USIOMBE IKUTOKEE

moyafricatz

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2015
Posts
2,905
Reaction score
4,928
*Vuta picha umelala mida ya alfajiri hivi usingizi ule wa kukesha jana yake*.

*Halafu kuna mtu anakuja kukugongea mlango kwa fujo sana kwenye mida ya kama saa moja moja hivi*.

*Ile unaamka na hasira zako kwenda kumfungulia unajikwaa kidole cha mwisho cha mguu ktk kona ya kitanda ile ndiiii.. kugeuka unaparamia ndoo za maji yanamwagika*.

*Mara unateleza ktk yale maji unaangukia meza unaangusha tv, deki na wewe chini* 🤣

*Mara waya wa umeme unakupiga short mgongoni, unafika mlangoni na maumivu ya kidole + uchovu + hasira + hasara na short juu unakutana na jamaa anakwambia nasajili line za Halotel!*


*Hapa ndo utaelewa samehe 7x70 inamaanisha nini*
 
Iliwahi nitokeaga hiyo nilikuwa nimelala mchana nikasikia mlango unagongwa nikaamka bahati mbaya nikajigonga kwenye mlango wa sebuleni mpaka ngeu , nakwenda kufungua mlango wa nje nikakuta bint mdogo anauza sabuni sikumbuki nilichomjibu nikafunga mlango nikasema "ah nilijua mtu wa maana" japo hakusikia

Lakini baadaye baada ya kukaa sawa nafsi yangu ilinisuta na niliumia sana kutamka maneno yale.

Huyo jamaa wa Halotel ningemsamehe tu.
 
Iliwahi nitokeaga hiyo nilikuwa nimelala mchana nikasikia mlango unagongwa nikaamka bahati mbaya nikajigonga kwenye mlango wa sebuleni mpaka ngeu , nakwenda kufungua mlango wa nje nikakuta bint mdogo anauza sabuni sikumbuki nilichomjibu nikafunga mlango nikasema "ah nilijua mtu wa maana" japo hakusikia

Lakini baadaye baada ya kukaa sawa nafsi yangu ilinisuta na niliumia sana kutamka maneno yale.

Huyo jamaa wa Halotel ningemsamehe tu.
 
Hii simulizi inafanana na mchungang'ombe kusimamisha basi la abiria likiwa mwendokasi likitokea mkoani kuelekea Dar, kisha kuuliza majira, eti "sahizi sangapi brother kaka?"
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…