Vijana wanasubiri bahati katika maisha

Vijana wanasubiri bahati katika maisha

Joined
Aug 17, 2016
Posts
69
Reaction score
46
KWANINI MAISHA YAKO YAWE YA BAHATI NASIBU?

Ni meangalia jamii yangu inayo nizunguka hasa kwa vijana bado kuna vimbi kubwa sana la watu wanaishi basi na kujua nn kusudi hasa la kuishi na wala hawana habari na kuyajua hayo wanaishi maisha ya udhalilishaji pasi na kujua wamekua chini zaidi ya wanyama wa mwituni kwa kifupi yaani unaweza sema kuwa wanaishi kwa bahati nasibu kwasababu gani ninasema wanaishi kwa bahati nasibu.

Kwasababu hawajui kwanini wanaishi wao wanao na kula, kunywa na kulala kukaa kupiga zoga basi inatosha unakuta mtu haya ndio maisha yake siku zinakatika miezi inaenda na miaka inakwisha hana bidii yeyote anayo onesha juu ya maisha yake ya usoni.

Na anayafanya haya kwa kukosa au kutojiwekea kipao mbele katika maisha yake hala lengo wala ramani ya maisha yake ya baada ye kwama hauna ramani yeyote ndugu yangu safari yako ya maisha itakuwa ngumu sana kuishi kwa kubahatisha sio zana ya kutosha katika safari kubwa ya maisha yako kama utaridhika kuishi bila muongozo utakuwa hauna tofauti na mnyama au wewe utakuwa ni zaidi hata ya mnyama porini kwasababu hata mnyama pia anaramani katika mawindo yake.

Uvivu hili ni janga sugu kwa vijana vijana wengi hawataki kabisa kujibiidisha hawataki kujisumbua kabisa wajiona wazito kuyaendea mambo ya maana yatayo wapa uhuru wa maisha yao lakini hawaoni uvivu kukaa kwenye Tv kufuatilia tamthila za kihindi za kichina tena anapanga mpaka ratiba kabisa ili zisimpite mtu yopo tayari kukaa masikani kuongela maisha ya watu au kuzungumia maisha ya watu maarufu dunia si vibaya kuangalia maisha ya watu maarufu waliofanikiwa kwa kujifunza mapito yao lakini hawa wanaangalia kwa kujifurahisha tu na wala hawajifunzi chochote kile.

Ngojea nikuambie ndugu yangu mimi nimfuatiliaji mzuri sana tena sana maisha ya viumbe vya Mungu waliofanikiwa lakini nimegundua hawa kufanikiwa kwa kukaa masaa matano kufuatilia tamthilia hawakuwa wavivu hawakuwa watu wakushinda maskani kutwa na hata kama wapo ambao wamefanikiwa bila kujituma na bidii basi ni wachache sana hata ukiamua kuhesabu hauwezi kumaliza vidole vya mkono wako mmoja lakini nimeona wingi wa waliofanikiwa ni wale walio amuakupigana na jinamizi hili la uvivu na wakalishinda kwa kufanya kazi na bidii walifanya kazi kwa mfululizo na kwa jitihada bila kupumzika.

Hii kwangu inanifundisha kuwa maisha yanakuwa ya mafanikio yanakuwap amoja na yule mwenye bidii, ujasiri na nia ya kutenda mambo kuliko walio ngojea bahati nasibu ziwa shukukie, wewe endelea kusubiri biko ikupe maisha au tatu mzuka kwa kukaa masikani na kwenye magenge ya porojo halafu usimame ujifananishe ya yule ambaye yupo juani na anatokwa na jacho kama mvua kwa ajli ya kupigania mustakabali mzima wa maisha yake familia na jamii yake

Kutoka RAMADHANI IBN KIMWERI

Inaendelea...
 
Mm Naona Vijana wa siku hizi ....wamefanikiwa sana kiasi kikubwa.......wanamiliki Nyumba hapa mjini Pamoja na Magari....pia weekend awakosi kuchoma nyama ...kila weekend......kwaiyo Jua mnazingua nyie mnaokaa kuwabeza vijana
 
Kuna kaukweli maana mtaa ninaokaa kuna majumba manner yote ya kubeti kumejaa vijana Na screen kubwa ukutani. Ukisema uvivu nakataa vijana wengi kama anapata sehemu ya kujikimu hawezi chezea hasa wa kileo ila wanaamka hawajui waende wapi hivyo wanakua tegemezi
 
Vijana ni wengi ila michongo ni michache.
Amini kunapokuwa na njia, hakuwezi kukosa wapitaji.

Vijana wengi waliomaliza masomo yao wanakosa tu michongo. Lakini walio wengi wanahitaji kuoneshwa njia. Wachache wanazitafuta wenyewe.
Hivyo usiwalaumu sana.

Kuna dogo kapiga bingo la 16m,
Leo hii kasimika duka lake. Akiamka asubuhi anaenda kufungua duka lake. Lakini ungemuona siku zilizopita ungemcheka kwa kuwa hana kazi.

Ajira hakuna, zilizopo ni za kujuana tu. Unaposema wakalime bila mtaji ni shiida sana.

Sitetei uvivu ila naongea haya kwa kuwa nilipitia msoto huu baada ya kumaliza chuo. Na watu inafikia hatua wanakuona mpuuzi japo unakuwa na elimu yako.
 
Vijana ni wengi ila michongo ni michache.
Amini kunapokuwa na njia, hakuwezi kukosa wapitaji.

Vijana wengi waliomaliza masomo yao wanakosa tu michongo. Lakini walio wengi wanahitaji kuoneshwa njia. Wachache wanazitafuta wenyewe.
Hivyo usiwalaumu sana.

Kuna dogo kapiga bingo la 16m,
Leo hii kasimika duka lake. Akiamka asubuhi anaenda kufungua duka lake. Lakini ungemuona siku zilizopita ungemcheka kwa kuwa hana kazi.

Ajira hakuna, zilizopo ni za kujuana tu. Unaposema wakalime bila mtaji ni shiida sana.

Sitetei uvivu ila naongea haya kwa kuwa nilipitia msoto huu baada ya kumaliza chuo. Na watu inafikia hatua wanakuona mpuuzi japo unakuwa na elimu yako.
Kwani kuna ulazima wa kusubili michongo? Mm kwa upande wangu naona kuwa vijana hatupendi kujiajiri bali tunakaa kusubili ajira huku tukilalamika kuwa maisha ni magumu bila kuchukua hatua
 
Kwani kuna ulazima wa kusubili michongo? Mm kwa upande wangu naona kuwa vijana hatupendi kujiajiri bali tunakaa kusubili ajira huku tukilalamika kuwa maisha ni magumu bila kuchukua hatua
Hatuna uthubutu.
Lakini utathubutu vipi bila kianzio cha kukuwezesha.
 
Ndugu kianzio si lazima kiwe kikubwa, kama una nia ya dhati hata Elfu 10 ni mtaji tosha
 
Kwani kuna ulazima wa kusubili michongo? Mm kwa upande wangu naona kuwa vijana hatupendi kujiajiri bali tunakaa kusubili ajira huku tukilalamika kuwa maisha ni magumu bila kuchukua hatua
Wajiajiri na nini mkuu wakati mitaji hawana? Ndo wanahangaika kujikusanya ktk vibarua vinavyowaingizia kipato kidogo mno!! Habari gani kwa wale waliopata nafasi wakaingia kwenye kujiajiri mara biashara au kilimo kikayumba na kupoteza kila kitu nao utawaita wavivu? Mkuu vijana wana njozi na uwezo wa kupambana wanao ila vianzio ndiyo shida kumbuka kama kuna mtu alianza safari yake bila kuyumba basi ni wachache ila hao unaowaona wavivu wapo katika shule ya muda ya maisha, acha waujue upande mwingine wa shilingi ya maisha, kuna vingi hii shule inawafundisha wakija kupata gap hakika utayaona mambo yao na mipango yao ikiwa safi, na hutaamini. Nina uzoefu na hiki nilichokiandika hapa.
 
Ni ujinga uliopitiliza kuwalaumu vijana kwa jambo lolote as if hao vijana walijizaa na kujilea wao wenyewe hadi kufikia hatua waliyonayo kwa sasa.

Chochote kinachofanywa na vijana huwez kukitenganisha na misingi waliyokulia hawa vijana.

Na maisha wanayoyaishi ni matokeo ya kile ambacho jamii imekuwa ikiwalisha tangu walipozaliwa.

Sasa wewe badala ya kukomaa na mzizi wa tatizo, wewe unakomaa na tatizo huku chanzo unakiacha kiendelee kuzalisha unproductive population group.
 
Tatizo hawa wanaozalisha watoto na kutekeleza tunakuwa hakuna malezi mazuri ya baba wala mama, tunakulia magetoni, hakuna ramani yeyote ya maisha,...maisha atayaanza vipi
 
Wajiajiri na nini mkuu wakati mitaji hawana? Ndo wanahangaika kujikusanya ktk vibarua vinavyowaingizia kipato kidogo mno!! Habari gani kwa wale waliopata nafasi wakaingia kwenye kujiajiri mara biashara au kilimo kikayumba na kupoteza kila kitu nao utawaita wavivu? Mkuu vijana wana njozi na uwezo wa kupambana wanao ila vianzio ndiyo shida kumbuka kama kuna mtu alianza safari yake bila kuyumba basi ni wachache ila hao unaowaona wavivu wapo katika shule ya muda ya maisha, acha waujue upande mwingine wa shilingi ya maisha, kuna vingi hii shule inawafundisha wakija kupata gap hakika utayaona mambo yao na mipango yao ikiwa safi, na hutaamini. Nina uzoefu na hiki nilichokiandika hapa.
Umeongea ukweli mtupu mkuu
 
Ni ujinga uliopitiliza kuwalaumu vijana kwa jambo lolote as if hao vijana walijizaa na kujilea wao wenyewe hadi kufikia hatua waliyonayo kwa sasa.

Chochote kinachofanywa na vijana huwez kukitenganisha na misingi waliyokulia hawa vijana.

Na maisha wanayoyaishi ni matokeo ya kile ambacho jamii imekuwa ikiwalisha tangu walipozaliwa.

Sasa wewe badala ya kukomaa na mzizi wa tatizo, wewe unakomaa na tatizo huku chanzo unakiacha kiendelee kuzalisha unproductive population group.
Umenena point muhimu sana,Jamii na siasa ya nchi yetu haiko pouwa.
Mfano mimi mwenyewe mwaka jana niliooteza mtaji wangu wa 1million plus baada ya waziri mkuu kuzuia mahindi kuzuia mahindi kwenda nje ya nchi.
Sasa kwa mazingira hayo kwa nini nisibet tu huenda siku moja nikapata.
Tusilaumiane sana tuangalie kiini cha tatizo kama mdau ulivopendekeza.
 
Umeongea ukweli mtupu mkuu
Ndo hivyo mkuu, vijana hasa hawa graduate wanalaumiwa sana wakati mifumo yetu ndo haipo sawa, watu wapo tayari kwa kufanya vitu vikubwa lakini vianzio na changamoto zake hata baada ya kuanza ni kubwa kuwazidi hata kama imetokea wewe ukafanikiwa usidhani wote watafanikiwa kwa muda huo huo, tukumbuke kuwa kila mmoja ana wakati wake wa kutusua kikubwa ni kuwa na njozi na mipango madhubuti.
 
Back
Top Bottom