Ushauri wangu kwa Serikali kuhusu kuhamia Dodoma

Ushauri wangu kwa Serikali kuhusu kuhamia Dodoma

wynejosee

Senior Member
Joined
Jan 28, 2014
Posts
148
Reaction score
59
Kuamia Dodoma serikali ni jambo zuri mno, ila tatizo ni kwamba je wizara zote zitakuwa tayari kujenga ofisi na makazi mara moja kwa watumishi!
Serikali ingechukua uamuzi wa kuhamisha wanafunzi wote wanaosoma faculty ya informatics au Social na kuwapeleka kuwapeleka kule kwenye Faculty ya education ambapo pia kuna majengo Mengi na yatatosha, ili sasa kati ya faculty ya informatics au social ndiopo baadhi ya majengo yatumike kama makazi ya watumishi katika wizara mbalimbali pia kama office za wizara mbalimbali ili tupunguze gharama za kujenga makazi kwa ghafla na ofisi!
Karibu kuboresha wazo na sio matusi.
Wenu katika ujenzi wa taifa hili teule la Tanzania.

Watakao weza mfikishia mkuu wa nchi hili wazo nitafurahi, maana hata ukiangalia kwa TCU guide book UDOM inazidi kupunguza udahili wa wanafunzi tofauti na kipindi cha awali chuo kilivyoanza, mie naamini kuna majengo mengi ya kutosha, hata kiusalama kwa Dodoma UDOM nafikiria ndio the highest peak from the sea level .
 
Mkuu alisema ndani ya miaka 4 ya awamu hii serikali itahamia yote.

Wanaotangulia ni wale wenye majengo ya ofisi tayari. Utaratibu unaendelea kupanga au kujenga kwa wale wasiokuwa nayo. Busara ni kuhama bila kuathiri utekelezaji wa malengo ya wizara/serikali ukizingatia Mkubwa katoa miaka 4.
 
Wizara hata zihamie chini ya miti lakini kuhamia kuko palepale.
 
Kuamia Dodoma serikali ni jambo zuri mno, ila tatizo ni kwamba je wizara zote zitakuwa tayari kujenga ofisi na makazi mara moja kwa watumishi!
Serikali ingechukua uamuzi wa kuhamisha wanafunzi wote wanaosoma faculty ya informatics au Social na kuwapeleka kuwapeleka kule kwenye Faculty ya education ambapo pia kuna majengo Mengi na yatatosha, ili sasa kati ya faculty ya informatics au social ndiopo baadhi ya majengo yatumike kama makazi ya watumishi katika wizara mbalimbali pia kama office za wizara mbalimbali ili tupunguze gharama za kujenga makazi kwa ghafla na ofisi!
Karibu kuboresha wazo na sio matusi.
Wenu katika ujenzi wa taifa hili teule la Tanzania.

Watakao weza mfikishia mkuu wa nchi hili wazo nitafurahi, maana hata ukiangalia kwa TCU guide book UDOM inazidi kupunguza udahili wa wanafunzi tofauti na kipindi cha awali chuo kilivyoanza, mie naamini kuna majengo mengi ya kutosha, hata kiusalama kwa Dodoma UDOM nafikiria ndio the highest peak from the sea level .
Kwanza nikupongeze kwa wazo zuri. tusaidie serikali kimawazo na kimkakati ili kufanikisha zoezi hili ambalo kwangu tangu nikiwa mdogo tuliimba wimbo wa kuhamia makao makuu Dodoma hadi sasa nimeshapata wajukuuu zoezi bado. binafsi naunga mkono Serikali kila linalowezekana lifanyike serikali ihamie Dodoma mengine tutajipanga taratibu. hilo la kutumia majengo ya chuo kwa muda huku tukijipanga vizuri ni jambo jema maana hata hapa Dar kuna wizara au taasisi za serikali zimepanga kwenye majengo ya watu binafsi
 
Hata mi nilikuwa na wasiwasi wa kuhamia Dodoma kwa muda mfupi huu. Gharama ziatakuwa nyingi wakati kuna mambo mengi yanatakiwa kufanyika.
 
Ningelikuwa na uwezo na kama maoni yangu yanasikilizwa ningeshauri kuhamia dodoma kufanyike kwa hatua ambapo wizara zote zisihame kwanza, waanze na taasisi zilizoko chini ya wizara then wizara full zifuate. bila kufanya hivyo kila siku kutakuwa na safari za kuja dar kwa ajili ya kufanya mikutano then back to dodoma.Au serikali ichukue modal ya south africa ambako Executive,judiciary and Legislative ziko sehemu tofauti tofauti. kwa kufanya hivi kutasaidia maendelea ya kila sehemu kuliko kuweka kila kitu dar es salaam.
 
Kwanza nikupongeze kwa wazo zuri. tusaidie serikali kimawazo na kimkakati ili kufanikisha zoezi hili ambalo kwangu tangu nikiwa mdogo tuliimba wimbo wa kuhamia makao makuu Dodoma hadi sasa nimeshapata wajukuuu zoezi bado. binafsi naunga mkono Serikali kila linalowezekana lifanyike serikali ihamie Dodoma mengine tutajipanga taratibu. hilo la kutumia majengo ya chuo kwa muda huku tukijipanga vizuri ni jambo jema maana hata hapa Dar kuna wizara au taasisi za serikali zimepanga kwenye majengo ya watu binafsi
Ahsante sana kwa support yako, ukipata nafasi mdokeze raisi afanye hili....akitaka mawazo mengine ninayo ya kujenga zaidi na si kubomoa!
 
Back
Top Bottom