sepema
JF-Expert Member
- Jun 13, 2019
- 591
- 1,000
Habari zenu wakuu.
Nimekutana na vurugu yahatari jioni hii. Jamaa alikuwa anatwangana makonde na mdada fulani. Mdada alikuwa mzuri wasura na umbo. Hata hivyo alionekana nimzuri kwenye mapambano yakutumia mikono yake.
Baada ya wadau kusogea karibu tukasikia mdada analalamika kwamba jamaa kamwambia ananuka mdomo.
Jamaa nae Huku akiendelea kujitetea asiumizwe sana kwani alionekana kuzidiwa nguvu na mdada, akawa anasema jamani Kama mnabisha mkaribieni karibu mtaamini nilichomwambia.
Watu waliokuwa wanamfahamu yule dada wakawa wananong'ona kwamba nikweli mdada anakaharufu fulani mdomoni.
Walichokuwa wakilalamika mashuhuda nikwamba jamaa hakutakiwa amwambie live yule dada kwani kwa wao walivyotafsiri ni tukio la udhalilishaji.
Mwisho ugomvi ule uliamuliwa na kila mmoja akapita njia yake.
Sasa wakuu tusaidiane, wewe mtu akija kwa ujasiri akakwambia ukweli kuwa unanuka mdomo utafanya Jambo gani kuonyesha kuwa ujumbe umekufikia?
Wasalaam!
Nimekutana na vurugu yahatari jioni hii. Jamaa alikuwa anatwangana makonde na mdada fulani. Mdada alikuwa mzuri wasura na umbo. Hata hivyo alionekana nimzuri kwenye mapambano yakutumia mikono yake.
Baada ya wadau kusogea karibu tukasikia mdada analalamika kwamba jamaa kamwambia ananuka mdomo.
Jamaa nae Huku akiendelea kujitetea asiumizwe sana kwani alionekana kuzidiwa nguvu na mdada, akawa anasema jamani Kama mnabisha mkaribieni karibu mtaamini nilichomwambia.
Watu waliokuwa wanamfahamu yule dada wakawa wananong'ona kwamba nikweli mdada anakaharufu fulani mdomoni.
Walichokuwa wakilalamika mashuhuda nikwamba jamaa hakutakiwa amwambie live yule dada kwani kwa wao walivyotafsiri ni tukio la udhalilishaji.
Mwisho ugomvi ule uliamuliwa na kila mmoja akapita njia yake.
Sasa wakuu tusaidiane, wewe mtu akija kwa ujasiri akakwambia ukweli kuwa unanuka mdomo utafanya Jambo gani kuonyesha kuwa ujumbe umekufikia?
Wasalaam!