereva, huyu mtu aliyelewa kiasi hicho katibu alishindwa kumwambia maana kazi yao ni kumsaidia waziri asifanye mambo ya aibu. Sasa utawala uliofitinika hauwezi kusimama kamwe kuongoza taifa,” alisema Lema.

Waziri wa Zamani wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha alimpa pole Kitwaga akisema, hata yeye alikuwa anakunywa ndovu akiwa waziri lakini hakuwahi kutimuliwa.

“Namuonea huruma Kitwanga kwa sababu alikuwa haijui CCM, kama ni pombe mbona hata mimi nilikuwa nakunywa ndovu, nakijua chama hicho nilianzia chipukizi, hata umoja wa vijana, lakini niliamua kutoka,” alisema Masha.


Chanzo: Mwananchi

My take;

CHADEMA kwa Masha mmebugi ni moja ya gamba linalochafua taswira yenu kwa kasi.Hakika Gamba hili la Masha litagharimu chama hasa ukizingatia kuelekea uchaguzi ndani ya chadema anakwenda kugombea nafasi muhimu ili kukidhi mkakati wa Lowasa kukihodhi chama.NI BORA ANGENYAMAZA.
 
sasa hao wabunge wa CCM wanaomponda kitwanga mbona walikuwa wanamshangilia wakati akijibu hayo maswali?

Wazee wa ndiyo hutawaweza. Lazima wakubali uwepo wa upinzani umeleta changamoto sana.
Ukiingia kujibu hoja kama huko vizuri lazima utafute mbinu ya kubust akili kama alivyofanya Kitwanga ikamgharimu.
 
Sasa huyo Ndassa naye anaongea nini kheri akanyamaza tu, jamaa ni mlevi huku jimboni maendeleo hakuna hlafu akija kutwa ananunulia raia ndoo za pombe tena za kienyejii kabisa hii ni aibu kabisa.
Mbunge haleti maendeleo... Fanyeni kazi kwa bidii
 
Ilikuwa imeandikwa iwe hivyo, amshukuru Mungu bado yupo hai, angalao mama Kilango amepata kampani kwa hiyo pressure itapungua
 
Hapo ndo naanza kuamini kuwa ccm ni janga. Hao wabunge wote wa sisiem hakuna aliyesikika akimkosoa kitwanga kabla. Baada ya katimuliwa ndo wanaonesha unafiki wao.
 
Umeanza vizuri umeharibu mwishoni.........Chadema na masha kumbe ndivyo vinavyokunyima usingizi...
My take;
Leo wekend nenda kapigwe upepo kando ya bahari au piga kiroba cha valuu akili ikukae sawa!
 
Tatizo lenu mmeuona ulevi mmoja tu kwa kitwanga ila huo ulevi wenu wa madaraka hamuuoni namna unavyoligharimu taifa letu kwan mbunge wa upinzan akiongea point nyie walevi wa madaraka mnashindana kumshambulia personal badala ya kujenga hoja
 
Masha alitoka ccm baada ya kupigwa chini na Ngereja kule Sengerema na si kingine
 
Sunday, May 22, 2016
Wabunge Wampa Makavu Waziri Kitwanga .
Siku moja baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga kutimuliwa nafasi hiyo kwa ulevi, wabunge na wasomi wameendelea kumbana zaidi wakisema hatua hiyo ya Rais imechelewa.
Wapinzani wamekuwa wakimtaka Rais amuondoe kwenye nafasi hiyo kutokana na kuhusishwa na Kampuni ya Infosys ambayo ilitoa ushauri kwa Kampuni ya Lugumi Enterprises iliyopewa zabuni ya kufunga vifaa vya kuchukua alama za vidole (AFIS) katika vituo vya polisi.
Wakati wasomi wakisema hayo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema uamuzi huo ulikuwa sahihi na swali ambalo Kitwanga hakulijibu vizuri kutokana na hali ya ulevi, litapaswa kujibiwa upya baada ya wabunge kuomba mwongozo wa swali hilo.
Majaliwa alisema Rais ametengua uteuzi wa Kitwanga kuanzia juzi baada ya kuonekana amelewa wakati wa kazi.
“Na hili lilibainika pale alipokuwa akijibu maswali ya wizara yake...,”alisema Majaliwa.
Alisema uamuzi wa Rais Magufuli umefuata kanuni za utumishi wa umma ambazo zinakataza mtumishi kulewa akiwa kazini.
Ingawa Majaliwa hakutaja kanuni hiyo, Kifungu cha 34 cha Sheria ya Utumishi wa Umma ya Mwaka 2002 pamoja na Kanuni ya 65 (1) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za Mwaka 2003, kinasema, “Watumishi wa Umma wanapaswa kuepuka tabia ambayo inavunja heshima ya utumishi wao kwa umma hata wanapokuwa nje ya mahali pa kazi."
Tabia inayoweza kuvunja heshima hiyo inatajwa kuwa ni pamoja na matumizi ya dawa za kulevya, ulevi, kukopa kwa kiwango ambacho hawawezi kurejesha na mwenendo mbaya na kujihusisha na vitendo vyovyote viovu mbele ya jamii.
Bunge kuchukua hatua?
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah alipoulizwa adhabu ambazo mbunge anaweza kupata iwapo ataingia bungeni akiwa amelewa, alisema wanaoweza kujibu hilo ni Waziri Mkuu ambaye ni kiongozi wa shughuli za Serikali bungeni na Mnadhimu wa Serikali Bungeni, Jenister Mhagama.
Hata hivyo, Mhagama ambaye ni Waziri Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, alisema hawezi kueleza hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa kuwa tayari Rais ameshachukua uamuzi wa kutengua uteuzi huo.
“Ila Bunge lina taratibu na kanuni zake, nadhani Spika au katibu wa Bunge watakueleza vizuri,” alisema Mhagama.
Spika Job Ndugai hakupatikana kwenye simu, huku Naibu Spika simu yake iliita bila kupokewa.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel alisema: “Kanuni hazijaweka utaratibu wa mbunge anayeingia bungeni amelewa ila kuhusu suala la Kitwanga ni la nidhamu ya utumishi wa umma, labda kama atafanya jambo ambalo siyo la kawaida.”

Wabunge 'Wampa Makavu'
Wabunge wa CCM na upinzani nao walitoa maoni kuhusu hatua hiyo wakisema ilikuwa haki kwa waziri kuachishwa kazi kwani alikuwa ametia aibu Serikali huku wakimpongeza Rais Magufuli kuwa yuko makini.

Mbunge wa Kaliua (CUF), Magdalena Sakaya alisema alichokifanya Magufuli ni kizuri na kwa sababu waziri huyo alishindwa kujiwajibisha mwenyewe.
Sakaya ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), alisema kitendo cha Dk Magufuli kumtimua mtu wake wa karibu, ni ishara tosha kuwa amedhamiria kuwasaidia wanyonge na kuwatahadharisha mawaziri wengine kuwa makini na kazi zao.
“Huyu waziri angeweza kujiwajibisha mwenyewe kutokana na makandokando yake, lakini akachelewa na sasa amekutana na mkono wa Rais kwa kuwa hataki uchafu, ni kweli jana (juzi) Kitwanga alikuwa amelewa wala siyo utani,” alisema Sakaya.
Mbunge wa Sumve, Richard Ndasa (CCM), alimpongeza Rais Magufuli kwa kuona jambo hilo akisema, haiwezekani kufanya kazi na watovu wa nidhamu hasa katika masuala ya ulevi.
Ndasa alisema kulewa ni sehemu ya utovu wa nidhamu lakini inakuwa shida zaidi pale viongozi wenye dhamana wanapolewa tena nyakati za kazi kwani inakuwa ni mfano mbaya, hivyo waziri huyo amevuna alichopanda.
Ali Saleh (Malindi – CUF) alisema Kitwanga alichelewa kuondolewa katika nafasi yake kwani alikuwa ni miongoni mwa majipu.

Alisema waziri huyo alipaswa kuchunguzwa na Ikulu mapema baada ya kuanza kwa kelele za wapinzani, lakini watu wengi walishindwa kumpa Rais habari za ukweli kuhusu waziri wake.

Alisema kutumbuliwa kwa Kitwanga kusitafsiriwe kwa mambo ya ulevi pekee, maana wakuu wa mikoa na wilaya wataanza kufanya hivyo kwa uonevu kwa watu ambao watakuwa wamewanyima hata pombe vilabuni.
Joel Mwaka (Chilonwa – CCM) alimpongeza Rais Magufuli kuwa ni mtu anayeyaishi yale anayoahidi na hivyo kuwapa nafasi kubwa Watanzania na hasa wa chini huku akitahadharisha viongozi kuacha kuwadharau watu wa hali ya chini.
Suzan Kiwanga (Mlimba – Chadema) aliyeanzisha sakata hilo, aliwalaumu wasaidizi wa Kitwanga pamoja na dereva wake kwamba walishindwa kumshauri asiingie bungeni.
“Hakuwa katika hali ya kawaida, alilewa sana jamani hadi akashindwa kujibu swali, ningeshauri Rais aangalie sana kwa mawaziri wake kwani wengi wanaonekana kulewa hata madaraka na kujibu maswali kwa nyodo,” alisema Kiwanga.

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema alisema: “Eti wanadai ametumbuliwa sababu ya ulevi, hebu jiulize Waziri wa Mambo ya Ndani ana wasaidizi, ana mlinzi ana katibu ana dereva, huyu mtu aliyelewa kiasi hicho katibu alishindwa kumwambia maana kazi yao ni kumsaidia waziri asifanye mambo ya aibu. Sasa utawala uliofitinika hauwezi kusimama kamwe kuongoza taifa,” alisema Lema.
Waziri wa Zamani wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha alimpa pole Kitwaga akisema, hata yeye alikuwa anakunywa ndovu akiwa waziri lakini hakuwahi kutimuliwa.
“Namuonea huruma Kitwanga kwa sababu alikuwa haijui CCM, kama ni pombe mbona hata mimi nilikuwa nakunywa ndovu, nakijua chama hicho nilianzia chipukizi, hata umoja wa vijana, lakini niliamua kutoka,” alisema Masha.

My take;
CHADEMA kwa Masha mmebugi ni moja ya gamba linalochafua taswira yenu kwa kasi.Hakika Gamba hili la Masha litagharimu chama hasa ukizingatia kuelekea uchaguzi ndani ya chadema anakwenda kugombea nafasi muhimu ili kukidhi mkakati wa Lowasa kukihodhi chama.NI BORA ANGENYAMAZA.
Yn hyo nyumbu ataharibu hyo saccos hawatakuja sahau!!
 
Yani wewe bwegge katika habari hii yote umemuona Masha tu? Jinga kabisa.
Hizi heading mara nyingi Mods huwa wanazibadilisha tofauti na mleta mada alivyokusudia, hivyo ni vigumu kumhukumu mleta mada kuanzia kwenye heading. Ni maudhi sana, hata mimi threads zangu kadhaa mods wali edit heading zangu.
 
Sasa huyo Ndassa naye anaongea nini kheri akanyamaza tu, jamaa ni mlevi huku jimboni maendeleo hakuna hlafu akija kutwa ananunulia raia ndoo za pombe tena za kienyejii kabisa hii ni aibu kabisa.
Kweli Ndasa angepiga kimya tu, sababu yeye mwenyewe ni balaa, kwa vile tu hakuna kipimo cha pombe bungeni, ungekuta nae yumo.
 
Mnafiki tu!!;anahamahama tu majimbo!;alianzia nyamagana nako walipiga chini!!;atahama sn vyama!!
Kumbe wanafki wapo wengi, waliomahama majimbo wapo Jakaya Kikwete, Hussein Mwinyi, Peter Serukamba, Zitto Kabwe, James Mbatia, Augustine Mrema, Hamis Kingwangallah kwa uchache, labda utueleze kuhama chama ni uhaini?
Mnafiki tu!!;anahamahama tu majimbo!;alianzia nyamagana nako walipiga chini!!;atahama sn vyama!!
Kumbe wanafki wapo wengi, waliomahama majimbo wapo Jakaya Kikwete, Hussein Mwinyi, Peter Serukamba, Zitto Kabwe, James Mbatia, Augustine Mrema, Hamis Kingwangallah kwa uchache, labda utueleze kuhama chama ni uhaini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom