Utapeli katika kuomba kazi 'data entry'

Mapujds

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2011
Posts
1,286
Reaction score
129
HABARI WAKUU
Jana niliomba kazi kupitia zoomtanzania kuhusu data entry zilitolewa nafasi sita, muda huu nimepokea sms ifuatayo ikiwa na maelezo ya kufanya baadhi ya mabo ili nipate kazi, sms ndo hii
"Habari, naitwa Shafii From Data Plus Dar. Nipo kikaoni tunapitia CV tupate majina ya kuinterview for Data Entry Post. I Like your Cv na ntakusaidia upate hii kazi kwa sharti lifuatalo, Mshahara ni 1.5 Million kwa mwezi, ukilipwa mwezi wa kwanza utanipa Sh. Laki 3 for helping you, If you agree do the following, By saa 11 Jioni uwe Umetuma Scaned Copy Ya vyeti Vyako to africfuture@gmail.com Na Sh. Elfu 30 by Tigo pesa kwenye namba hiihii au M-pesa 0764642365 ili nimpe mtu wa interview anipe maswali ntakutumia kwenye e-mail, Nikitoka kikaoni utapigiwa simu lini uje for Interview".namba ya mtumaji ni 0652795853
huu si wizi wakubwa?
 
mwambie akufanyie mpango upate kazi ikibidi atoe elfu 30 zake halafu mshahara wa kwanza unamwachia wote. Au unamwachia mishahara ya miezi 3 mfululizo.utashangaa tu hatoi tena ushirikiano.
 
Daaah kwahiyo km hauna hela???daaah nchi hii inaenda wapi cjui........!
 
Huyo ni shafii bana zile zile za akina rachel wana tangaz la kaz la project officer(9) nako ni hvyo wanatak elfu30 me naona hapo zoom ndo gear ya kupata pesa mana wanajua weng wanaipitia bahati mbaya n kwamb wameiba sana tangu desemba walianz na elfu 10 wakapanda mpak30 .hakika wizi mbaya cjui kama wanapata nn maana many people wamediscover hzo mbinu zao
 
Kuna watu wangu wa karibu watatu wamenitumia hizi sms baada kuomba hizo nafasi,hawa dawa yao ndogo sana maana utapeli wao wenyewe ni wa kishamba sana.

totolucky wa Zoom inabidi mjipange kuhakiki kama kweli kampuni husika zinazotangaza nafasi ni halali ili iwe rahisi kuchukua hatua.Zipo njia rahisi tu kujua uhalali wa kampuni kama ina exist.

Kuweni makini na wizi wa namna hii hasa kwa vijana wetu walio desparate na ajira.
 
Last edited by a moderator:
ndio zao hawa matapeli mi washanitummia sana hizo mesegi looh ..ikafikia hatua nikawatukana sana waisnitumie msg zao za wiziii.... zoom sasa hivi kumeharibika sana
 
mwambie akulipie kisha ukipata kazi utampa laki tatu na nusu.
 
hizo namba kwanini msiwape polisi wazifanyie kazi?
 
thanks to MOLA NA JF kumenifanya nifunguke sana kuhusu matapeli, siwezi kuibiwa kirahisi rahisi
 

same message nami nimeipata leo! kiukweli hapa hamna lolote kama bahati ipo ipo tu
 
same message nami nimeipata leo! kiukweli hapa hamna lolote kama bahati ipo ipo tu
Looks like jana walikuwa na project hii ya kuendelea kudhulumu,hawa ni matapeli kwasababu namba wanazozitumia zimetengenezwa mwezi huu huu wa pili..hakuna chochote wanachofanya kwenye namba hizo zaidi ya kupokea hela za watu wanaotapeliwa.

Angalieni shot hii..
 

Attachments

  • Screen_20130218_170018.jpg
    42.2 KB · Views: 101
Aise happen to me just few minutes,nimemwambia anilipie then nitamrudishia later.
 
I received the same msg! duh hawa watu balaa, lkn kwan kazi mpaka utoe rushwa mawazo ya kizamani sn.
 
Hizo namba zimesajiliwa kwa majina ya i Abasi madenge na Shaffy Madenge mnaweza kuwaripoti kwa kuomba rushwa ili liwe fundisho
 
Habari, kwanza napenda kuwajulisha kuwa ZoomTanzania sio recruitment agency, ZoomTanzania ni Online Business Directory na katika mambo tunayofanya ni kutangaza nafasi za kazi. Kutangaza kazi ZoomTanzania ni bure, nataka kuwajulisha kuwa kuna watu wanatumia nafasi hiyo kuwaibia watafutaji kazi. Hii ni sababu wanajua kuna watu wako desperate na kupata kazi na watashawishika kulipia nafasi hizo. Kila mtu anayetuma maombi ya kazi kwa kupitia ZoomTanzania ana account, siku ya kufungua account kulikuwa na Code of Conducts na katika Code mojawapo ilisema hivi " I understand that I should never be asked to make a payment to apply for any job. I will report to ZoomTanzania.com any employer that requests a payment." na tunashukuru kuwa kuna watu wamekua wakitusaidia kureport kazi ambazo wameombwa kutoa malipo ya aina yoyote. ZoomTanzania haihusiki na utapeli huu, narudia tena ni watu wachache wanaotaka kutake advantage ya jobseekers wanafanya mchezo huo. Kila listing inayoingia ZoomTanzania inapitiwa na nakubali wakati mwingine ni ngumu kujua ipi ni ya kweli na ipi sio. Lengo la ZoomTanzania ni kuwahabarisha kuhusu nafasi za kazi mbalimbali lakini kuna waharibifu wanatuchafulia jina letu. Napenda kushukuru kwa wale wote watupao taarifa ya nafasi mbalimbali wanazokuwa na mashaka nazo. Utapeli wa namna hii unatumika sio Tanzania tu ata nchi zingine. Mi ninachoomba tufanye kazi pamoja, kutusaidia kutoa taarifa pale mtu apatapo ujumbe kama huo. ZoomTanzania najua wengi mnakubali tunatangaza nafasi za ukweli na wengine mmewahi labda kuitwa katika interviews ama kupata kazi kwa kupitia Zoom. Naomba tushirikiane katika hili. Asante.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…