Wanajamii,
Kuna wakati wabunge wa CCM huwa wananipa wakati mgumu kweli kuwaelewa. Utamkuta mbunge wa CCM anasimama bungeni na kuongea kana kwamba yeye ni mjumbe wa baraza la mawaziri. Sasa mimi huniacha hoi na kubaki kujiuliza hivi hawa wabunge wa CCM hawajui kazi na wajibu wa mbunge anapokuwa bungeni? Hivi wao hawajui kwamba pamoja na majukumu mengine, majukumu ya mbunge ni kuisimamia,kuishauri,kuikosoa na kuiwajibisha serikali? Ni kweli katika mabunge ya kunakuwa na kambi mbili. Kambi ya upinzani na kambi ya chama tawala. Lakini kuwa kambi ya chama tawala hakumuondoshei mbunge wajibu wake mkuu wa kisheria. Inafika mahali katika bunge letu haujui Waziri ni nani na mbunge ni nani Wote wamegeuka wasemaji wa serikali. Sasa katika hali kama hiyo bunge linamaana linamaana gani? Yanini kupoteza pesa za wavuja jasho masikini wa nchi hii?
Kuna wakati wabunge wa CCM huwa wananipa wakati mgumu kweli kuwaelewa. Utamkuta mbunge wa CCM anasimama bungeni na kuongea kana kwamba yeye ni mjumbe wa baraza la mawaziri. Sasa mimi huniacha hoi na kubaki kujiuliza hivi hawa wabunge wa CCM hawajui kazi na wajibu wa mbunge anapokuwa bungeni? Hivi wao hawajui kwamba pamoja na majukumu mengine, majukumu ya mbunge ni kuisimamia,kuishauri,kuikosoa na kuiwajibisha serikali? Ni kweli katika mabunge ya kunakuwa na kambi mbili. Kambi ya upinzani na kambi ya chama tawala. Lakini kuwa kambi ya chama tawala hakumuondoshei mbunge wajibu wake mkuu wa kisheria. Inafika mahali katika bunge letu haujui Waziri ni nani na mbunge ni nani Wote wamegeuka wasemaji wa serikali. Sasa katika hali kama hiyo bunge linamaana linamaana gani? Yanini kupoteza pesa za wavuja jasho masikini wa nchi hii?