Habari zenu jf, moja kwa moja kwenye mada hivi uzinzi mnauchukuliaje, maana nilikuwa nasikiliza kipindi cha mwarobaini cha chaneli ten, nadhani kuna swali walikuwa wameuliza ambalo linauhusu siri ambazo umewahi kufanya wakati uko na x wako na hajawai kuzijua mpaka leo. Baadhi ya majibu kutembea na mashosti zake x, kuzaa na mjomba, kutembea na marafiki wa kiume, kutembea na baba na mtoto ingawa demu alimuacha mtoto kazamia kwa mshua. Nimejikuta naumia ndani yangu ghafla, alafu na kuwa na maswali mengi kwa Mungu wangu cjui hata nisemeje. Hivi nyie wezangu mnachukuliaje
Leo nilihudhuria ibada,ktk homilia Padre akatoa mfano namna dunia ya leo watu wanavyoaminishwa kwamba hii miili yetu ni mali yetu na siyo Hekalu la Roho Mtakatifu (Wakorinto 1 6:19) ,somo muhimu sana la kujua kusudi la uzima tulio nao,nguvu tulizo nazo akili zetu tunazitumia kuwaza nini?
Watu wanaamua tu wazini,waibe waue wenzao,wasengenye wenzao kuwakatishia ridhiki zao yote yakifanywa na kiumbe ambae ilibidi awaze mema kwake na kwa wenzake