Bernard bakari
JF-Expert Member
- Mar 30, 2016
- 407
- 781
Ushauri huu sehemu nyingine ukienda hasa kwa wanasaikolojia unalipia pesa kuupata leo mtanzania mwenzangu unaupata bureeeee kabisa, gharama zako ni muda tu unaoutumia kuusoma ushauri huu.
Watu wengi wanayotabia ya kuchepuka, neno hili kuchepuka limechukua matumizi badala ya neno usaliti. Namainisha mwanaume anaweza kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanamke mwingine ile hali anamke wake, au anampenzi wake mwenye lengo la kumwoa. Hali kadhalika vivyo vivyo kwa mwanamke.
Kwanza ifahamike kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria ya ndoa ya Tanzania, lakini pia ni kinyume cha dini zetu tunazoziamini hapa tunasema unakuwa unafanya dhambi ya uzinzi. Haifai tunamwuzi mwumba na pia tunavunja sheria ya nchi.
Lakini ushauri wangu wa leo ni kuwa chepuka kakangu, chepuka dadayangu lakini ole wako uchepuke na rafiki kipenzi wa mwenza wako. Yaan mpenzi wako akijua umekuja kufanya mapenzi na rafiki yake kipenzi amini usiamini hatokuja kukusamehe kamwe katika maisha yake yote. Naongea hivyo maana nimeshuhudia kijana mmoja alilala na rafiki wa mke wake yapata miaka sita sasa imepita mke wake bado anasononeka anasema bora angelala na mwanamke yeyote lakini si rafiki yangu. Mke wake amekuwa akiwatongoza marafiki wa mme wake lengo awe analipa kisasi kafanya hivyo mara kadhaa lakini bado ile hali haijamtoka kichwani ndipo nilipogundua kuwa ni pigo kubwa kufanya mapenzi na rafiki wa mwenza wako.
Nilivyoiona hali hii nikasema nije nitoe ushauri huu kwa wanajopu wenzangu ili kwa namna moja au nyingine inaweza saidia baadhi ya watu na ushauri huu ukawa unazunguka kichwani kila akitaka kufanya mambo kama haya akakukumbuka kidonda atakachomwachia mwenza wake hakitopona milele. BAKI NJIA KUU MICHEPUKO SI DILI.
Watu wengi wanayotabia ya kuchepuka, neno hili kuchepuka limechukua matumizi badala ya neno usaliti. Namainisha mwanaume anaweza kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanamke mwingine ile hali anamke wake, au anampenzi wake mwenye lengo la kumwoa. Hali kadhalika vivyo vivyo kwa mwanamke.
Kwanza ifahamike kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria ya ndoa ya Tanzania, lakini pia ni kinyume cha dini zetu tunazoziamini hapa tunasema unakuwa unafanya dhambi ya uzinzi. Haifai tunamwuzi mwumba na pia tunavunja sheria ya nchi.
Lakini ushauri wangu wa leo ni kuwa chepuka kakangu, chepuka dadayangu lakini ole wako uchepuke na rafiki kipenzi wa mwenza wako. Yaan mpenzi wako akijua umekuja kufanya mapenzi na rafiki yake kipenzi amini usiamini hatokuja kukusamehe kamwe katika maisha yake yote. Naongea hivyo maana nimeshuhudia kijana mmoja alilala na rafiki wa mke wake yapata miaka sita sasa imepita mke wake bado anasononeka anasema bora angelala na mwanamke yeyote lakini si rafiki yangu. Mke wake amekuwa akiwatongoza marafiki wa mme wake lengo awe analipa kisasi kafanya hivyo mara kadhaa lakini bado ile hali haijamtoka kichwani ndipo nilipogundua kuwa ni pigo kubwa kufanya mapenzi na rafiki wa mwenza wako.
Nilivyoiona hali hii nikasema nije nitoe ushauri huu kwa wanajopu wenzangu ili kwa namna moja au nyingine inaweza saidia baadhi ya watu na ushauri huu ukawa unazunguka kichwani kila akitaka kufanya mambo kama haya akakukumbuka kidonda atakachomwachia mwenza wake hakitopona milele. BAKI NJIA KUU MICHEPUKO SI DILI.