Kenya imekanusha ahadi za zabuni ya Julai iliyotolewa kwa Dubai Port (DP) World ambayo ingeruhusu kampuni hiyo yenye makao yake makuu katika UAE kutoa zabuni ya maendeleo, uendeshaji na usimamizi wa bandari nne za nchi hiyo.
DP World ilisema serikali ya Kenya iliahidi kutoa ombi la pendekezo la kibiashara la mikataba ya bandari kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9.
Kenya ilikuwa imekubali kutoa upendeleo kwa DP World, inayomilikiwa na serikali ya Dubai na mojawapo ya waendeshaji wakubwa wa bandari duniani, katika makubaliano yaliyotiwa wino kati ya Mataifa hayo mawili.
Hazina imekanusha kuwepo kwa mpango huo na kukanusha kuwahi kutaja mipango ya kutoa zabuni ifikapo Julai.
Mkataba unazinyima pande mbili mamlaka na haki ya kusitisha Mkataba, Serikali husika katika Mkataba hazitakuwa na haki ya kuvunja Mkataba (denounce), kujitoa (withdraw from), kuahirisha (suspend) au kusitisha (terminate) Mkataba katika mazingira yoyote yale. .