POTOSHI Video hii imetengenezwa kwa akili unde (AI)

POTOSHI Video hii imetengenezwa kwa akili unde (AI)

Uhalisia wa taarifa hii umepindishwa ili kupotosha
Source #1
View Source #1
kumekuwepo na video hi inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii husasani facebook na tiktok je ukweli wa video hii ni upi?


Screenshot_20251203-100319.jpg

 
Tunachokijua
Kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii kumekuwa na kipande cha video kinqchosambazwa na watumiaji mbalimbali kikionesha watalii wakiwa mbugani na mmoja wao anabebwa na Twiga.

Je, video hiyo ni halisi au imetengenezwa kwa Teknolojia ya Akili Unde?

JamiiCheck imefuatilia na kubaini kuwa video hiyo si halisi bali imetengenezwa kwa teknolojia ya akili unde.

Video hiyo ina mapungufu kadhaa ikiwemo si rahisi Twiga kumbeba binadamu mkubwa hivyo na kukimbia naye kwa kasi kubwa.

Aidha kwa kutumia nyenzo za kidigitali ikiwemo ya Hive Moderation, JamiiCheck imebaini kuwa video hiyo imeundwa kwa AI kwa takribani 99%.

1764837677380-png.3511181
Msiisumbue jamiichek kwa vitu vidogo kama hivyo.
Mbona iko wazi kabisa ni AI
Kuna vitu vingine hadi unabaki na wasiwasi wa uelewa wa mleta hoja,hii hata mtoto wa chekechea atakuambia ni katuni,kwa kuwa hajui mambo ya AI.

Sasa mtu mzima anayejua Kutumia smartphone na kupost vitu eti hajui kuwa hii ni AI ama sio
 
Kwetu sisi gen z kujua kama ni AI ni rahisi sana 🙌

Ila sasa kwa wale wa 70's mpaka 80's mnapata tabu sana
 
Back
Top Bottom