Kuwa na misingi isiyokubalika katika dini ni miongoni mwa sababu zinazokubalika kwa mwanamke wa kiislam kutoa katika ndoa.
Mimi nahisi akae chini na mumewe na amueleze wazi kwamba amemjua ni muuza unga, hivyo aache hiyo biashara. Asaaa kheri mume anaweza akamuelewa wakaendelea na maisha mengine.
Ikiwa mume atakataa, namshauri ajiondoe kwenye hiyo ndoa haraka sana. Litakapokuja kubumburuka basi jamaa na mkewe na mtoto wao wataingia kwenye balaa kubwa sana.
Na wewe pia mtoa mada ndugu yangu nyakati zimebadilika. Angalia namna ya kuachana na hii ID maana wakikutafuta uisaidie jamhuri kuwaonyesha hugo rafiki ili wampate mumewe basi na wewe washakupotezea muda wako.