FUTA KIOO TU
Kuna wakati haina maana kupoteza nguvu zako kufuta bodi ,we hangaika na kioo tu.
Acha tope la kwenye body likukumbushe mapambano, lakini ukiliacha kwnye kioo UTAPOTEZA PAMBANO
Yesss....namaanisha hivi....
Usiruhusu mapambano ya maisha, masimango, dharau, wivu na chuki zikuzibe ufahamu wako...zikutie unyonge..zikunyime kujiamini...usikubali.
Acha wazione kwenye mdomo yao lakini wewe usizione kwenye ndoto zako.
Kwanini unatumia muda mwingi kutaka uoshe gari lote ndo uendelee na safari wakati unahitaji pakuonea bara bara tu? Hangaika na kioo tu best, utaosha lote ukifika.
Pangusa kioo, Pasua tope.