Ushauri: Mpenzi wa zamani katuma ujumbe kwenye simu yangu, mke hataki kunielewa

Mtanzanyika

JF-Expert Member
Feb 12, 2015
368
425
Habari za jioni wana MMU,

Mimi ni mfanyakazi katika benki moja maarufu nchini, nafanya kazi katika moja ya matawi yake mkoani Mwanza. Nimeoa na nimebahatika kupata watoto wawili. Mke wangu ni mtumishi wa umma yeye ni mwalimu wa moja ya shule za Sekondari hapa mkoani Mwanza.

Sasa kuna msichana mmoja niliwahi ku-date naye kipindi hiko nipo Chuo kikuu cha Mzumbe, miaka 7 iliyopita. Yeye alikuwa anasoma LLB kwa bahati mbaya aka-disco first year, kwa kuwa wazazi walikuwa vizuri kifedha akaenda kusoma chuo Marekani. Sasa alivyoenda kule tukawa bado tunawasiliana, yeye alisoma Bachelor na kuunganisha na Masters moja kwa moja.

Tuliendelea kuwa na mawasiliano kwa takribani miaka 2 then baadaye mawasiliano yakapungua taratibu na baadaye kukatika kabisa.
Sasa siku ya Ijumaa kuu nikiwa kanisani kwenye ibada wakati wa kuabudu msalaba nikamuona huyo msichana, nilistuka sana kwa kweli maana sikutegemea kuonana naye.

Nikamfuatilia kwa macho mpaka nikafanikiwa kumuona mahali alipoketi, baada ya ibada kuisha nikajisogeza eneo alipo na kuonana naye, kwa kweli tulishangaana sana na kutoamini macho yetu kama tumeonana tena.

Tuliongea mambo mengi sana na kuahidiana kuonana Jumatatu ya Pasaka ili kuongea kwa kirefu. Tukaachana pale kanisani kwa kila mtu kuingia kwenye usafiri wake na kuondoka.

Sasa Jumamosi mke wangu akaniambia kuna rafiki yake anataka kuja Pasaka nyumbani maana ni miaka mingi hawajaonana na yupo Mwanza. Nikamuambia it's ok mkaribishe sana.

Basi J2 ya Pasaka nikiwa nimetulia nyumbani mke wangu akifanya maandalizi ya chakula huyo rafiki yake akaja, yaani wana MMU sikuamini macho yangu maana alikuwa ni yule yule ex - girlfriend wangu wa Mzumbe tuliyekutana kanisani, kila mmoja kati yetu alistuka sana na kupigwa na butwaa la ajabu, mpaka mke wangu akashtuka sana na kutuuliza kama tunafahamiana.

Ikabidi tumwambie ukweli kwamba tunafahamiana tulisomaga wote chuo Mzumbe, basi tukapiga story pale na kushinda naye kutwa nzima mpaka mida ya jioni alipotuaga na kurudi kwake.

Basi kesho yake Jumatatu ya pasaka tukaonana kama kawaida, tuliongea mambo mengi sana na akanipa hongera kwa kuwa na familia na akamsifu mke wangu kuwa ni mwanamke mwenye tabia njema sana.

Ila sasa nikashangaa sana aliponiambia kwamba bado ananipenda sana na anahitaji tuendelee kuwa wote japo mimi nina mke na watoto wawili. Mimi nikamuambia ni jambo ambalo haliwezekani coz tayari nina familia na ninampenda sana mke wangu na kumheshimu. Akaniambia nikafikirie vizuri then nimjibu baada ya kutafakari, tukaagana na kuachana pale kila mtu akarudi kwake.

Sasa nikafika nyumbani nikaweka simu yangu chumbani na mimi nikawa nipo sebuleni naangalia TV na wanangu. Mara simu yangu ikawa inaita mke wangu aliyekuwa chumbani anapanga nguo akaichukua akawa ananiletea sebuleni, jina limeandika la yule rafiki yake. Nikapokea na kuongea naye akawa ananiuliza kama nimefika salama nikamwambia ndiyo.

Nilivyomaliza kuongea naye mke wangu akaniomba simu yangu nikampa, kumbe akaichukua kuprove ile namba kama kweli ni ya rafiki yake, kwa bahati mbaya kulikuwa na sms mbili kumbe zimetumwa akafungua akazisoma moja ilisema "Nimefurahi sana kuonana tena na wewe leo nimekumbuka mbali enzi za Mzumbe tukiwa kwenye penzi moto moto, nilikumiss sana mpenzi, japo umeshaoa nazidi kukuomba usinisahau".

Ndugu wana MMU hivi ninavyoandika thread hii, tangu juzi mke wangu amenuna na hataki kabisa kuniongelesha wala kunisemesha. Nimejitetea vya kutosha mke wangu hataki kunielewa, nmemwambia hadi huyo ex - girlfriend wangu ampigie mke wangu na amuombe radhi lakini mke wangu bado hataki kunielewa kabisa. Anahisi bado natoka na huyo msichana na anahisi hiyo juzi tulienda kufanya mapenzi.

Naombeni ushauri wana MMU, nampenda sana mke wangu na sikuwahi kumvunjia heshima hata siku moja. Ebu nishaurini nifanye nini ndugu yenu, kazi haziendi ofisini, nipo na mawazo sana.
 
Umemweleza ukweli, hilo ni jambo jema. Endelea kumweleza ukweli huohuo, maana ukiongea ukweli hata mwili nao huudhihirisha huo ukweli.

Atakuelewa tu japo siyo lazima iwe ndani ya siku moja.

Wengine huwa mioyo yao inafunguka taratibu, hivyo nakuaihi endelea tu kuukazia ukweli wako na usitumie nguvu au haraka.

Pole sana mkuu.
 
Duh! Kweli uko na mke mwenye uvumilivu na mstaarabu mno kwa ushahid wote huo bado bi mkubwa yupo hme anaendelea na shughuli zake ni kakuchunia tu..Wengine ungekuta unaomba ushauri hapa ni kwa jinsi gani utamfuata wife kwao tena ukiwa na rundo la wazee...Nikushauri kama kweli unampenda wife wako hutokubali mazoea ya kupitiliza na ulikosea sana kutokumaliza kila kitu ulipokaa na huyo babyz wa chuo ungeweka wazi tu hadi aina ya mawasiliano ya akisi uclass mate tu na nothing more sababu huna moyo wa kupenda watu wawili na hauwezi kabisa kuwa nae..Sasa pambana na wife arudi line then piga stop kubwa huyo wa chuo aache mazoea...
 
Umemweleza ukweli, hilo ni jambo jema. Endelea kumweleza ukweli huohuo, maana ukiongea ukweli hata mwili nao huudhihirisha huo ukweli.

Atakuelewa tu japo siyo lazima iwe ndani ya siku moja.

Wengine huwa mioyo yao inafunguka taratibu, hivyo nakuaihi endelea tu kuukazia ukweli wako na usitumie nguvu au haraka.

Pole sana mkuu.
Nashukuru sana kwa ushauri wako Mkuu., nitaendelea kusimama katika ukweli. Nampenda sana mke wangu
 
Duh! Kweli uko na mke mwenye uvumilivu na mstaarabu mno kwa ushahid wote huo bado bi mkubwa yupo hme anaendelea na shughuli zake ni kakuchunia tu..Wengine ungekuta unaomba ushauri hapa ni kwa jinsi gani utamfuata wife kwao tena ukiwa na rundo la wazee...Nikushauri kama kweli unampenda wife wako hutokubali mazoea ya kupitiliza na ulikosea sana kutokumaliza kila kitu ulipokaa na huyo babyz wa chuo ungeweka wazi tu hadi aina ya mawasiliano ya akisi uclass mate tu na nothing more sababu huna moyo wa kupenda watu wawili na hauwezi kabisa kuwa nae..Sasa pambana na wife arudi line then piga stop kubwa huyo wa chuo aache mazoea...
Nimekuelewa mkuu., ndo ninachopambana hicho. Kuhusu huyu ex - girlfriend nimeshampiga marufuku kuwasiliana na mimi. Najuta hata kukutana naye kanisani.
 
Duh! Kweli uko na mke mwenye uvumilivu na mstaarabu mno kwa ushahid wote huo bado bi mkubwa yupo hme anaendelea na shughuli zake ni kakuchunia tu..Wengine ungekuta unaomba ushauri hapa ni kwa jinsi gani utamfuata wife kwao tena ukiwa na rundo la wazee...Nikushauri kama kweli unampenda wife wako hutokubali mazoea ya kupitiliza na ulikosea sana kutokumaliza kila kitu ulipokaa na huyo babyz wa chuo ungeweka wazi tu hadi aina ya mawasiliano ya akisi uclass mate tu na nothing more sababu huna moyo wa kupenda watu wawili na hauwezi kabisa kuwa nae..Sasa pambana na wife arudi line then piga stop kubwa huyo wa chuo aache mazoea...

Awesome advice.. Follow this advice .. Thanks..
 
Nimekuelewa mkuu., ndo ninachopambana hicho. Kuhusu huyu ex - girlfriend nimeshampiga marufuku kuwasiliana na mimi. Najuta hata kukutana naye kanisani.
That's good if una msimamo stay na familia yako.. Stay away from that Snake... Una uhakika gani kama yeye hana mtu wake mwingine huko... She just wants kuvuruga nyumba yako.. I just don't get it why a woman with respect na akili timamu wants to have a relationship with somebody else's husband ..

This is crazy.. Hivi kwani wanaume / wanawake wote wameisha hadi mume / mke was MTU... Sipendi Exes because most of them are mess waliopagawa na maisha baada ya kuwashinda... Nachukiaaaa..... Focus on your family , dear... Usithubutu kummpa chance aisogelee family yako wala mkeo ,snake mkubwa huyo Dada... Tena avunje hata relationship yake na mkeo.. Asije akafanya another crazy thing ya kuwachonganisha.. Because people like that wakiona wameshindwa plan ya kwanza, wanaenda kutafuta plans nyingine za ku destroy, to steal and to kill ... Women like that , I call them a psychopathy...

Thanks..
 
Endelea na msimamo wako huo wa kumpenda mkeo na kutomsaliti... Huyo x usiendekeze ukaribu nae sio mtu mzuri kwa ndoa yako. Naamini mkeo atakuelewa na amani itarudi tena,mpe muda tu
Nashukuru sana Valentina.! Kwa kweli ukaribu naye nimeuvunja kabisa., maana nimemuona kama shetani aliyekuja kuvuruga ndoa yangu.
 
That's good if una msimamo stay na familia yako.. Stay away from that Snake... Una uhakika gani kama yeye hana mtu wake mwingine huko... She just wants kuvuruga nyumba yako.. I just don't get it why a woman with respect na akili timamu wants to have a relationship with somebody else's husband ..

This is crazy.. Hivi kwani wanaume / wanawake wote wameisha hadi mume / mke was MTU... Sipendi Exes because most of them are mess waliopagawa na maisha baada ya kuwashinda... Nachukiaaaa..... Focus on your family , dear... Usithubutu kummpa chance aisogelee family yako wala mkeo ,snake mkubwa huyo Dada... Tena avunje hata relationship yake na mkeo.. Asije akafanya another crazy thing ya kuwachonganisha.. Because people like that wakiona wameshindwa plan ya kwanza, wanaenda kutafuta plans nyingine za ku destroy, to steal and to kill ... Women like that , I call them a psychopathy...

Thanks..
Umeongea point sana sana Mkuu. Nimekuelewa mno na nitayazingatia sana maneno yako. Nampenda sana mke wangu na siko tayari kumpoteza.
 
Back
Top Bottom