Vituko mitandaoni. Tupia chako

#HABARI Walinzi wa Pwani ya Marekani wamesema sehemu ya mabaki ya chombo cha chini ya maji cha OceanGate kilichopoteza mawasiliano saa 1:45 tangu kuanza kwa safari yake ya kuzama baharini Jumapili imegunduliwa ndani ya eneo la utafutaji na roboti ya ROV karibu na mabaki ya Meli ya Titanic.

Katika safari hiyo masalia ya Meli Titanic huonekana kwa kwenda umbali wa mita 3,800 chini ya bahari na chombo hicho kina uwezo wa kwenda mita 4,000 chini ya Bahari.

Chombo hicho kilikuwa na watu watano waliokuwa wakienda kutalii mabaki ya Meli ya Titanic, akiwemo Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya OceanGate inayohusika na safari hiyo Stockton Rush.

#EastAfricaTV

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…