Yaan mmi nimelia nao sana kwanza ile 100 huduma kwa wateja haipo huwez kuwapata, pili waongo sana wanaenda kwenye ukurasa wa Rais samia wanajiandikisha vitu et tumeboresha zaid mm kila nilipokua nikijaribu sion kitu week kama moja na nusu jana nimeamua rasim kuhama voda na kwenda zantel, jamani hamia zantel raha tupu. J.b na m.b za kufa mtu dakika kibao mitandao yote voda bayee nitachukua line niweke simu ndogo kwa ajiri ya m.pesa baaas.
Hahahah hiki kifurushi changu nilichojifichamo baada ya yule mkurugenzi mwehu kuleta wehu ofisini! Atakuwa anajutia bangi aliyovuta siku ile 😝😝😝 kabla hajatoa maagizo ya GB moja kuuzwa elfu 3
Mkitaka kupata ofa kabambe nunueni sim card mpya. Sasa wewe mteja wa Voda toka mwaka 2003 wakuvutie kwa lipi wakati wanauhakika wewe ni mteja wao? Mleta mada anasema ukweli ila hiyo ofa sio kwa nyie wateja loyal kwa voda.