uzito wa maneno ya viongozi.

uzito wa maneno ya viongozi.

asakuta same

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2011
Posts
14,829
Reaction score
5,039
Nchi za wenzetu kauli ya kiongozi inatosha kumfanya kiongozi awajibike kisiasa kwa kuachia wadhifa wake.
Tofauti na hapa Tanzania viongozi wamekuwa wanatoa maneno yenye utata , ubaguzi , kejeli , chuki , dharau na uongo bila kuzichukulia hizo kauli uzito wowote.

Leo hii anasimama waziri mkuu anasema " hizi fedha si za umma" , halafu imakuja kudhibitika ni za umma na umetumika udanganyifu kuzipora lakini hatuoni umuhimu wa yeye kuwajibika kwa kauli yake hii.

Leo hii anasimama waziri wa nishati na madini anadanganya ndani ya bunge kwa kejeli na ubabe na anasema fedha zilizodhibitika na mkaguzi mkuu wa Serikali ni fedha za Umma , lakini inaonekana hamna umuhimu wa yeye kuwajibika kwa kauli yake hii.

Leo anasimama katibu mkuu wa wizara anadanganya anapotosha na anakejeli mbunge , lakini tunaona hakuna umuhimu wa kumuwajibisha huyu kwa kauli yake.

Leo hii ana simama mwanasheria mkuu wa serikali anayekejeli kwa kumuita mbunge ndani ya bunge "tumbili" , "hizi fedha siyo za umma" , mimi ndiye niliidhinisha zitoke" , leo hii inaonekana hakuna umuhimu wa hawa watu kuwajibika.

Kama TAIFA la Tanzania ndiyo tupo hapa basi Viongozi wetu wa umma ni genge la wahuni kama wakaao vijiweni lisilojali linataamka nini , wapi na wakati gani.

Imefikia mahali tumechoka kuibiwa fedha zetu na watu tuliowakabidhi dhamana ya kutulindia , Watanzania tuchukue hatua sahihi kuiwajibisha hii serikali ya wezi na watetea wezi.
 
Umechelewa tu kujua kuwa nchi yetu haina viongozi! Hata gennge la majambazi hufika wakati likaamua kupumuzika au hata kuchagua kipi wapore na kipi wasipore. Hawa jamaa they will still kitu chochote na wakiweza hata uchafu wa c-h-o-o-n-i
 
Tuna tatizo la uwajibikaji katika taifa letu, yaani bunge limeshindwa kuwawajibisha majizi yenye vyeo vya ubunge kwa kuvuliwa vyeo walivyopewa na bunge, kwa mfano chenge anapaswa kuvuliwa cheo chake cha mwenyekiti wa kamati ya bajeti ya bunge. Bunge liingize maazimio haya waziwazi na umma uone, bila kuchukua hatua hiyo bunge haliwezi kuwa jasiri kunyoshea vidole muhimili mwingine. Waanze wenyewe kwanza kuwajibishana!
 
Kuna watu wameshajifanya nchi hii yao peke yao.

Namlaumu Rais wetu kwa kutudhihirishia udhaifu wa wazi.

Ningekuwa karibu naye ningembonyeza tezi lake dume hadi akome...hawezi kuwa kimya tu na watu wanaglma kuwajibika yeye ametulia tu.
 
Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya udhaifu wa Rais Kikwete..JM
Naibu spika: Futa kauli
JM:Sifuti kauli
 
Kuna watu wameshajifanya nchi hii yao peke yao.

Namlaumu Rais wetu kwa kutudhihirishia udhaifu wa wazi.

Ningekuwa karibu naye ningembonyeza tezi lake dume hadi akome...hawezi kuwa kimya tu na watu wanaglma kuwajibika yeye ametulia tu.
Mimi nawalaumu zaidi Wananchi kwa ujumla.
Yaani tupo wapole sana , tumezoea kulalamika tu.
 
Back
Top Bottom