Wabongo tunapenda sana kusalimiana kinafki

Wabongo tunapenda sana kusalimiana kinafki

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
23,716
Reaction score
57,243
Natambua kuwa Ni adabu njema unapowakuta watu kuwasalamia na Kisha Mambo mengine kuendelea.lakini kinachonikera ni Aina ya hizi salamu.kwa mfano mtu unakutana naye unamwambia Mambo vipi?yeye anakujibu POA.ni shwari? Anajibu fresh..lakini unakuta huyo mtu ana umwa au ana matatizo mengi TU Ila hawezi kukwambia kwamba sio poa.ni Kama tumekariri TU hizi Salamu tunafanya kwa mazoea

Me ninachoona tuwe tukikutana tunaanza TU Kuongea Jambo fulani kuliko kuanza kusalimiana masalamu marefu ambayo yapo Kama kuchorana TU kinafki.masalamu haya ndo yanafanya tuwe slow sana kwenye communication na kufikiri,we ukikutana na Mimi ongea TU shida Yako tuone tunafanyaje tukianza masalamu Mambo yatakuwa mengi na Mimi Sasa hivi Niko na haraka.
 
Natambua kuwa Ni adabu njema unapowakuta watu kuwasalamia na Kisha Mambo mengine kuendelea.lakini kinachonikera ni Aina ya hizi salamu.kwa mfano mtu unakutana naye unamwambia Mambo vipi?yeye anakujibu POA.ni shwari? Anajibu fresh..lakini unakuta huyo mtu ana umwa au ana matatizo mengi TU Ila hawezi kukwambia kwamba sio poa.ni Kama tumekariri TU hizi Salamu tunafanya kwa mazoea
Me ninachoona tuwe tukikutana tunaanza TU Kuongea Jambo fulani kuliko kuanza kusalimiana masalamu marefu ambayo yapo Kama kuchorana TU kinafki.masalamu haya ndo yanafanya tuwe slow sana kwenye communication na kufikiri,we ukikutana na Mimi ongea TU shida Yako tuone tunafanyaje tukianza masalamu Mambo yatakuwa mengi na Mimi Sasa hivi Niko na haraka.
Bado asubuhi sana Mkuu
Pumzika kwanza,kisha andika tena kwa umakini



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tukisema tuwaambie wote tunaosalimiana nao hali zetu kiuhalisia,.tutawaambia wangapi??siku nzima si utakuwa na kazi ya kujidadavua tuu...

Halafu wabongo ni wanafiki kama ulivyosema,.hata ukimuambia hivyo ndio atafanya nini zaidi ya kukupa pole tuu,.na pengine ukiondoka akuseme "yule nae,kila siku anaumwa yeye si afe tuu kama kachoka kuishi"😂lol
 
Huo ni Utamaduni wa Maeneo mengi sio Bongo tu

Ughaibuni unaingia kwa Daktari you hoi umechakaa kwa maradhi na Daktar anakusalimia ‘How are you’ unamjibu I’m fine
 
Nina hakika
Neno UNAFIKI hatulijua,na kama tulijua maana yake,Basi tutakuwa tunajua kwa maana finyu

Kupeana Salamu,si unafiki,wala haimaanishi ukiulizwa hali yako,Basi utaje shida zako zote
Sio maana yake
Mtoa salamu na Mpokeaji,wote wana shida,ila shida hazilingani,ila ndani ya shida walizonazo,kuna unafuu upo ndani yao
Unapokuwa na UHAI
Unapokuwa na akili timamu
Hizi zote ni alama njema

Wakuu
Tuwe na nia njema na dhana nzuri
Lawama hazijengi
Na neno zuri lenye matarajio,ni dawa mbele ya mgonjwa,hata kama pumzi zakw zinahesabika kwa vidole

Shukran

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wataalamu wa lugha wanasema mojawapo ya kazi ya lugha ni kuanzisha na kuendeleza mahusiano mazuri ya watu (PHATIC FUNCTION) Kupitia mambo mbalimbali kama vile SALAMU (kutoa ama kuitikia) na unaposalimiwa lazima uitike positively hata kama una matatizo ili kuepuka kumkwaza au kumchelewesha mtoa salamu.ukijibu negatively unaibua hisia mbaya.lakini pia atalazimika akuulize kwanini umejibu /habari ni mbaya/ hivyo kumfanya aanze kusikiliza matatizo yako kitu ambacho wengi hawakipendi.ndiyo maana tukisalimiwa tunajibu-poa, safi, bomba, fresh, njema, nzuri n.k hata kama hatujibu kwa uhalisia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom