Amini nawaambieni! "Mke mwema ni hospitali ya rufaa ya mumewe." Kule kwingine ni "zahanati na vituo vya afya". Nimesema 'mke mwema, tuelewane hapo.
Kwa asili mwanaume ni mgonjwa, anaumwa ugonjwa wa "upweke." Rejea kitabu cha Mwanzo 2:18. Uzoefu unaonesha kuwa wanaume wengi, waliokimbia hospitali zao za rufaa na kwenda "zahanati/vituo vya afya", walipotetereka kiuchumi au kupata matatizo ya kudumu kiafya, waliandikiwa kurudi rufaa kwa
matibu zaidi.
Ukibahatika kupata "hospitali bora ya rufaa" (mke mwema) usitoroke. "Zahanati/vituo vya afya" havina vifaa tiba vya kutosha, hivyo hawawezi kukaa na wewe hali ikiwa tete.