Najua wengi wenu mtahisi au mtaniona kama mropokaji lkn kamwe damu ya kitanzania na kamwe haitakuwa ya tanganyika wala ya kizanzibari. kwangu hupatwa na mfadhaiko nikimsikia mtu anajitambulisha yy ni mzanzibari au yy ni mtanganyika. uchezeeni muungano leo lkn kesho mutajuta. tunachotakiwa ni kuurekebisha mfumo wa muungano wa si kutengana haswa ktk wakati huu ambao tuhitaji kuujenga uchumi wetu. lkn mkiamua kamwe sitokuwa mtanganyika wala mzanzibari.
Nikujibu ndugu,
Hakuna mtanzania yeyote anapenda kuona muungano uvunjike lakini muundo wa muungano uliopo hauvumiliki kwa watanganyika na wazanzibar. Linalotakiwa ni kuwauliza watanzania ni aina gani ya muungano wanapenda au wanapendelea. Jibu la wengi ni kuwa na serikali tatu ingawa mwalimu Nyerere alitahadhalisha gharama ya kuendesha serikali tatu hatuwezi na mzigo mkubwa utaiangukia Tanganyika, kuwa na serikali moja kamwe visiwani hawatokubali. Kama itatokea tusielewane ni heri tuachane salama kila upande uwe na serikali yake ili tujenge nchi zetu. Tanganyika waijenge tanganyika yao na wazanzibari waijenge zanzibar yao. Tutashirikiana kiuchumi, kijamii na kisiasa. Iwapo hili likitokea, basi utanzania umeisha na hakutokuwa na taifa la Tanzania. Sasa basi, kama hutakiwi kuwa mtanganyika au mzanzibari basi jiandae kuwa raia wa nchi nyingine tofauti na hizo mbili tajwa hapo juu. Sijui utasafiria passport gani, utakuwa na kitambulisho gani, nadhani unayasema haya kwa kuwa hayajatokea, ikitokea huna pa kwenda ndugu yangu. Tusingependa kuona hayo yote yakitokea kwa kuwa na mimi mwenyewe naupenda muungano wetu. Serikali 2 ni mzigo kwa raia wote, tujadili la serikali 3 au moja.
Jiongelee mwenyewe, we mgeni hapa? Ulifanya poling ukapata 100% ya Watanzania wanataka Muungano?Hakuna mtanzania yeyote anapenda kuona muungano uvunjike
Hatuwezi kujuta, muungano sio lazima, viinchi vingapi vidogo kama karanga vina nguvu kuliko Tanzania na li muungano lake?
Swaziland, Lesotho, Botswana, wameungana na nani?
Hatujaenda Ulaya, viinchi kama Belgium, Luxembourg, Uswizi wameungana na nani?
Kill the Muungano!
Najua wengi wenu mtahisi au mtaniona kama mropokaji lkn kamwe damu ya kitanzania na kamwe haitakuwa ya tanganyika wala ya kizanzibari. kwangu hupatwa na mfadhaiko nikimsikia mtu anajitambulisha yy ni mzanzibari au yy ni mtanganyika. uchezeeni muungano leo lkn kesho mutajuta. tunachotakiwa ni kuurekebisha mfumo wa muungano wa si kutengana haswa ktk wakati huu ambao tuhitaji kuujenga uchumi wetu. lkn mkiamua kamwe sitokuwa mtanganyika wala mzanzibari.
Najua wengi wenu mtahisi au mtaniona kama mropokaji lkn kamwe damu ya kitanzania na kamwe haitakuwa ya tanganyika wala ya kizanzibari. kwangu hupatwa na mfadhaiko nikimsikia mtu anajitambulisha yy ni mzanzibari au yy ni mtanganyika. uchezeeni muungano leo lkn kesho mutajuta. tunachotakiwa ni kuurekebisha mfumo wa muungano wa si kutengana haswa ktk wakati huu ambao tuhitaji kuujenga uchumi wetu. lkn mkiamua kamwe sitokuwa mtanganyika wala mzanzibari.
nakuunga mkono mkuu,
hata mimi nitabaki mtanzania daima.
Tanganyika siijui,
sikuzaliwa Tanganyika,
wakoloni ndio wanaoijua Tanganyika,
hii Tanganyika ilikuwa shamba la bibi kwa wakoloni,
ha wao wanjua kuwa hawatathubutu kuigeuza Tanzania koloni lao, haiwezekani
Tanzania ni huru na haijawahi kutawaliwa
Tanganyika na Zanzibar yote ni makoloni na hayajawahi kuwa huru
muungano ndio uliokamilisha uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
Tanzania ni jina la kizalendo
tena linaakisi uhuru na azma ya kujitawala
tanganyika inaakisi utumwa, ukoloni, na unyonyaji
siipendi Tanganyika,
siipendi Zanzibar
napenda Tanzania
daima nitaililia Tanzania
Mungu ibariki Tanzania!!!
nakuunga mkono mkuu,
hata mimi nitabaki mtanzania daima.
Tanganyika siijui,
sikuzaliwa Tanganyika,
wakoloni ndio wanaoijua Tanganyika,
hii Tanganyika ilikuwa shamba la bibi kwa wakoloni,
ha wao wanjua kuwa hawatathubutu kuigeuza Tanzania koloni lao, haiwezekani
Tanzania ni huru na haijawahi kutawaliwa
Tanganyika na Zanzibar yote ni makoloni na hayajawahi kuwa huru
muungano ndio uliokamilisha uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
Tanzania ni jina la kizalendo
tena linaakisi uhuru na azma ya kujitawala
tanganyika inaakisi utumwa, ukoloni, na unyonyaji
siipendi Tanganyika,
siipendi Zanzibar
napenda Tanzania
daima nitaililia Tanzania
Mungu ibariki Tanzania!!!
Mnaotaka muungano uvunjwe mbona hamsemi hizo hasara mnazozipta kwa uwepo wa muungano. Tunataka ushahidi uletwe jamvini.
Ndugu yangu hatuwezi kuwa na mfumo ule ule wa maisha milele. Usipoamini katika mabadiliko hutakaa ufanikiwe.
Watanzania wengi hatukuamini mfumo wa vyama vingi tukidhani kuwa tutapigana vita vya wenyewe kwa wenyewe lakini baada ya kulazimishwa kuyakubali mabadiliko leo tunafurahia. Kama tungeachwa na mfumo wa chama kimoja unadhani tungekuwa hivi tulivyo leo?
Tanganyika ilishakuwapo bila shida hata baada ya uhuru, Zanzibar imeendelea kuwepo kama zanzibar bila tatizo.
Lazima tukubali mabadiliko. kama vile ambavyo binadamu tunabadilika.
Kitu chochote kisicho faida basi ni hasara. Kama watu hawaoni faida ya Muungano basi huo Muungano ni hasara by default
Labda mnaojua faida za Muungano ziwekeni hapa tuzichambue.
Mtuambie bila Muungano tulioporwa utaifa wa tanganyika tunapoteza nini. Na kwa huu muungano tuliokuwa watanganyika tunapata nini?
wakati wa shida walipenda muungano, sasa wamevimbiwa hewa inawatoka ovyo wanataka nafasi.... labda hewa inanuka sana yakhe!!!
wapende wasipende wataendelea kuitegemea Tanganyika kwa kila kitu, jeuri yao mafirauni wa kiarabu? kwani Somalia, yemen inayopakana na Saudia au Uganda, wote hawa wako kwenye jumuiya ya nchi za kiislam na kiarab ligi, je wana nini kuliko sisi? sema jawako sawa kimentali hao jamaa zetu wazenji, sema kwa mademu si haba alhamdulillahi, japo mademu wenye mara wanagoma kutoa mpaka uzunguuke mlango wa uwani...
Hivii, naweza kuruhusiwa kugombea uwakilishi au ubunge huko Zenji bila kikwazo?naombeni wale wote ambao wanasema muungano uvunjike wataje hasara mbili 2. mimi nimeshataja faida ninazoziona
1: elimu - wazanzibari wanfaidaka ktk elimu ya juu wakija kusoma tanganyika wankopeshwa sawa na wanalip[a ada sawa kama watanganyika na watanganyika wakienda zanzibar hivyohivyo wanapata fursa hiyo.
2; kuna free trade btn zanzibar na tanganyika. mzanzibar hapati aina yyte ya kikwazo akitaka kufanya biashara tanganyika kwa sababu ya uzanzibar wake na mtanganyika hivyohivyo hapati vikwazo akitaka kufanya biashara zanzibar.
sasa nyinyi munaouona hauna faida tajeni hasara mbili mnazozipta kwa ajili ya huu muungano wetu.
MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU UBARIKI MUUNGANO WETU.