Usiyaogope maisha

Mungu akubariki.
 
Nimea assume tu mkuu kwa sababu wewe kwenye kutembeza fimbo hujambo.
Sasa naomba nikupe maarifa,kwenye maisha jitahidi kuto assume kitu,pili kama umesoma vizuri nyuzi zangu,yes hayo mambo ndio niliyafanya lakini miaka 40 iliyopita kwa hii age kwa sasa,nafanya mambo yafuatayo:
1.nasaidia wanaume na wanawake kuoana,na hapa nimewezesha kama ndoa 3 au 4 hivi
2.nasaidia kusuluhisha migogoro ya ndoa
3.nashauri vijana juu ta mbinu za kukabiliana na maisha
 
Nakuuelewa mkuu lakini nikikumbuka ule Uzi wako usemao fimbo ya ukwaju napata mashaka mkuu.
 
Siri kubwa ya ushindi ni uvumilivu,kwa viongozi wa siasa uvumilivu huo huitwa stahmala,kwa maisha ya kawaida ni uvumilivu,utulivu na kutopapatika kujibu au kufanya kitu bila tafakiri kubwa.Angalia navyojibu hoja humu,kuna watu wananitukana,sijibu kwa matusi,kuna wanaokejeli,siwajibu kwa kejeli,kuna watu wanatoa kashfa mie najibu kwa staha.Basi tumeumbwa kusaidiana humu duniani hata mimi nilisaidiwa sana tu.Mimi niliwahi kwenda faroe islands na nikaugua ghafla nikiwa supermarket,nilianguka ghafla,pembeni yangu alikuwepo dada mmoja mwafrika akakimbia kunisaidia,kwenye koti nililovaa kulikuwa na pin ya rangi za bendera ya tanzania,akaniuliza hii umepata wapi? maana kwa wajihi wangu huwezi kuamini kuwa mie ni mtanzania maana nimetokea na rangi ya baba yangu.Nikamjibu mimi ni mtanzania.Akanisemesha kiswahili na tukaongea,yeye ndio alisimamia matibabu yangu yote,guess what? huyo dafa anaitwa paulina,mnyakyusa ila kaolewa faroe islands
 
Mambo magumu sana sana jamani,sijui tufanyeje?
 
Mungu akupe kheri kwa mazuri uliyodhamiria mkuu..

Kwa dunia ya sasa kuna watu wanahitaji hata space ya mtu kuonesha anajali wanayopitia ili wapate ahueni ya kiakili na kihisia

Kuna wengine wanahitaji msaada wa kifedha

Wengine kiroho na kiakili

Inahitaji commitment na dedication kufanya haya. Wengine ndio maana wanaanzisha NGOs lakini kwa unachojitolea kwa capacity yako bado ni sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…