Ushauri na Maelekezo

edifice

Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
58
Reaction score
21
Habari ndg wana JF, ninakuja kwenu kuomba mnijuze taratibu za ununuzi wa chombo cha moto unafanyikaje, ni vitu gani vya kuzingatia ili kuepuka matatizo yasiyo ya lazima ya 'Sikujua'natanguliza shukrani wakuu
 
Chombo cha moto unamaanisha piki piki, gari, bajaji, au bunduki?
 
Hata AK 47 ni chombo cha moto mkuu
Sema ni nini unataka kununua
Kila mtu ame experience kweny sekta yake
Wengine magari wengine pikipiki wengine bajaji
 
Una miradi yako inayokuingizia hela?

Usikimbilie kununua gari kama huna hela ya maana. Usitegemee mshahara kununua wese.

Jipange fresh utaenjoy gari.
 
Una miradi yako inayokuingizia hela?

Usikimbilie kununua gari kama huna hela ya maana. Usitegemee mshahara kununua wese.

Jipange fresh utaenjoy gari.

Kuna watu watasema unaroho mbaya, wachache sana watakuelewa. Ulichokiongea akiufuata huo ushauri hatojuta.
 
Ushauri wenu nauzingatia, kuna ka Starlet kanauzwa nimekuwa interested kwa leo ningependa kujua ni namna gani mauziano yanafanyika
 
Kuna watu watasema unaroho mbaya, wachache sana watakuelewa. Ulichokiongea akiufuata huo ushauri hatojuta.
Mkuu niliposema ushauri nilimaanisha vitu vya kufanya wakati wa manunuzi kuhusu matumizi hilo ni suala jingine'Mtoto wa nyoka hafundishwi kuuma'
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…