Usilazimishe penzi hata kama umependa

Anold

JF-Expert Member
Jul 15, 2010
1,456
614
1. Ukipenda sipopendwa, adhabu wajitakia,
Moyo utapondwapondwa, maradhi wajitakia,
Utachekwa na watawa, aibu itatukia,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

2. Usilazimishe kupenda, majuto yatakujia,
Mtima utakupinda, ubovu utaingia,
Wajuzi watakuwinda, wakubeze kwenye njia
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

3. Mpende mwenye kupenda, mwache asiyekupenda,
Usishindane mshinda, dhalili itakudenda,
Ghadhabu itakuwinda, kama kamanda wa kanda,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

4. Meseji utazituma, vocha nazo hupeleka,
Utabaki uyatima, faida hutaidaka,
Utaingia gharama, ukose hata nafaka,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

5. Mtaani utabezwa, vijiweni utangazwe,
Hutakosa kubatizwa, buzi jina utawazwe,
Wataikosa na dawa, ili japo utulizwe,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

Nimeandika shairi hili kuwaonya wale wanaolazimisha kupenda/kupendwa kwani majuto, kuvunjwa moyo, kukatishwa tama na hata kudhalilishwa na kupotezewa muda na pesa ni sehemu ya adha wanazokumbana nazo siku hadi siku. Lazima ujenge utaratibu wa kutathmini mahusiano yako na mpenzi wako kama yana ufanisi na faida kwako.
 
Umenigusa mkuu,
saingine ukipenda hata alama unashindwa kusoma vizuri.
Sasa unapotendwa mhhh!
 
Mkuu yalinikuta hayo niliteswa nikaliwa hela zangu mpaka kuja kushtka nilishafilisiwa vya kutosha ila malipo ni hapa hapa duniani n i kno god is there.bt stay in touch mkuu shairi fundishoni
 
1. Ukipenda sipopendwa, adhabu wajitakia,
Moyo utapondwapondwa, maradhi wajitakia,
Utachekwa na watawa, aibu itatukia,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

2. Usilazimishe kupenda, majuto yatakujia,
Mtima utakupinda, ubovu utaingia,
Wajuzi watakuwinda, wakubeze kwenye njia
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

3. Mpende mwenye kupenda, mwache asiyekupenda,
Usishindane mshinda, dhalili itakudenda,
Ghadhabu itakuwinda, kama kamanda wa kanda,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

4. Meseji utazituma, vocha nazo hupeleka,
Utabaki uyatima, faida hutaidaka,
Utaingia gharama, ukose hata nafaka,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

5. Mtaani utabezwa, vijiweni utangazwe,
Hutakosa kubatizwa, buzi jina utawazwe,
Wataikosa na dawa, ili japo utulizwe,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.

Nimeandika shairi hili kuwaonya wale wanaolazimisha kupenda/kupendwa kwani majuto, kuvunjwa moyo, kukatishwa tama na hata kudhalilishwa na kupotezewa muda na pesa ni sehemu ya adha wanazokumbana nazo siku hadi siku. Lazima ujenge utaratibu wa kutathmini mahusiano yako na mpenzi wako kama yana ufanisi na faida kwako.

Ni kweli mkuu. Huwezi kulazimisha maji yapande mlima. Hata ukitumia pump, siku ikiharibika yatafuata mkondo, nawe utabakia kulia 'maji yangu, maji yangu' wakati yatakuwa yanatumiwa na wengine kwenye bustani zao.
 
Back
Top Bottom