tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA MKOA WA KATAVI VYASHIRIKI MAZOEZI YA PAMOJA
Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama Oktoba 3, 20205 wamefanya mazoezi ya matembezi (Route Match) kwa kutembea zaidi ya kilomita 10 kuzunguka maeneo mbalimbali Manispaa ya Mpanda.
Mazoezi hayo yamejumuisha Jeshi la Polisi, Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jeshi la Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Idara ya Uhamiaji na Idara ya Usalama.
Soma pia: Golugwa: Vyombo vya ulinzi na usalama visiwashambulie raia
Lengo la matembezi hayo ni kuimarisha mshikamano baina ya vyombo vya ulinzi na usalama, kujenga afya ya mwili na akili na kuendelea kujiweka tayari katika kulinda amani na usalama wa raia na mali zao.
Akizungumza baada ya mazoezi hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Kaster Ngonyani amewapongeza washiriki wote na kuhimiza kuendeleza mshikamano katika kuhakikisha ulinzi na usalama unaendelea kuimarika.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama Oktoba 3, 20205 wamefanya mazoezi ya matembezi (Route Match) kwa kutembea zaidi ya kilomita 10 kuzunguka maeneo mbalimbali Manispaa ya Mpanda.
Mazoezi hayo yamejumuisha Jeshi la Polisi, Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jeshi la Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Idara ya Uhamiaji na Idara ya Usalama.
Soma pia: Golugwa: Vyombo vya ulinzi na usalama visiwashambulie raia
Lengo la matembezi hayo ni kuimarisha mshikamano baina ya vyombo vya ulinzi na usalama, kujenga afya ya mwili na akili na kuendelea kujiweka tayari katika kulinda amani na usalama wa raia na mali zao.
Akizungumza baada ya mazoezi hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Kaster Ngonyani amewapongeza washiriki wote na kuhimiza kuendeleza mshikamano katika kuhakikisha ulinzi na usalama unaendelea kuimarika.