Vijana walioko kwenye uongozi ambao tulikuwa na imani nao wametuangusha na wanazidi kuididimiza nchi hii. Hivi inakuaje kijana mwenye akili timamu kutumikia ufisadi? Hivi hatujui kwamba kizazi chakondokitapata shida miaka hijayo? Hivi unaona raha gani kusaliti wananchi wa Tanzania kisa kupewa pesa za kula na magari ya kutembelea? Hivi ni miaka mingapi utaishi hapa duniani kabla ya kufa? Hivi hao watoto na familia yako wakati hukiwa umekufa nao utawaachia husia kwamba wafanye mambo mabaya hili waendelee kuishi kama wakati ambao hupo hapa duniani?
Embu kijana wa kitanzania tufikirie sana sana. Leo nimesikia DW vijana wa Rwanda wameshindwa kupewa matokeo yao ya kidato cha sita kisa wamegoma kujiunga na M23. Wamekimbilia nchi jirani na pia wamesema wanatishiwa kuuliwa na wanausalama wa kwao kisa wamegoma kutumikia mambo ambayo hayana faida kwa wananchi wengine. Hivi sisi vijana wa Tanzania tunashindwa kukataa mambo kama hayo? Hivi kwenye nyumba za ibada tunaendaga kujionyesha kwa watu au tunakwenda kumwomba mungu? Mimi nazani wewe kama unashiriki kwa namna moja au nyingine ktk kuleta maisha ya mtanzania kuwa magumu jifikilie mara mbili mbili.
VIJANA WA TANZANIA TUBADILIKE, HII NI NCHI YETU SIO YA WATU WACHACHE, TUKATAE KUTUMIKA WAKATI MAMA, WATOTO, BABA, BABU, BIBI NA NDUGU ZETU WANAKUFA KWAKUKOSA MATIBABU YA HUAKIKA, VIJANA TUNAKOSA ELIMU BORA, HAKUNA MADAWATI, HAKUNA VITABU, WALIMU HAWAENDI KWENYE KOZI ZAO KUIMARISHA UJUZI, MAJI VIJIJINI HATA MIJINI BADO SHIDA, MAGONJWA YA KAWAIDA YANATUMALIZA, KILIMO BADO HAKIJA IMARIKA.
TAFAKARI, CHUKUA HATUA.