Vodacom kuna tatizo

Tanzania Mpya

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2012
Posts
252
Reaction score
145
Toka usiku hakuna mtandao, nikafikiri ni simu yangu tu. Lakini asubuhi nikacheki na simu ya wife nayo pia haina mtandao. Kuna tatizo gani huu mtandao wa Vodacom? Je wenzetu hapa Dar mnapata mtandao?
 
Ni kweli hakuna mtandao wa Vodacom. Wiki iliyopita pia ilikuwa hivyo pesa zetu za kununua Luku zimeliwa hatukupata token na ukiwapigia ni ubabaishaji tu.
 
watoke hadharani watuambie....
 
Kuna tatizo gani? Biashara za kiswahili bwana!
 
Toka usiku hakuna mtandao, nikafikiri ni simu yangu tu. Lakini asubuhi nikacheki na simu ya wife nayo pia haina mtandao. Kuna tatizo gani huu mtandao wa Vodacom? Je wenzetu hapa Dar mnapata mtandao?

Homa yao inafanana na Tgo unaweza pigia mtu simu uka ambiwa haipatikani ihali ipo online..... Used technology.......
 
Mbano mm natumia mtandao wa Voda? Jana siku nzima mpaka saa sita usiku nimetumia na asubuhi hii naendelea nao.Wametaka wenyewe wakanipa siku saba free internet.Nakomaa nao mpaka waombe poo.Full download mpaka tablet imepata moto.
 
Mbano mm natumia mtandao wa Voda? Jana siku nzima mpaka saa sita usiku nimetumia na asubuhi hii naendelea nao.Wametaka wenyewe wakanipa siku saba free internet.Nakomaa nao mpaka waombe poo.Full download mpaka tablet imepata moto.

Upo Dar mh?
 
hakuna network kabisa, mimi nilidhani chip yangu imeharibika.
 
pcman unaulizwa,uko dar,maana mlalamikaji amesema yuko dar.
 
Last edited by a moderator:
Sio dar tu, mpaka huku dodoma. Juzi walinitumia msg ya kunipa ofa ya internet bure kwa siku 7, nlipotumia net wakakata pesa yote, jana wakanitumia sms ya kuomba radhi na kusema pesa itarudishwa, mpaka sasa sijaona hata senti.
 
Inategemea uko dar sehem gn. Mi npo dar na napata full network. Yawezekana pia mnara wa karibu yako una matatizo. Pole
 
Mimi 3G Yao siipati mwezi sasa Edge ndo inapatikana balaa hili
 
Tunarekebisha baadhi ya switch zetu.

Tunaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza.

Vodacom. Power to you.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Semen basi sio w2 tunamichöngo yetu af mnatukwamisha.
 
Sumu, marekebisho mfanye nyie halafu gharama tulipe sisi? Sasa hzo fedha zetu zilizopitea sababu ya hayo marekebisho yenu tunazipataje?
Sio mbaya, boresheni, kwa muda huu tunahamia bundle za mitandao mingine, maana mnatuingiza hasara tunaofanya biashara kwa net
 
Toka usiku hakuna mtandao, nikafikiri ni simu yangu tu. Lakini asubuhi nikacheki na simu ya wife nayo pia haina mtandao. Kuna tatizo gani huu mtandao wa Vodacom? Je wenzetu hapa Dar mnapata mtandao?
Mkuu siyo jana tu, VODACOM wana tatizo almost wiki mbili au zaidi.
Mimi sijawahi kubadili namaba ya simu yangu for almost 10 yrs na sasa naona madudu
  • ukipiga simu hai-connect
  • ukipiga simu unasikia sauti yako mwenyewe-its crazy!!!
  • simu ikisha connect in jam na kukata mawasiliano
  • wakati mwingine kuna muungurumo kwenye mawasiliano
  • ukikata simu haikatiki na inaendelea kukata senti
Naamini TCRA wata fuatilia tatizo hili maana baada tu ya kupunguza gharama za connection kati ya makampuni ya simu ndiyo haya matatizo yamekithiri.
 
Mimi 3G Yao siipati mwezi sasa Edge ndo inapatikana balaa hili

Exactly!! I'm facing the same problem here.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Tunarekebisha baadhi ya switch zetu.

Tunaomba radhi kwa usumbufu unaojitokeza.

Vodacom. Power to you.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

... Kazi ni kwako...
 
Niliipenda voda ila airtell walinipenda zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…