Mkubwa Dawa
Member
- Nov 13, 2008
- 64
- 1
Naomba nichukue fursa hii kuomba msaada kufahamishwa kuhusu ushuru wa kutoa gari bandarini. Je kuna unafuu wowote wa kodi kwa mwanafunzi wa kitanzania aliyekuwa masomoni ng'ambo anapotaka kuingiza gari ya matumizi ya binafsi? Na kama ipo afueni ya kodi je ni asilimia ngapi inatakiwa kulipia ushuru? Vile vile nilikuwa naomba kama naweza kufahamishwa links za madalali wa magari japan.
Shukrani.
Hakuna msamaha wa kodi kwa mwanafuzi wa ki-TZ aliyekuwa nje kwa masomo pale anapofika nchini na kutaka kununua gari, labda uwe mtumishi wa umma tayari. Ila kama gari ulilinunua ukiwa huko ng'ambo na ukalitumia angalau kwa mwaka mmoja kama sikosei ndo kodi hupungua ukija nalo japo sijui ni kiasi gani.
Mawakala wa magari japani waweza kutembelea links hizi hapa japo kwa uchache.
www.autotrader.co.jp, http://www.tradecarview.com, http://ccnjp.com. www.japanesevehicles.com.
Pia waweza kuutumia mtandao vizuri kutafuta mawakala huko maana wako wengi mno ila uwe makini kuna watu walituma pesa na hawakupata hayo magari.
Ahsante ndugu mwendapole kwa kunijuza kuhusu hiyo taarifa.Kama ulinunua gari na kulitumia ukiwa huko nje kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja ukirudi nalo bongo hautakiwi kulipa kodi ya aina yeyote.
Kama ulinunua gari na kulitumia ukiwa huko nje kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja ukirudi nalo bongo hautakiwi kulipa kodi ya aina yeyote.
Hii sheria ya kijinga kweli, yaani ununue gari ulitumie ndio ukileta upate punguzo la ushuru, badala ya kuhamasisha kuleta gari mpya ndio upewe punguzo la ushuru, serikali yetu na sheria zake zinazotungwa na wachaga wa pale TRA zinatuhamasisha tulete ma-scrap! ajabu kubwa hii.
Ingekuwa, ukitoka nje, kama unasoma au kufanya kazi huko, hakikisha gari lako ulilokwisha kulitumia bovu bovu, liache huko huko na jaribu kuja na jipya au jipya jipya (kama una uwezo) na sisi (serikali) kukuhamasisha na kuhamasisha wengine wafanye bidii ya kwenda nje, tutakupa ahueni ya ushuru asili mia 100. Au mtu kakaa anasoma, ka save vipesa vyake, kajinyima hata kula vizuri huko nje ili akirudi anunuwe gari japo sekeni-hendi aje nalo, naye japo aonekane kweli katoka nje, anaambiwa mpaka awe amekaa nalo huko nje zaidi ya Mwaka, sasa hii ni akili kweli?
Hii mitunga sheria ya nchi yetu inatunga sheria za kiroho mbaya tu, misheria ya kukomoana tu. Hivi lini tutajikombowa japo kwa kuwa na sheria za kusaidiana badili ya hizi za kukomoana. Hiki kipengele cha ''zaidi ya mwaka mmoja'' kina husu nini? na kina faida gani? Hata mtu akienda katika ki semina au ki shoti-kozi cha miezi miwili, akajipatia kigari chake cha dola elfu mbili, ukimsaidia ushuru si umemsaidia maisha yake na usafiri na umehamasisha yeye na wengine kufanya bidii ya kwenda huko nje? Hii fikira ya kuwa magari ni kitu luxury, ililetwa na nani hasa?
Kwa kuongezea, utalipa tu kodi ya uchakavu (chuma chakavu) kama gari ni la chini ya mwaka 2000 isipokuwa pickups/double cabin, malori, matrekta na mabasi. Vinginevyo kama waliosema hapo juu, kaa na gari mwaka mmoja nje ya nchi na utaliingiza bila ushuru
Ahsante Mwalimu Zawadi lakini tumlaumu nani TRA au bunge lilopitisha sheria maana gari nadhani ni kitu ambacho mtu unahitaji kula siku lakini bado kodi ipo juu na mizengwe chungu nzima!Ukabila! ukabila! ukablia! Mkuu Dar es Salaam, sheria zinapitishwa na bunge au kuna kabila la kupitisha sheria?
MziziMkavu ntawasiliana na wewe basi kwa hotmail ili nijue kiunagaubaga zaidi. Shukrani!Mkubwa Dawa kama unataka Gari zuri pasipo na wasiwasi jaribu kuwasiliana na mimi kwa email nitakupa Contact ya mtoto wa kaka yangu anaishi UK uwasiliane nae yeye ndio shughuli zake za kununuwa magari na kuuza huko UK na ni mkweli hana wasi wasi kimaisha ukiwasiliana nae tu anaweza kukuletea hapo bongo kwa njia ya contena ili mradi mkubaliane nae bei nitumie email ili nikupe contact zake email yangu ni fewgoodman@hotmail.com
Naomba nichukue fursa hii kuomba msaada kufahamishwa kuhusu ushuru wa kutoa gari bandarini. Je kuna unafuu wowote wa kodi kwa mwanafunzi wa kitanzania aliyekuwa masomoni ng'ambo anapotaka kuingiza gari ya matumizi ya binafsi? Na kama ipo afueni ya kodi je ni asilimia ngapi inatakiwa kulipia ushuru? Vile vile nilikuwa naomba kama naweza kufahamishwa links za madalali wa magari japan.
Shukrani.
Hii sheria ya kijinga kweli, yaani ununue gari ulitumie ndio ukileta upate punguzo la ushuru, badala ya kuhamasisha kuleta gari mpya ndio upewe punguzo la ushuru, serikali yetu na sheria zake zinazotungwa na wachaga wa pale TRA zinatuhamasisha tulete ma-scrap! ajabu kubwa hii.
Ingekuwa, ukitoka nje, kama unasoma au kufanya kazi huko, hakikisha gari lako ulilokwisha kulitumia bovu bovu, liache huko huko na jaribu kuja na jipya au jipya jipya (kama una uwezo) na sisi (serikali) kukuhamasisha na kuhamasisha wengine wafanye bidii ya kwenda nje, tutakupa ahueni ya ushuru asili mia 100. Au mtu kakaa anasoma, ka save vipesa vyake, kajinyima hata kula vizuri huko nje ili akirudi anunuwe gari japo sekeni-hendi aje nalo, naye japo aonekane kweli katoka nje, anaambiwa mpaka awe amekaa nalo huko nje zaidi ya Mwaka, sasa hii ni akili kweli?
Hii mitunga sheria ya nchi yetu inatunga sheria za kiroho mbaya tu, misheria ya kukomoana tu. Hivi lini tutajikombowa japo kwa kuwa na sheria za kusaidiana badili ya hizi za kukomoana. Hiki kipengele cha ''zaidi ya mwaka mmoja'' kina husu nini? na kina faida gani? Hata mtu akienda katika ki semina au ki shoti-kozi cha miezi miwili, akajipatia kigari chake cha dola elfu mbili, ukimsaidia ushuru si umemsaidia maisha yake na usafiri na umehamasisha yeye na wengine kufanya bidii ya kwenda huko nje? Hii fikira ya kuwa magari ni kitu luxury, ililetwa na nani hasa?
....mimi naomba kujua njia gani nitumie kukwepa huo ushuru, sitaki kukaa nalo mwaka mmoja ughaibuni!
haiwezekani baada ya kulipa ushuru na gharama za usafirishaji najikuta nimetumia almost 100% ya bei nilonunulia 'mtumba' wangu!...
mfano, 25% Import Duty, 18% Excise Duty, na 5% VAT yote ya nini haya wakati Wabunge wanasamehewa ushuru kila miaka mitano wanapoingiza 'mashangingi' ya zaidi ya 30m/=?
...Hii fikira ya kuwa magari ni kitu luxury, ililetwa na nani hasa?
Ukabila! ukabila! ukablia! Mkuu Dar es Salaam, sheria zinapitishwa na bunge au kuna kabila la kupitisha sheria?
KWa mara ya Kwanza naoana mkuu Dar es salaam unaanza kuadmit kuwa kuna mambo ovyo Tanzania. Siku zote wewe unaonekana kuunga mkono kilakitu kinachofanywa na serikali. Siamini kama kweli ni wewe Mkuu Dar es salaam unawashambulia watunga sheria ambao siku zote unawapigania na kuwasifu. Naona kweli Idd el fitr imetuletea mengi, nawashauri jamani tuendelee kufunga akili zetu zinarudi kuwa nzuri.