Polisi wengi mtawaonea tu hawanaga tatizo na mtu zaidi ya kuchukua virushwa vidogo vidogo vya kubrashia viatu.
Kazi ya uaskari ni kazi ya maelekezo kutoka kwa boss na maelekezo haya hutolewa kwa mfumo wa amri (commands), askari wa cheo kidogo kazi yake ni kupiga saluti na kusema ndio afande/ndio mkuu. Hilo liko hivyo mpaka Ulaya ambako wewe namimi tunadhani polisi wao ni tofauti.
Askari asiyetii maelekezo ya mkuu wake anachukuliwa hatua za kinidhamu ambapo ni pamoja na kufukuzwa kazi, sasa kama Mwijage ambae ni waziri anaogopa kufukuzwa je polisi constable? Ni vema mkajua hata polisi nao wana familia zinawategemea.
Maskini jeuri hua ni msemo tu, hata wewe na mimi tukiwa polisi leo hali uitakua ile ile tu, tukitaka kuibadilisha ni mpaka tubadilishe katibu yetu ili rais na viongozi wastaafu waweze kushtakiwa wanapomaliza awamu zao.
Hapo ndipo uwezo wa jeshi ulipoishia. Badala ya kuhakikisha mikutano inafanyika kwa amani, kama sheria inavyoruhusu na kutoa haki kwa wananchi, wao hawatekelezi wajibu wa kazi yao ya kuwalinda wananchi na mali zao, bali kutumia njia rahisi ambayo inawanyima haki ya msingi kabisa, wananchi wanaowalipa mshahara ambao hata hawaufanyii kazi.